Jengo jipya la ubalozi DC - Dola milioni 10?

Nafikiri ni wazo zuri. Jengo lenyewe ni orofa sita. Liko katikati ya mji, karibu na Georgetown na K Street ambayo ni maeneo ya biashara, maofisi makubwa ya lobbyists na lawyers wa Washington. Ubalozi utatumia orofa tatu na zile tatu zitapangishwa. Kwa hiyo in time hizo hela zitarudi.
 
kwa mujibu wa experience yangu,
investing in CONSTRUCTION PAYS A LOTS
Year its true but ishu inakuja palepale pesa zitatufikia wadanganyika? maana kila kitu kama kinatumika ipasavyo hua kinalipa hata "Migodi" na "maliasili" kibao zinalipa ila tu Mshiko unaishia kwa wajanja!!
 
I'm a bit skeptical about this...but I can't put my finger on why I feel this way...let me try to get some more details
 
jengo la bilion 10 kwa nchi kama tz ambayo majority ya wapiga kura wanaishi chini ya dola moja kwa siku.ama kweli priorities
 
mimi nadhani ni safi kuinvest kwenye majengo, lakini nina wasi wasi isije ikawafaidisha mafisadi tu na wale walala hoi wakaishia kuona kwenye makaratasi tu
 
Year its true but ishu inakuja palepale pesa zitatufikia wadanganyika? maana kila kitu kama kinatumika ipasavyo hua kinalipa hata "Migodi" na "maliasili" kibao zinalipa ila tu Mshiko unaishia kwa wajanja!!
now,thje highlighted item is ANOTHER CUP OF TEA!.......and it needs a lots of explanations and justifications
 
Kama kuna uwezakana wa kuongeza ufanisi wa majengo haya basi itakuwa vizuri, Kenya wana ofisi za kibalozi nyingi zaidi lakini sisi bado, Hatuwezi kupiga hatua kubwa ya maendeleo na kama hatakuwa na ofisi zetu za kibalozi, Kuendelea kukodisha majengo haya kwa pesa nyingi afadhali kujenga sisi mwenyewe kuwa mali zetu, kwa hiyo ni kitu kizuri
 
nimechwa na kila siku kutaja mabaya ya rais wetu Mh JK pamoja na timu yake nzima........but hata hili la kupiga picha ni baya jamani?
Kwasababu kama ni rais mwenye picha JK anaongoza.....samahani kwa kutoka nje ya mada.....lol
Mazungumzo baada ya habari
 
nimechwa na kila siku kutaja mabaya ya rais wetu Mh JK pamoja na timu yake nzima........but hata hili la kupiga picha ni baya jamani?
Kwasababu kama ni rais mwenye picha JK anaongoza.....samahani kwa kutoka nje ya mada.....lol
Mazungumzo baada ya habari
NI NZURI KAMA UTAKUJA NA THREAD YAKO MPYA!hapa unatuharibia moods wengine,nisije nikazihamishia hasira zangu kwako bure mkuu!
 
Binafsi naunga mkono ununuzi wa jengo hilo na hakika nitasema kwamba huwezi kuelewa thamani ya kitu kama huishi maeneo hayo..
Jamani leo hii Kariakoo nyumba za vyumba sita zinauzwa hadi millioni moja, sidhani kama kuna mmoja wetu anaweza kuona faida ya ununuzi kama huo kama huelewi kinachoendelea... Wapo watu huko Tz leo wanaingia mkataba wa kujenga maghorofa na mwenye kiwanja akapewa top floor kisha baada ya miaka 10 nyumba inarudi kwa mwenye kiwanja.. Hii yote haiwezi kuingia akilini kwa mtu asofahamu pato la kupangisha kwa miaka 10 maeneo ya Kariakoo.

Hivyo mjue tu kwamba jumba lililonunuliwa DC,lipo mjini eneo ambalo zipo condo au office zinauzwa hadi millioni iweje jengo zima la ghorofa 6 iwe ghali sana kununuliwa kwa millioni 10. Mlitaka linunuliwe kwa kiasi gani?
Idd Amin alinunua jengo New York mwaka 72 dunia nzima wakamwona kichaa leo hii thamani ya jengo hilo hilo ni mara 10. Na nchi kibao zimefuata mfano wa kichaa yule, wananunua kama hawana akili si jengo la Ubalozi tu hata nyumba za wawakilishi wao wa kudumu huko UN nyingi zimenunuliwa.

Kwa hiyo tusiwe wapuuzi sana ktk investment, leo Mchina anakuja nchini kununua nyumba Kariakoo tunalia nao iweje tena sisi kununua nyumba Marekani iwe issue...au mmesahau mamillioni ya kodi zenu yanayotumika kila msafara wa viongozi wetu toka wakati wa Mkapa...
 
..je, ununuzi wa jengo la ubalozi ulikuwepo kwenye ahadi za uchaguzi za JK?

..fedha walizonunulia hilo jengo la ubalozi wangeweza kujenga maabara na maktaba ktk shule zote za wilayani kwetu.

..binafsi naona watoto wetu kule kijijini kuwa na maabara na maktaba ni muhimu kuliko huo ubalozi.
 
Jamani leo hii Kariakoo nyumba za vyumba sita zinauzwa hadi millioni moja, sidhani kama kuna mmoja wetu anaweza kuona faida ya ununuzi kama huo kama huelewi kinachoendelea... .

Mkandara, au utaka kuandika milioni mia moja? Maana bei za Kariakoo hazikamatiki ..
 
jengo la bilion 10 kwa nchi kama tz ambayo majority ya wapiga kura wanaishi chini ya dola moja kwa siku.ama kweli priorities

Je, hizo shilingi bilioni 10 ni ngapi zitaingia mifukoni mwa mafisadi? Tusishangae baada ya ujenzi wa jengo hilo kwisha tukaambiwa kutokana na kupanda gharama za ujenzi gharama halisi za jengo hilo ni shilingi bilioni 40, msisahau yaliyotokea kwenye ujenzi wa Twin Towers maana Tanzania ndiyo inaliwa hivyo ati! na mafisadi.
 
Je kuinvest kwenye real estate kwenye soko la DC ni wazo zuri? Litalipa?

Kulipa ni lazima.
Tusiwe na mawazo ya kufikiria kimaskini,nimetembelea DC na nimekuta Balozi nyingi ziko uchochoroni.
Washington DC haitetereki kesho wala mtondogoo hivyo hii investment is of good value.
 
Dah bado tunasafari ndefu saaana kufikia malengo.

Naam kwa maoni yangu kuna priorities ambazo zina umuhimu mkubwa zaidi ya kujenga ofisi ya ubalozi DC. Kwa mfano majengo ya shule zetu ambazo nyingi hayana hata hadhi ya kuitwa shule. Wanafunzi wa shule nyingi bado wanakaa chini au kuboresha drainage system ya Dar ambayo kwa sasa ni hovyo kabisa maana mvua kubwaya dakika 20 tu basi mafuriko kila kona ya jiji. Hizo bilioni 10 zingeelekezwa huko nadhani zingekuwa na matokeo mazuri sana badala ya kujenga jengo ambalo lazima gharama zake zitagubikwa na ufisadi wa hali ya juu. Tusubiri kama hizo gharama tunazoambiwa sasa hazitaongezeka mara tatu au hata zaidi jengo hilo litakapokwisha.
 
Back
Top Bottom