Jenerali Mboma aendelea kuula TPDC

Ng'wanza Madaso

JF-Expert Member
Oct 21, 2008
2,268
333
Jenerali Mboma aendelea kuula TPDC




Na Mwandishi wetu



16th September 2009







Mboma.jpg

Jenerali Mstaafu, Robert Mboma.




Rais Jakaya Kikwete amemteua tena Jenerali Mstaafu Robert Mboma kuendelea kuwa mwenyekiti mpya wa Bodi ya Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) kwa kipindi cha miaka mingine mitatu.
Kikwete amemteua Mboma, aliyekuwa mkuu wa majeshi wakati wa uongozi wa Serikali ya awamu ya tatu kuendelea na wadhifa huo kuanzia Julai mwaka huu hadi Juni mwaka 2012.
Taarifa iliyotolewa na Msemaji wa Wizara ya Nishati na Madini Alyoce Tesha, inasema kufuatia uteuzi huo, Waziri wa Wizara hiyo, William Ngeleja amewateua wajumbe tisa kuunda bodi hiyo.
Wajumbe hao ni Emanuel Ole Naiko ambaye ni Mkurugenzi Mkuu wa Kituo cha uwekezaji, Ngosha Magonya, Kamishna wa Fedha za Nje wa Wizara ya Fedha na Uchumi, Maduka Kessy Meneja Uhusiano wa Sekta Binafsi na Serikali kutoka Shirika la Maendeleo la Taifa(NDC), wabunge Gosbert Blandes (Karagwe) na Mudhihir Mudhihir (Mchinga)
Wengine ni Faida Bakari (Viti Maalumu), Prosper Victus Kamishna Msaidizi wa Mafuta na gesi wa Wizara ya Nishati na Madini, Mwalimu Mwalimu, Katibu Mkuu Wizara ya Maji, Ujenzi, Nishati na Ardhi (MUNA) Serikali ya Mapinduzi Zanzibar na William Haji (Mhasibu) ambaye ni Kaimu Mkurugenzi Mkuu, Shirika la Ndege Tanzania (ATC).




CHANZO: NIPASHE

Maoni yangu: Je nilini wazee watastaafu?. Ni nini maana ya neno kustaafu? Ni lini vijana watafanya kazi mchanganyiko na wazee? Ni lini wabunge wataendelea kuwa wawakilishi wa wananchi na baada ya Bunge kurudi majimboni mwao na kuwahudumia wananchi ana kwa ana badala ya kuendilea kuwepo mjini kwa sababu wanahudhuria vikao vya bodi?
 
Maoni yangu: Je nilini wazee watastaafu?. Ni nini maana ya neno kustaafu? Ni lini vijana watafanya kazi mchanganyiko na wazee? Ni lini wabunge wataendelea kuwa wawakilishi wa wananchi na baada ya Bunge kurudi majimboni mwao na kuwahudumia wananchi ana kwa ana badala ya kuendilea kuwepo mjini kwa sababu wanahudhuria vikao vya bodi?

Hoja hiyo wana JF
 
Wana JF naomba kujua umri wa huyu mzee,kafanya kazi jeshini kwa miaka mingapi, Je ana chochote au ndio Raisi kamtembelea kaona maisha yake yote jeshini hakuwa fisadi kampa hiki angalau ajengee nyumba?
 
Kuna usemi kuwa Old soldiers never die...they just fade away. Nina shaka na huyu old soldier wetu. Does he fall into that category of old soldiers whose names refuse to die?
 
Nashindwa kuelewa jinsi serikali hii inavyofanya kazi; bungeni imeishazungumzwa na mawaziri wanapashwa kusikiliza na kuelewa kuwa kuna conflict of interest kwa wabunge kuwa wajumbe wa bodi za mashirika ya umma na ndio maana BOT imewatoa wote kutoka kwenye bodi za benki za umma. Sasa huyu Ngeleja sijui huwa haelewi kinachozungumzwa bungeni au yeye sio sehemu ya serikali iliyoona conflict of interest hii. Mawaziri kama Ngeleja hawamsaidii Rais kutekeleza utawala bora na hawafai kabisa kuwa mawaziri kwani wanaonyesha ukihiyo wao ingawa wanadigrii za sheria za kuchonga!!
 
