Wa Mjengoni
JF-Expert Member
- May 4, 2010
- 480
- 128
Jengo la Mackay House lililopo katikati ya mji wa Dodoma ni moja ya majengo makongwe kabisa ya mji huu. Jengo hili linamilikiwa na Diocese of Central Tanganyika. Kwa sasa jengo hili kwa nje ni chafu na halipendezi machoni kana kwamba watu wamehama Ofisi hizo. Tunaomba Uaskofu wa Central tanganyika ufanye lolote kulinusuru jengo hili ili mandhari ya mji wetu mkuu yaendelee kupendeza.