Jengo la Machinga: NSSF imekula hasara ya bilioni 30

Kwani hapakuwa na business plan. In modern society hivi bado kuna kampuni zinafanya biashara za kombolela.
 
Mnapiga makelele bureee kuhusu NSSF lakini kulingana na hali ya Dra sasa hivi NSSF ndiye ataibuka mshindi. Jengo lile halikujengwa vibaya bali wamegawa vipande ambavyo hata kuviondoa haitawagharimu kiasi kikubwa. Jengo hilo linaweza kubadilishwa na kuwa Mall au hata ofisi za mashirka binafsi na kadhalika, hivyo NSSF wamejipatia kiwanja na jengo bila hata kutoka jasho. Hasara ni kwa manispaa ya Ilala, hii inaonyesha uongozi mbaya wa Manispaa hiyo kujiingiza na kubariki swala la Umachinga.

Walichotakiwa wao kujiuliza ni kwa nini vijana wengi wamechukua Umachinga kama njia ya kujipatia ajira na wataweza vipi kupambana na Umachinga ikiw ni kero kwa Taifa naq vijana wenyewe. Hivyo, kilichotakiwa ni kupambana na nacho na sio kukipa uwezo zaidi. Kwanza, ni manispaa kuzalisha kazi nyinginezo ambazo zinaleta maendeleo zaidi kwa manispaa na vijana wenyewe.

Pili, wananchi wengi wanapenda kununua mali zao kwa Machinga kwa sababu hakuna sehemu moja kama Mall ambayo unaweza kupata kila kitu ukitakacho. Na kutokana na msululu wa magari Dar, traffic jam mtu huwezi kwenda mjini ukapata kila kitu, huwezi kwenda Kariakoo ukapata kila kitu, huwezi kwenda soko la Ilala ukapata kila kitu lakini unaweza pata vitu vingi kwa machinga barabani wakati ukielekea nyumbani au kazini..

Suluhisho ni kujenga Malls au sunday market kila manispaa ambapo wafanyabiashara wenye maduka ya vitu vya Machinga ndio wapewe sehemu hizo za duka ili kurahisisha wanunuzi kuweza kwenda jengo moja na kupata vitu vyote wavitakavyo.. One stop shopping waingereza wanasema. Na hao Machinga, wapeni kazi ya kusimamia parking za magari, kusafisha barabara, kuweka matangazo, kuchimba mitaro na kadhalika.. Ni muhimu kwa manispaa kufikiria kazi za kuwawezesha vijana wao waondokane na Umachinga na sio kuwabariki ktk umachinga..
 
Mnapiga makelele bureee kuhusu NSSF lakini kulingana na hali ya Dra sasa hivi NSSF ndiye ataibuka mshindi. Jengo lile halikujengwa vibaya bali wamegawa vipande ambavyo hata kuviondoa haitawagharimu kiasi kikubwa. Jengo hilo linaweza kubadilishwa na kuwa Mall au hata ofisi za mashirka binafsi na kadhalika, hivyo NSSF wamejipatia kiwanja na jengo bila hata kutoka jasho. Hasara ni kwa manispaa ya Ilala, hii inaonyesha uongozi mbaya wa Manispaa hiyo kujiingiza na kubariki swala la Umachinga.

Walichotakiwa wao kujiuliza ni kwa nini vijana wengi wamechukua Umachinga kama njia ya kujipatia ajira na wataweza vipi kupambana na Umachinga ikiw ni kero kwa Taifa naq vijana wenyewe. Hivyo, kilichotakiwa ni kupambana na nacho na sio kukipa uwezo zaidi. Kwanza, ni manispaa kuzalisha kazi nyinginezo ambazo zinaleta maendeleo zaidi kwa manispaa na vijana wenyewe.

Pili, wananchi wengi wanapenda kununua mali zao kwa Machinga kwa sababu hakuna sehemu moja kama Mall ambayo unaweza kupata kila kitu ukitakacho. Na kutokana na msululu wa magari Dar, traffic jam mtu huwezi kwenda mjini ukapata kila kitu, huwezi kwenda Kariakoo ukapata kila kitu, huwezi kwenda soko la Ilala ukapata kila kitu lakini unaweza pata vitu vingi kwa machinga barabani wakati ukielekea nyumbani au kazini..

