Itakumbukwa kwamba walimu wamekuwa wakikatwa fedha kutoka kwenye mishahara yao midogo kwa ajili ya ujenzi wa jengo ambalo lilikamilika mwaka juzi, na linajulikana kama Mwalimu House. Lipo pale Ilala Boma. Jengo hili limepangishwa lakini haijulikani fedha zitokanazo na pango zinaingia kwenye mfuko gani, na walimu waliolijenga watanufaika vipi. Kuna wasiwasi kwamba fedha hizo zinaingia mifukoni mwa wajanja wachache. Mbaya zaidi ni kwamba walimu bado wanaendelea kukatwa fedha kwa ajili ya ujenzi. Ni ujenzi upi tena? Haieleweki. Wakuu wenye kufahamu undani wa jambo hilii wamwage data humu.