Tetra
JF-Expert Member
- Oct 5, 2012
- 1,520
- 764
Suala uaminifu limeelekezwa kwa wapenzi ktk ndoa au nje ya ndoa.Wapo watu walio nje ya uhusiana fulani.Wao kila kukicha wanapanga,wanabuni mbinu za kila aina ili ampate mke/mme au mchumba wa fulani.Hadi kufikia kubainika na kuvunja uhusiano wa mtu.Kama mwizi umeingia ktk uhusiano huo na kuiba kitu kisicho mali yako.Na uondokapo unaacha aibu na uchungu ktk moyo wa uliyemdanganya na kumwachia hatia.Huu ni ukatili maana unajeruhi moyo,familia na unaweza kuleta madhara ukibainika.Hebu tujifunze kuheshimu uhusiano wa wenzetu Ni kweli,we ni bingwa wa kukubaliwa,unababaisha wengi,,basi JIHESHIMU ili tupunguze idadi ya wanaotendwa na wanaoangukia kwa wenzi wasio wao.Ndoa nyingi zinakosa amani kwa sababu mtu anaingia ktk ndoa akiwa na majeraha,,usilete Jeraha la moyo kwa watu ambao wana uhusiano.Usiende kutoa ushauri kabla hawajakuomba,,huwezi jua neno lako moja laweza kuharibu uhusiano wa watu.
Neno langu kwako usiwe chanzo cha Jeraha la moyo,kwani moto unaowasha kumchoma jirani yako hukuunguza zaidi wewe kuliko yeye.
Neno langu kwako usiwe chanzo cha Jeraha la moyo,kwani moto unaowasha kumchoma jirani yako hukuunguza zaidi wewe kuliko yeye.