Rutashubanyuma
JF-Expert Member
- Sep 24, 2010
- 219,470
- 911,173
Jela miaka 30 kwa wizi wa nazi
Imeandikwa na Kennedy Kisula, Lindi; Tarehe: 26th January 2011 @ 06:18
MKAZI wa kijiji cha Kiwalala wilayani Lindi mkoani hapa, Salumu Ally (25) amehukumiwa kifungo cha miaka 30 baada ya kuthibitika kufanya kosa la unyan'ganyi wa nazi kwa kutumia silaha.
Hukumu hiyo ilisomwa na Hakimu Mfawidhi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi, Dunstan Ndunguru jana, baada ya kusikiliza ushahidi wa pande zote mbili.
Awali Wakili wa Serikali, Mwahija Hamad alisema mshitakiwa Salumu Ali mkazi wa kiwalala alifikishwa mahakamani Octoba, 10 mwaka jana na kupatikana na hatia ya kumjeruhi kwa kutumia silaha, Somoe Issa (42).
Alidai mshitakiwa alimjeruhi Issa Septemba, 26 mwaka jana saa nane mchana kwa kutumia kisu sehemu za paja, shingoni na usoni.
Hamadi alidai baada ya hapo mshitakiwa alimbinya Issa sehemu za shingoni mpaka alipoteza fahamu kutoka saa 8.00 mchana mpaka saa 2.00 usiku alipozinduka.
Baada ya hapo mshitakiwa anadaiwa alichukua nazi 25 shambani mwa mlalamikaji baada ya kudhani kuwa alishafariki lakini wananchi walitoa taarifa kituo kidogo cha Polisi na msako ulianza na baadaye mshitakiwa alikamatwa.
Naye Hakimu Ndunguru alisema Mahakama inamtia hatiani kwa kosa la unyang'anyi wa kutumia silaha na adhabu yake ni kifungo cha miaka 30 ili iwe fundisho kwa wengine ambao wanataka kutenda kosa kama hilo.