Mwita Maranya
JF-Expert Member
- Jul 1, 2008
- 10,564
- 7,973
Jamani,
Jerry Muro ameajiriwa TBC. Alilazimika kuondoka IPP Media (ITV), baada ya jitihada za kumzuia kwenda Marekani kwa kozi fupi kushindikana. Wakubwa zake ITV walijaribu kumzuia, bila ya sababu za msingi na ni kinyume cha jittihada za kuwaendeleza vijana, lakini waliomdhamini, Wamarekani wa USAID, walimpeleka baada ya kuona sababu za kumzuia ni "roho mbaya". Vivyo hivyo kwa kijana mwingine wa ITV, Sudi Mnette, ambaye naye walitaka kumzuia asiende Deutsche Welle, Sauti ya Ujerumani kwa kozi ya miezi sita, lakini akalazimika kuachana na ITV, kwa sababu kama za Jerry Muro na akaenda, akamaliza kozi, sasa ameajiriwa pia na TBC! Hayo ndiyo ya IPP Media na maendeleo ya vijana!
Bwassa
Ni kweli kabisa Bwassa,
Sudi Mnete amerudi toka Deutsche Welle sasahivi yuko TBC, kwa mtu anayefuatilia matangazo ya TBC atakuwa amemsikia au kumuona.Jery Muro naye ameshapata ajira TBC muda si mrefu ataanza kuonekana kwenye runinga ya TBC1.
Lakini suala la watangazaji mahiri kuondoka ITV/IPP sio suala geni, ni watu wengi sana wamekimbia, nadhani kuna tatizo la msingi IPP ambalo linahitaji kupatiwa ufumbuzi. Sasahivi taarifa za habari za ITV imeshakuwa ni kazi ya watu wawili, Nitwa na Chiku Lweno, sasa kwa kampuni kama IPP inakuwa inajiaibisha kwa kutolinda watangazaji wake tena hata wale mahiri.