Jembe la mkono sasa basi - Mh. Pinda

Ngambo Ngali

JF-Expert Member
Apr 17, 2009
3,517
1,359
Pinda: Jembe la mkono sasa basi


Thursday, 13 May 2010 05:46
Na Mwandishi Wetu

Waziri Mkuu Mizengo Pinda amesema Kilimo cha jembe la mkono nchini sasa basi kwa vile kimeshindwa kuleta Mapinduzi ya Kilimo na badala yake lazima kutumia zana za kisasa na utalaamu.

Alikuwa akihutubia Mkutano wa hadhara katika Kijiji cha Mirumba, Kata ya Kibaoni, Tarafa ya Mpimbwe baada ya kukabidhi matrekta kwa vikundi vya wakulima katika siku yake ya nne ya ziara yake ya jimbo.

“Jembe la Mkono siyo zana ya kutegemea kubadili maisha yetu… Wenzetu wanalima kwa matrekata madogo na makubwa, wanapanda na kuvuna kwa matrekta… majembe ya mkono yalitumika zaidi ya miaka 2,000 iliyopita,” alisema.

Alikabidhi trekta moja kubwa kwa kikundi cha mbugani cha Kijiji cha Itenka; moja dogo kwa kikundi cha Jitume cha Kijiji cha Magamba na jingine dogo kwa kikundi cha Ufugaji Nyuki cha Kijiji cha Uruira.

Trekta kubwa aina ya Tafe, liliotengenezwa India, lina thamani ya sh. milioni 51 na wakulima wanatakiwa kuilipa Halmashauri ya Wilaya ya Mpanda sh. milioni 10 ambayo ni asilimia 20 ya gharama ambazo halmashauri hiyo iliingia kulinunua.

Trekta dogo aina ya Kubota la Japan wakulima hutakiwa kulipia sh. milioni 1.5, ikiwa ni Asilimia 10 tu ya bei yake.

Halmashauri ya Wilaya ya Mpanda tangu mwaka 2007/2008 imekuwa ikitekeleza agizo la serikali la kununua matrekta na kuyasambaza kwa wakulima kwa bei ya chini, ikiwa ni sehemu ya kuendeleza kilimo cha zana na cha kisasa.

Kwa mwaka huu wa fedha unaomalizika Mwezi ujao (2009/2010), Halmashauri ya Wilaya ya Mpanda ilipanga kununua matrekta madogo 36, kwa gharama ya sh. milioni 284 na matrekta makubwa matano ya sh milioni 258, ikiwa ni utekelezaji wa Mpango huo.



Napenda ndoto zake, seriously!!!!!!!!
 
Mtoto wa mkulima kwa hili la kutumia matrekta ya Tafe na Kubota linaniingia akilini lakini hili la Power tiller aghaaaaaaa ulichemka. Ki ukweli power tiller ni mzigo kwa wakulima kwani hili linafaa sana kwenye maeneo ambayo ni soaked land na sio yenye dry/hard land kama dodoma nk na pia si mazuri kwenye milima kama lushoto. Cha kushangaza sasa wakurugenzi wa halmashauri wameyanunua bila kuomba ushauri wa maofisa kilimo wao wakisema ni agizo la waziri mkuu na bei ya power tiller moja ni kama tsh 5 mil ila limenunuliwa kwa 12mil na hizi halimashauri. Matokeo yake sasa wananchi wameshindwa kuyatumia baada ya kuona wenzao wanaoyatumia hayawasidii zaidi ya kuwaletea magonjwa kama kifua kikuu kutokana na vumbi na pia kuwanyong'onyeza kiafya kwani ili lilime linahitaji mkulima atumie nguvu nyingi, kama ukifika kwenye bohari au maeneo mengi ya ofisi za ujenzi Tanzania utayakuta haya matreka madogo yakiwa yamepark, ukiuliza utaambiwa kuwa wakulima hawaji kuyakopesha.Maswali Je ilikuwa agizo toka kwa Waziri mkuu kuwa kila wilaya ni lazima inunue power tiller? Je wataalamu wa kilimo na udongo walihusishwa kikamilifu kutoa ushauri wao kama power tiller zinunuliwe au la au wakurugenzi walinunua kisiasa zaidi, Je azimio la kilimo kwanza litaleta mapinduzi ya kijani au litapindisha migongo wakulima?. Ushauri wataalamu wa kilimo wasikilizwe, serikali itenge hela ya kutosha uli kuweza kuagiza mbolea na matrekta kama kubota ambayo yana uwezo wa kulima hekta nyingi kwa siku bila kuadhili afya ya mkulima, swala la siasa lisiingie kwenye vitu muhimu kama kilimo nk na wakurugenzi waache nidhamu ya woga wafanye kazi kutokana na ushauri mzuri wa maofisa wao walio chini kama DALDO, Waziri mkuu awachukulie hatua za kisheria wale wote ambao wamenunua mapoer tiller kwa bei za juu ikiwa hali bei zake si kubwa kivile kwani hapo kuna chembe chembe za rushwa na ufisadi Mwisho Haiwezekani kilimo kuwa kwanza kinadhalia tu wakati katika bajeti ya nchi kimepewa kipaumbele cha nne, ni vema kuwa makini kwa kila jambo sio kushika hili na lile baadae moja lazima lituponyoke tu.