Suluhisho ni kujenga Malls au sunday market kila manispaa ambapo wafanyabiashara wenye maduka ya vitu vya Machinga ndio wapewe sehemu hizo za duka ili kurahisisha wanunuzi kuweza kwenda jengo moja na kupata vitu vyote wavitakavyo.. One stop shopping waingereza wanasema. Na hao Machinga, wapeni kazi ya kusimamia parking za magari, kusafisha barabara, kuweka matangazo, kuchimba mitaro na kadhalika.. Ni muhimu kwa manispaa kufikiria kazi za kuwawezesha vijana wao waondokane na Umachinga na sio kuwabariki ktk umachinga..

Bob Mkandara.
Ni kweli kama unavyosema yale majengo pale Ilala walichokosea ni kuweka vile vibanda ndani ya majengo nani atakuja kuweka bidhaa zake kwenye kizimba cha nyavu cha futi 3.

Pale wakiamua kukata flam za futi sita kwa sita kwa bei ya laki 5 kwa mwezi ndani ya wiki mmoja patakuwa pamejaa.

Tatizo Jiji watataka kuwalizimisha wachuuzi kuwa wafanya biashara.
 
Last edited by a moderator:
Maachinga Complex Mimi Nashauri ibadilishwe Matumizi tu ili kuepuka Gharama zaidi. Hapafai kufanyia Biashara kwa sababu ni Mpuuzi gani atakayeweka Soksi au T-shirt au Suruari au Hand kerchief kule Ghorofani wakati kuna wengine wameweka same bidhaa, same price ground floor? Aliyebuni ule Mradi anapaswa Kushtakiwa kwa sababu hakulishauri shirika vizuri hali iliyopelekea kupata Hasara kubwa
 
NSSF wanataka wafilisi kabisa ule mfuko kwa kujiingiza katika uwekezaji ambao kamwe hautaweza kurudisha hela za wanaochangia institution hiyo. Inauma sana! Lakini chakufanya wala hatukioni sisi tunaochangia mfuko huo. Ni wizi tuuuu yaani mpaka sasa inachosha.
 
Labda kama kuna mtu anaweza kutusaidia swali moja; NSSF inaongozwa na sera au taratibu gani kabla ya kuamua kuwekeza fedha za mfuko huo kwenye miradi mbalimbali? Kwa mfano, ni kitu gani kiliwafanya watoe fedha kwa mradi huu wakiamini kuwa utawarudishia faida?

Mkuu swali zuri sana umeuliza. Mimi ni mwanachama wa NSSF ninachoona ni kuwa mfuko huu umekosa utawala bora. kwa utaratibu wa utawala bora wa makampuni (corporate governance) NSSF kama shirika la kijamii lilipaswa kuwa na mambo yafuatayo. 1. Kuwa na mwongozo au sera ya uwekezaji iliyo wazi na kujulikana na wanachama.

2. Wajumbe wa Bodi ya wakurugenzi wanapaswa kuwa wanawajibika kwa wanachama wa mfuko na bunge, na mkurugenzi mkuu (CEO) anapaswa kuwa anawajibika kwa Bodi ya wakurugenzi sio kwa Waziri wala Rais.

3. Mkurugenzi mkuu apewe mkataba wa muda mfupi mfano miaka mitatu au mitano na mkataba unapaswa kupitiwa kila mwaka kuangalia ufanisi wake. Wakurugenzi wengine wachaguliwe kila mwaka.

4. Mishahara na marupurupu yote ya wakurugenzi iwe inawekwa wazi na kujulikana. Malipo yao pia yatokane na ufanisi katika kuendesha mfuko si vinginevyo.

5.Sheria iruhusu vyama vya wafanyakazi na wanachama kuwa na uwezo wa kuwashitaki wakurugenzi kwa kuvunja wajibu wa kufanya kazi kwa maslahi ya mfuko (fiduciary duty to act in the best interests of the Fund). Hii itafanya wakurugenzi waogope kufanya maamuzi ya ajabu katika uwekezaji maana wataweza kushitakiwa wao kwa majina yao na kulipishwa fidia kwa hasara waliosababisha.

6.Akaunti zilizokaguliwa ziwekwe wazi kwa wanachama.

