Jamani naitafuta makala hii ya Jenerali Ulimwengu. Ilitoka katika jarida la Rai ikiwa na sehemu kama tatu au nne. Ilikuwa ni barua ndefu fulani ikielezea jinsi Ulimwengu alivyomfahamu Jakaya Kikwete tangu enzi za Umoja wa Vijana wa TANU. Hivi Ulimwengu alizungumzia nini zaidi katika barua ile ndefu. Mwenye nayo atuingizie humu.