Mkereketwa
 
To be honest napenda kuwauliza Hivi mrisha fanya research ya hizo tender za wanao leta ma trecktor yao na Je yanahimili mbuga zetu za huko kilosa na ardhi za kuho kanda ya ziwa na kaskazini? tusije jaribu jaribu vitu hapa na baaada tukaanza point finger to each of us, kabisa nawambieni ngojeni mtaniambia kuhusu izo pembejeo zitakapo fika maana naona watu wanakimbilia tu kuchukua tender za kuuza hizo pembe jeo.me namashaka nazo sana ipo ziku zitakuja kutupotezea mwelekeo wa maendeleo yetu kama hatuto simamia hizi (a.k.a Kauli mbiu),sera na sheria tuzianzishazo wandugu

Kipindi cha nyuma kuna company moja kubwa dunia ya tracktor waliomba kibari cha kufanya assemble ya hayo ma tracktor lakini ndani ya serikali yetu kwa sababu haojamaa walikuwa hawana mtu na wakapingwa vibaya basi ile kambuni ilishuka kusini mwa africa na wakapewa kibali cha ku assemble tracktor sasa sijui hawa viongozi wetu hawakujua kuwa kuna kilimo kwanza au ndio wame implement juzi juzi? tu basi mjue hata kuendelea kwake kutatuchukuwa miaka ku reach hizo goals za kilimo kwanza kwa wakulima i mean kwa watanzania watakao penda kuwa wakulima
 
Mtoto wa mkulima kwa hili la kutumia matrekta ya Tafe na Kubota linaniingia akilini lakini hili la Power tiller aghaaaaaaa ulichemka. Ki ukweli power tiller ni mzigo kwa wakulima kwani hili linafaa sana kwenye maeneo ambayo ni soaked land na sio yenye dry/hard land kama dodoma nk na pia si mazuri kwenye milima kama lushoto. Cha kushangaza sasa wakurugenzi wa halmashauri wameyanunua bila kuomba ushauri wa maofisa kilimo wao wakisema ni agizo la waziri mkuu na bei ya power tiller moja ni kama tsh 5 mil ila limenunuliwa kwa 12mil na hizi halimashauri. Matokeo yake sasa wananchi wameshindwa kuyatumia baada ya kuona wenzao wanaoyatumia hayawasidii zaidi ya kuwaletea magonjwa kama kifua kikuu kutokana na vumbi na pia kuwanyong'onyeza kiafya kwani ili lilime linahitaji mkulima atumie nguvu nyingi, kama ukifika kwenye bohari au maeneo mengi ya ofisi za ujenzi Tanzania utayakuta haya matreka madogo yakiwa yamepark, ukiuliza utaambiwa kuwa wakulima hawaji kuyakopesha.Maswali Je ilikuwa agizo toka kwa Waziri mkuu kuwa kila wilaya ni lazima inunue power tiller? Je wataalamu wa kilimo na udongo walihusishwa kikamilifu kutoa ushauri wao kama power tiller zinunuliwe au la au wakurugenzi walinunua kisiasa zaidi, Je azimio la kilimo kwanza litaleta mapinduzi ya kijani au litapindisha migongo wakulima?. Ushauri wataalamu wa kilimo wasikilizwe, serikali itenge hela ya kutosha uli kuweza kuagiza mbolea na matrekta kama kubota ambayo yana uwezo wa kulima hekta nyingi kwa siku bila kuadhili afya ya mkulima, swala la siasa lisiingie kwenye vitu muhimu kama kilimo nk na wakurugenzi waache nidhamu ya woga wafanye kazi kutokana na ushauri mzuri wa maofisa wao walio chini kama DALDO, Waziri mkuu awachukulie hatua za kisheria wale wote ambao wamenunua mapoer tiller kwa bei za juu ikiwa hali bei zake si kubwa kivile kwani hapo kuna chembe chembe za rushwa na ufisadi Mwisho Haiwezekani kilimo kuwa kwanza kinadhalia tu wakati katika bajeti ya nchi kimepewa kipaumbele cha nne, ni vema kuwa makini kwa kila jambo sio kushika hili na lile baadae moja lazima lituponyoke tu.