7. Sehemu zote wanakowekeza kuwe kunatangazwa na kuwe na kiwango maalumu cha uwekezaji katika mradi mmoja mfano wanaweza sema wasiruhusiwe kuwekeza zaidi ya bilioni 20 katika mradi mmoja.

Kwa maoni yangu mambo hayo juu yanapaswa kufuatwa ili mifuko hii iendeshwe kwa ufanishi. Kinachotokea sasa ni utawala mbovu na kwa kuwa sheria zinazoanzisha mashirika haya ni mbovu, serikali na wakurugenzi wa mashirika wanatumia nafasi hiyo kujineemesha, na kufanya maamuzi yasiyo sahihi.
 
tumeona issue ya uwekezaji wa NSSF Dodoma na huku kwingine; nadhani watu wanatakiwa kuwa waangalifu hasa mifuko hii inaposukumizwa kuwekeza
Huu sio "uwekezaji" wa NSSF, bali mkopo, liability ya NSSF iko hedged with collateral ya ardhi ya Jiji.

Kwenye "uwekezaji" the capital is not collateralized.

Lets get the issues right, please.
 
Wenzutu wanakazania kujenga Malls sisi tutajenga vibanda vya kuku, Si afadhali wangejenga Mall hiyo bilioni 30 kama hii hapa kuliko kufanya ufisadi. Aliyetoa aidia ya kujengwa Machinga Complex hakuwa na akili timamu hata NSSF hawakuangalia kwa undani walichofikiria wao ni kupiga pesa ya kiufisadi sasa imekula kwao

Menlynmall23.JPG


mall.jpg


menlyn mall.jpg
 
Huu sio "uwekezaji" wa NSSF, bali mkopo, liability ya NSSF iko hedged with collateral ya ardhi ya Jiji.

Kwenye "uwekezaji" the capital is not collateralized.

Lets get the issues right, please.

wrong. Serikali inasema ni uwekezaji! au hujasoma ripoti ya CAG uone wanavyopishana kati ya Serikali na NSSF. Ingekuwa mkono kungekuwa na mkataba wenye kusema hivyo...
 
wrong. Serikali inasema ni uwekezaji! au hujasoma ripoti ya CAG uone wanavyopishana kati ya Serikali na NSSF. Ingekuwa mkono kungekuwa na mkataba wenye kusema hivyo...

Mkuu,

Hebu nionyeshe wapi waliwekeza initial capital investment kama NSSF katika report ya CAG. Kumbuka madai yako unaassume kuwa NSSF ndio mwenye kumiliki hilo Jengo wakati mie ninavyofahamu ule ni mkopo waliopewa Manispaa ya ilala na Jiji wakajenge utumbo wao. NSSF lazima watakuwa wamepata guarantee ya serikali nitashangaa sana ikiwa watakuwa wametoa huo mkopo bila ya guarantee ya serikali kuwa kama mkopo hautaweza kulipwa serikali italipa deni lote pamoja na riba. Ni vema utupatie mchakato mzima wa mkataba baina ya jiji na NSSF before starting accussing something Mwanakijiji!!
 
Mstahiki meya wa Ilala anapaswa kuja kutupa maelezo ya kina, hapa kuna ulaji tu watakaothirika ni wanachama wa NSSF; ipo siku NSSF itashindwa kuwalipa wanachama wake mafao; jiji haliwezi kuwaweka machinga sehemu kwani linaudhaifu mkubwa wa kusimamia sheria ilizozitunga; mpango mzima wa kujenga ilitaliwa na ufisadi.

Chama
Gongo la Mboto DSM
 
Hakukuwa na business plan, kilichokuwepo ni siasa na umaarufu wa haraka haraka. Rais Kikwete hakushauriana na mtaalam yoyote kama alivyogawa bilioni 21 hovyo

NSSF hawakutumia wataalam kutathmini huo uwezekezaji. Walichofanya ni kumfurahisha Rais ili kila mtu abaki na utamu wake. Hivi hii mifuko ya umma haiwezi kuendeshwa bila uingiliwaji na serikali?

Halmashauri ya jiji na hasa manispaa ya Ilala haikujua nini cha kufanya. Hakuna mtaalam aliyetumika kufanya tathmini.

Meya wa manispaa ya Ilala naye hajui nini wananchi wake wanahitaji na kwanini. Amekubali mradi unaokufa kabla ya kuanza. Tena huyu ni meya Kijana tuliyetegemea mawazo tofauti.

