Ngambo Ngali
JF-Expert Member
- Apr 17, 2009
- 3,517
- 1,359
Pinda: Jembe la mkono sasa basi
Thursday, 13 May 2010 05:46
Na Mwandishi Wetu
Waziri Mkuu Mizengo Pinda amesema Kilimo cha jembe la mkono nchini sasa basi kwa vile kimeshindwa kuleta Mapinduzi ya Kilimo na badala yake lazima kutumia zana za kisasa na utalaamu.
Alikuwa akihutubia Mkutano wa hadhara katika Kijiji cha Mirumba, Kata ya Kibaoni, Tarafa ya Mpimbwe baada ya kukabidhi matrekta kwa vikundi vya wakulima katika siku yake ya nne ya ziara yake ya jimbo.
Jembe la Mkono siyo zana ya kutegemea kubadili maisha yetu Wenzetu wanalima kwa matrekata madogo na makubwa, wanapanda na kuvuna kwa matrekta majembe ya mkono yalitumika zaidi ya miaka 2,000 iliyopita, alisema.
Alikabidhi trekta moja kubwa kwa kikundi cha mbugani cha Kijiji cha Itenka; moja dogo kwa kikundi cha Jitume cha Kijiji cha Magamba na jingine dogo kwa kikundi cha Ufugaji Nyuki cha Kijiji cha Uruira.
Trekta kubwa aina ya Tafe, liliotengenezwa India, lina thamani ya sh. milioni 51 na wakulima wanatakiwa kuilipa Halmashauri ya Wilaya ya Mpanda sh. milioni 10 ambayo ni asilimia 20 ya gharama ambazo halmashauri hiyo iliingia kulinunua.
Trekta dogo aina ya Kubota la Japan wakulima hutakiwa kulipia sh. milioni 1.5, ikiwa ni Asilimia 10 tu ya bei yake.
Halmashauri ya Wilaya ya Mpanda tangu mwaka 2007/2008 imekuwa ikitekeleza agizo la serikali la kununua matrekta na kuyasambaza kwa wakulima kwa bei ya chini, ikiwa ni sehemu ya kuendeleza kilimo cha zana na cha kisasa.
Kwa mwaka huu wa fedha unaomalizika Mwezi ujao (2009/2010), Halmashauri ya Wilaya ya Mpanda ilipanga kununua matrekta madogo 36, kwa gharama ya sh. milioni 284 na matrekta makubwa matano ya sh milioni 258, ikiwa ni utekelezaji wa Mpango huo.
Napenda ndoto zake, seriously!!!!!!!!
Thursday, 13 May 2010 05:46
Na Mwandishi Wetu
Waziri Mkuu Mizengo Pinda amesema Kilimo cha jembe la mkono nchini sasa basi kwa vile kimeshindwa kuleta Mapinduzi ya Kilimo na badala yake lazima kutumia zana za kisasa na utalaamu.
Alikuwa akihutubia Mkutano wa hadhara katika Kijiji cha Mirumba, Kata ya Kibaoni, Tarafa ya Mpimbwe baada ya kukabidhi matrekta kwa vikundi vya wakulima katika siku yake ya nne ya ziara yake ya jimbo.
Jembe la Mkono siyo zana ya kutegemea kubadili maisha yetu Wenzetu wanalima kwa matrekata madogo na makubwa, wanapanda na kuvuna kwa matrekta majembe ya mkono yalitumika zaidi ya miaka 2,000 iliyopita, alisema.
Alikabidhi trekta moja kubwa kwa kikundi cha mbugani cha Kijiji cha Itenka; moja dogo kwa kikundi cha Jitume cha Kijiji cha Magamba na jingine dogo kwa kikundi cha Ufugaji Nyuki cha Kijiji cha Uruira.
Trekta kubwa aina ya Tafe, liliotengenezwa India, lina thamani ya sh. milioni 51 na wakulima wanatakiwa kuilipa Halmashauri ya Wilaya ya Mpanda sh. milioni 10 ambayo ni asilimia 20 ya gharama ambazo halmashauri hiyo iliingia kulinunua.
Trekta dogo aina ya Kubota la Japan wakulima hutakiwa kulipia sh. milioni 1.5, ikiwa ni Asilimia 10 tu ya bei yake.
Halmashauri ya Wilaya ya Mpanda tangu mwaka 2007/2008 imekuwa ikitekeleza agizo la serikali la kununua matrekta na kuyasambaza kwa wakulima kwa bei ya chini, ikiwa ni sehemu ya kuendeleza kilimo cha zana na cha kisasa.
Kwa mwaka huu wa fedha unaomalizika Mwezi ujao (2009/2010), Halmashauri ya Wilaya ya Mpanda ilipanga kununua matrekta madogo 36, kwa gharama ya sh. milioni 284 na matrekta makubwa matano ya sh milioni 258, ikiwa ni utekelezaji wa Mpango huo.
Napenda ndoto zake, seriously!!!!!!!!