Mkereketwa

Asante sana mkereketwa, kama ulikuwa kichwani mwangu
 
Naona Pinda anawanga khe khe ati trekta moja kubwa .... imbecile.
 
Pinda anaongea kufurahisha wapiga kura wake, hilo haliwezekani kwa Tanzania hii, na serikali haina nia ya kumsadia mkulima kwa hali ya chini kabisa, this is political statement - haina ukweli wowote na hali halisi.
 
Jamani, ni wakulima gani wadogo wa Tanzania ambao wanaweza kuwa na Sh. 10m kununua trekta kubwa au hata hiyo 1.5m kuweza kununua trekta dogo? Nadhani wananchi wenye uwezo na wenye matrekta waombwe kuwasaidia wakulima wadogo kwa kuwalimia mashamba bure ama kwa kuchangia mafuta maana wao tayari uwezo wanao.

Yupo Mbunge mmoja ambaye amejihakikishia kura za wananchi wa jimbo lake kwa sababu yeye baada ya kupata kiinua mgongo chake bungeni aliamua kununua trekta na kila msimu wa kilimo baada ya kumaliza kulima shamba lake amekuwa akitoa trekta hilo wananchi walitumie bureee mradi tu wachange fedha za mafuta na wakati mwingine mbunge huyo hujitolea kuwanunulia wananchi mafuta pale anapoona hawana uwezo wa kununua. Huo ni mfano bora wa kiongozi. Wananchi hao wameweza kulima mashamba makubwa na kujipatia kipato zaidi kutokana na kujitolea kwa mbunge wao kuwasaidia.
 
Hapa sijamuelewa mweshimiwa waziri. Ilo jembe moja ndo basi?

Halafu yeye akiongea kwa sababu ni waziri mkuu lazima awe specific aseme na aongeze kama anaongelea katika ngazi ya kitongoji, kijiji, kata, tarafa, wilaya, mkoa au Taifa.

Maana akiongea waziri Mkuu tunamtazama sana sana aongee kitaifa. Hivyo tunaomba achague maneno ya kusema vizuri.
 
Hapa sijamuelewa mweshimiwa waziri. Ilo jembe moja ndo basi?

Halafu yeye akiongea kwa sababu ni waziri mkuu lazima awe specific aseme na aongeze kama anaongelea katika ngazi ya kitongoji, kijiji, kata, tarafa, wilaya, mkoa au Taifa.

Maana akiongea waziri Mkuu tunamtazama sana sana aongee kitaifa. Hivyo tunaomba achague maneno ya kusema vizuri.

Mkuu kumbe nawe umeliona? yaani anaongelea kaeneo kadogo ndani ya Tz, afu ana generalise eti jembe la mkono basi!
Huyu naye nimemstukia ni mzee wa maneno ya kufurahisha baraza tu, utekelezajikiduchuu!
 
hawa watu wana matatizo; hivi wanakumbuka mara ya mwisho kusema "kuondokana na jembe la mkono" ilikuwa lini?
 
jamani, ni wakulima gani wadogo wa tanzania ambao wanaweza kuwa na sh. 10m kununua trekta kubwa au hata hiyo 1.5m kuweza kununua trekta dogo? Nadhani wananchi wenye uwezo na wenye matrekta waombwe kuwasaidia wakulima wadogo kwa kuwalimia mashamba bure ama kwa kuchangia mafuta maana wao tayari uwezo wanao.
hesabu rahisi........hivi zile bilioni 40 za kampeini tunanunua matrecta mangapi???fanya hesabu hii rahisi then unipe jibu........
40,000,000,000/1,500,000 au
40,000,000,000/10,000,000
ni sawa na mangapi?????
 
