Masanilo
Platinum Member
- Oct 2, 2007
- 22,286
- 4,493
Afungwa jela miezi sita kwa kukaidi kuvua baraghashia mahakamani
Tuesday, 31 August 2010
Hadija Jumanne
MSHAURI wa baraza la kata Gongo la Mboto, anayekabiliwa na kesi ya kutishia kuua na kusababisha fujo, Ally Sururu (60) amehukumiwa kifungo cha miezi sita jela, baada ya kukaidi amri ya hakimu aliyemtaka avue kofia aliyokuwa ameivaa kizimbani aina ya baraghashia.
Hukumu hiyo ilitolewa jana na Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Wilaya ya Ilala, WilbaForce Luhwago, mara baada ya mtuhumiwa huyo kumwambia hakimu huyo kuwa hana maadili kwa kumtaka yeye avue kofia.
Mara baada ya Sururu kutoa kauli hiyo mbele ya mahakama, hakimu Luhwago alimtaka akampumzike kwa muda katika mahabusu ya mahakama hiyo ya Ilala.
Lakini cha kushangaza, mtuhumiwa alikaidi amri hiyo huku akimweleza hakimu Luhwago kuwa baraghashia ni sawa na vazi lolote hivyo hawezi kuivua.
Hakimu Luhwago alimwambia mshtakiwa huyo kuwa kwa sababu hiyo ni tabia yako ya kudharau mahakama ukiachiwa utaendelea na tabia hiyo, hivyo utatumikia kifungo cha miezi sita jela huku kesi yako inaendelea kusikilizwa.
Sururu ambaye yupo nje kwa dhamana , kabla ya kuhukumiwa kifungo hicho cha miezi sita jela, jana hiyo alifika mahakamani hapo kwa ajili ya kuisikiliza kesi yake.
Kabla ya kupewa hukumu hiyo Mwendesha Mashtaka wa Polisi, Daniel Buma aliiomba mahakama hiyo kutoa adhabu kali dhidi ya mtuhumiwa kutokana na tabia aliyoionyesha ya kudharau mahakama na kudaia kuwa zikiachiwa tabia hizo mahakama hazitaheshimiwa"alidai Buma.
Awali mtuhumiwa alifikishwa katika mahakama ya wilaya ya Ilala akikabiliwa na kesi ya kutishia kuuwa na kutoa lugha chafu ikiwemo usumbufua katika baraza la kata.
Kwa mara ya kwanza kesi hiyo ilikuja katika mahakama hiyo Septemba 15, mwaka jana, na mtuhumiwa alitenda kosa hilo Agosti 27,mwaka 2008 katika eneo la Ukonga Mzambarauni.
Ilidaiwa na mwendesha mashtaka kuwa mtuhumiwa alitoa maneno makali wakati wakiwa katika mashauriano katika baraza la kata na hivyo kusababaisha usumbufu na uvunjifu wa amani katika baraza hilo.
Buma aliendelea kudai kuwa mtuhumiwa katika shtaka la pili anadaiwa kumtishia kumuua Mzee Shija .
Ilidiwa siku hiyo majira ya saa 5 asubuhi mtuhumiwa alimtishia kwa maneno mzee Shija kwa kumwambia "Wewe Mzee Shija nitakushughulikia kisawasawa na kuwa ndio mwisho wako"alisema mtuhumiwa huyo katika baraza la kata na hivyo kusababisha hofu kwa mlalamikaji.
Hata hivyo kesi hiyo ilikuja kwa ajili ya kutajwa kwa kuwa upelelezi ulikuwa bado haujakamilika.
Gazeti la Mtanzania
Tuesday, 31 August 2010
Hadija Jumanne
MSHAURI wa baraza la kata Gongo la Mboto, anayekabiliwa na kesi ya kutishia kuua na kusababisha fujo, Ally Sururu (60) amehukumiwa kifungo cha miezi sita jela, baada ya kukaidi amri ya hakimu aliyemtaka avue kofia aliyokuwa ameivaa kizimbani aina ya baraghashia.
Hukumu hiyo ilitolewa jana na Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Wilaya ya Ilala, WilbaForce Luhwago, mara baada ya mtuhumiwa huyo kumwambia hakimu huyo kuwa hana maadili kwa kumtaka yeye avue kofia.
Mara baada ya Sururu kutoa kauli hiyo mbele ya mahakama, hakimu Luhwago alimtaka akampumzike kwa muda katika mahabusu ya mahakama hiyo ya Ilala.
Lakini cha kushangaza, mtuhumiwa alikaidi amri hiyo huku akimweleza hakimu Luhwago kuwa baraghashia ni sawa na vazi lolote hivyo hawezi kuivua.
Hakimu Luhwago alimwambia mshtakiwa huyo kuwa kwa sababu hiyo ni tabia yako ya kudharau mahakama ukiachiwa utaendelea na tabia hiyo, hivyo utatumikia kifungo cha miezi sita jela huku kesi yako inaendelea kusikilizwa.
Sururu ambaye yupo nje kwa dhamana , kabla ya kuhukumiwa kifungo hicho cha miezi sita jela, jana hiyo alifika mahakamani hapo kwa ajili ya kuisikiliza kesi yake.
Kabla ya kupewa hukumu hiyo Mwendesha Mashtaka wa Polisi, Daniel Buma aliiomba mahakama hiyo kutoa adhabu kali dhidi ya mtuhumiwa kutokana na tabia aliyoionyesha ya kudharau mahakama na kudaia kuwa zikiachiwa tabia hizo mahakama hazitaheshimiwa"alidai Buma.
Awali mtuhumiwa alifikishwa katika mahakama ya wilaya ya Ilala akikabiliwa na kesi ya kutishia kuuwa na kutoa lugha chafu ikiwemo usumbufua katika baraza la kata.
Kwa mara ya kwanza kesi hiyo ilikuja katika mahakama hiyo Septemba 15, mwaka jana, na mtuhumiwa alitenda kosa hilo Agosti 27,mwaka 2008 katika eneo la Ukonga Mzambarauni.
Ilidaiwa na mwendesha mashtaka kuwa mtuhumiwa alitoa maneno makali wakati wakiwa katika mashauriano katika baraza la kata na hivyo kusababaisha usumbufu na uvunjifu wa amani katika baraza hilo.
Buma aliendelea kudai kuwa mtuhumiwa katika shtaka la pili anadaiwa kumtishia kumuua Mzee Shija .
Ilidiwa siku hiyo majira ya saa 5 asubuhi mtuhumiwa alimtishia kwa maneno mzee Shija kwa kumwambia "Wewe Mzee Shija nitakushughulikia kisawasawa na kuwa ndio mwisho wako"alisema mtuhumiwa huyo katika baraza la kata na hivyo kusababisha hofu kwa mlalamikaji.
Hata hivyo kesi hiyo ilikuja kwa ajili ya kutajwa kwa kuwa upelelezi ulikuwa bado haujakamilika.
Gazeti la Mtanzania