Ngeleja is just another stupid fellow. Sijui hata hiyo degree aliipata wapi manake hana reasoning kabisa. Gen. Mboma anakashfa ya kununua helkopta na ndege za kijeshi zilizo choka, ana kashfa ya kununua vifaru hewa, ana kashfa ya meremeta, ana kashfa ya kuingiza silaha DRC kwa waasi kwa kumruhusu Victor Bout kupitishia silaha mwanza. n.k. leo wewe pumbavu ngeleja unampa uenyekiti wa bodi??

Yule ni mkuu wa majeshi mstaafu, anapata mbuzi wa bule kila mwezi, mshahara, ana gari la jeshi la kumhudumia, n.k. Hivi hakuna vijana nchi hii?? mbona kila mwaka watu wana graduate pale UDSM, Open, Mzumbe, SAUT, Tumaini, DIT, MIST, n.k. hakuna watu wa kuweza kuwa wajumbe wa bodi?? mpaka hiyo mizee tu????

Narudia tena Ngeleja uache uoga, na usidhani utafia madarakani, na narudia tena "You are stupid"
 
Nashindwa kuelewa jinsi serikali hii inavyofanya kazi; bungeni imeishazungumzwa na mawaziri wanapashwa kusikiliza na kuelewa kuwa kuna conflict of interest kwa wabunge kuwa wajumbe wa bodi za mashirika ya umma na ndio maana BOT imewatoa wote kutoka kwenye bodi za benki za umma. Sasa huyu Ngeleja sijui huwa haelewi kinachozungumzwa bungeni au yeye sio sehemu ya serikali iliyoona conflict of interest hii. Mawaziri kama Ngeleja hawamsaidii Rais kutekeleza utawala bora na hawafai kabisa kuwa mawaziri kwani wanaonyesha ukihiyo wao ingawa wanadigrii za sheria za kuchonga!!

Nakwambia Ngeleja, Masha , nchimbi, ni mawaziri vijana wapumbavu wanaotuaibisha sisi vijana. Sasa hivi tuna mgao wa umeme mikoa sita, wala huwezi kusikia lolote kuhusinana na juhudi za kutatua hilo tatizo. Jk nae at one time aliwahi kusema mgao wa umeme utakuja kuwa historia, sijui kama anaweza kurudia hayo maneno hadharani, labda kama hana aibu mkwere huyu.
 
Nakwambia Ngeleja, Masha , nchimbi, ni mawaziri vijana wapumbavu wanaotuaibisha sisi vijana. Sasa hivi tuna mgao wa umeme mikoa sita, wala huwezi kusikia lolote kuhusinana na juhudi za kutatua hilo tatizo. Jk nae at one time aliwahi kusema mgao wa umeme utakuja kuwa historia, sijui kama anaweza kurudia hayo maneno hadharani, labda kama hana aibu mkwere huyu.
Kaka umenena wacha vijana wahangaike wazee waendelee kuturudisha kwenye ukoloni wa enzi zile. Kwani nikimuuliza babu yangu kwanini huwa mkali anasema alisoma shule ya mkoloni. Je hii tuendelee kuikubali?
 
Mwalimu Mwalimu, Katibu Mkuu Wizara ya Maji, Ujenzi, Nishati na Ardhi (MUNA) Serikali ya Mapinduzi Zanzibar

Huyu nae anafanya nini humo? Si wameishatangaza kuwa wameitimua TPDC Zanzibar? Si aseme "Thanks but no thanks"! Lakini mbele ya vibahasha.........

Amandla.....
 
Back
Top Bottom