Matumizi ya fedha za watu kwa uwekezaji wa namna hii ni hasara na hatari kubwa.
Fedha zilizojenga Machinga complex zingeweza kuwekezwa kwa kujenga nyumba za bei nafuu na kuwakopesha wanachama kwa mikopo nafuu. Kwanini mwanachama wa NSSF akope CRDB au NBC? Vipi kama angekopa kwenye mfuko anaochangia

Suluhisho si kuwajengea wamachinga eneo ni kutafuta chanzo kwanini wanazidi kujaa mjini, na je kwa kuuza shati 3 kwa siku mtu anamudu vipi maisha.
Kwanini usiwepo mbadala wa wao kutumia nguvu zao kuzalisha na si kuuchuza
 
Ni kituko kweli kweli. Inakuwaje fisadi kama Manji anapata pesa ya kuilipa NSSF lakini jiji linashindwa? Of course mchwa na watendaji kufikiri kwa masaburi. Masaburi mwenyewe ulaji mtupu na past yake utata mtupu. Kughushi na mambo mengine. Ulitegemea watu kama hawa wanaoendekeza dili wafanye kitu kinachoingia akilini. Jiji lina pesa sema inaishia kwenye mifuko ya wezi waliokabidhiwa jiji.
 
NSSF inao wasemaji wake humu

nashangaa wako kimya vipi?

zipo namna ya kuwachokonoa. mtawaona watakuja humu na moto kweli kweli
 
Huku ndo kunaitwa kukurupuka.

Hivi jengo hili lilijengwa baada ya utafiti wa kibiashara au ilikuwa ni matamko ya kisiasa?

Siyo kila biashara inafaa katika kila space.

Matatizo ya kiuchumi hayafumbuliwi kwa majibu ya kisiasa.

Wengi tunadahi kushindwa kwetu kwingi kunatokana na ukosefu wa fedha, ukweli ni kwamba ni ukosefu wa ubnifu na kufuata kanunni za biashara.

Ila kwa sababu hatujifunzi kila tufanyapo makosa naamini kabisa mradi huu utarudiwa tena mahali pengine
 
Nikiliangalia lile jengo huwa nashangaa sana wale walioshauri kuweka vile vizimba ndani ya jengo.

Binafsi naona jengo halina kasoro ingawa sijwahi kuingia mle ndani...
Kwa wale wenzangu na mimi ambao washawahi kufika China hasa miji ya Guangzhou, Yiwu na hata Hong Kong watakubaliana na mimi kuwa kule wenzetu wana majengo kama yale ambayo watu hufanya biashara huria na huko kwenye hayo majengo ndio wengi wetu ukisikia tumeenda China kibiashara ndio tunakoenda kuokoteza bidhaa.
Ukienda Guangzhou kwa mfano pale Caanan(Jianan), Tianshu baadhi ya maeneno ya Shamshuipo kule HongKong ni mithili wa hayo majengo ya Machinga Complex.
Binafsi nafikiria serikali ya manispaa ya Ilala ije na moja ya mikakati ifuatayo:
1. Wageuze matumizi ya yale majengo badala ya kuwa ya wauzaji wadogowadogo(machinga), badala yake wawekwe wauzaji wa jumla.
2. Kwa maelezo ya MMM,yale majengo yanatakiwa kujiendesha kibiashara, hivyo manispaa inabidi kuyatangaza ili umma ujue kwa wingi.
3. Moja ya masoko haya(Karume na Boma) kama si yote, inabidi manispaa iyaue au iyaamishie Machinga.
 
Aulizwe JK manake yeye ndio ilikuwa sera yake hiyo kwa Ilani ya chama cha magamba na si mwingine yeyote yule na ikumbukwe aliahidi Meli kila Ziwa alipokuwa anaenda kwenye Kampeni zake mwaka 2010.
 
Labda kama kuna mtu anaweza kutusaidia swali moja; NSSF inaongozwa na sera au taratibu gani kabla ya kuamua kuwekeza fedha za mfuko huo kwenye miradi mbalimbali? Kwa mfano, ni kitu gani kiliwafanya watoe fedha kwa mradi huu wakiamini kuwa utawarudishia faida?

Political push without Thinking!! and DAU is also a politician
 
Back
Top Bottom