POLITICIAN, ONE WHO SHAKES YOUR HAND BEFORE ELECTION AND YOUR CONFIDENCE LATER


Silent whisper kwa hii nitapendekeza waongezee kabatani
 
Wanatambua kauli zao hazina uhalisiaa ila wanafurahiaa tunapozijadilii tena kwa pumzii kubwaa..

Kwa ujumla pinda hana kauli iliyowahi kutekelezekaaa au yenye mantiki..
 
Ni maneno tu hata kwenye kanga yapo, hizi zana za kisasa zitamfikia lini mkulima wa Biharamulo, hizi trekta ziko Dar tu na vijijini wanaendelea na sera ya KILIMO NI UGONJWA WA UTI WA MGONGO!
 
Pinda anaongea kufurahisha wapiga kura wake, hilo haliwezekani kwa Tanzania hii, na serikali haina nia ya kumsadia mkulima kwa hali ya chini kabisa, this is political statement - haina ukweli wowote na hali halisi.

Elnino umeongea. Pinda anaongea ili kukamilisha ratiba ya ziara yake huko kwao. Ni polotical statement.
 
Pinda: Jembe la mkono sasa basi


Thursday, 13 May 2010 05:46
Na Mwandishi Wetu

Waziri Mkuu Mizengo Pinda amesema Kilimo cha jembe la mkono nchini sasa basi kwa vile kimeshindwa kuleta Mapinduzi ya Kilimo na badala yake lazima kutumia zana za kisasa na utalaamu.


Trekta kubwa aina ya Tafe, liliotengenezwa India, lina thamani ya sh. milioni 51 na wakulima wanatakiwa kuilipa Halmashauri ya Wilaya ya Mpanda sh. milioni 10 ambayo ni asilimia 20 ya gharama ambazo halmashauri hiyo iliingia kulinunua.

Trekta dogo aina ya Kubota la Japan wakulima hutakiwa kulipia sh. milioni 1.5, ikiwa ni Asilimia 10 tu ya bei yake.

Napenda ndoto zake, seriously!!!!!!!!

Mi nilifikiri anakwenda kugawa kila kijiji kumbe Mpanda, sasa hizo milioni kweli huyu mkulima wa jembe anazo? Mfanyakazi tu kumlipa KCC ya laki 3 ngumu, sasa huyu mkulima mwenye akiba ya 1.5m to start with..... kweli hawa viongozi wetu huwa wanajisahau wanafikiri wote tunapata mamilioni yasiyokatwa kama wao.
 
Siku sema thanks kufurahia maneno ya Mheshimiwa Pinda! La hasha! Hii ni kwa kuwa katika hali halisi mheshimiwa Pinda anaongea kufurahisha wananchi wake ambao ndio mtaji wa kura kwake. Nasema hivyo kwa udhati mkubwa kwani kwa hali halisi swala hilo haliwezekani kirahisi kwa mazingira ya Tanzania hii ambayo hata watoto wanafaulu darasa la saba wazazi wao wanashindwa kuwapeleka shule. Si kwakuwa hawapendi bali umaskini umekithiri. Pia kwa hali halisi serikali haina nia ya kumsadia mkulima kwa hali ya chini kabisa,kwa kuwa tunaona jinsi malighafi zinavyopanda.bei
 
PINDA na Serikali ya awamu ya JK,wamesema KILIMO KWANZA ,maana yake kuwa kilimo kitapewa kipaumbele na siyo MKULIMA KWANZA,hapa namaanisha kuwa kilimo kitafanyika na mfanyabiashara yeyote,na siyo lazima uwe mtanzania.tusipoteze muda kujadili kauli mbiu za viongozi,tuangalie je Wameweka mikakati ipi kuboresha maisha ya wakulima.
Gazeti la New African IC Publications | African Business | Home
limekuwa likitoa habari kuhusu mikataba ya kilimo kati ya nchi za uarabuni, mfano Mfalme wa Saudi amevuna mahindi aliyopanda ETHOPIA ,hivyo analo shamba kubwa ethopia wakati wakulima wa ethopia wana njaa kali.
nchi ya Madagascar,imepewa eneo la kulima mpunga nchi ya Mozambiki/Msumbiji.
kuna kitu kinaitwa FOOD SECURITY,waarabu wameanza kujipanga kwa kuja East Africa kununua maeneo ya mashamba kwa kilimo kwanza,Jana wamefika na uongozi wa nchi umeshawapokea ,
IN SHORT, ni KILIMO KWANZA na Mkulima wa Tanzania AtaJijua mwenyewe after elections.
 
Back
Top Bottom