Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Ni kawaida kwenye MAPENZI/MAHUSIANO watu kuwa na wivu..na ukifuatilia kwa karibu utaona kuwa watu wengi wanakuwa na wivu na wapenzi/wanandoa wenzao kwa sababu wanadai ni sehemu ya mapenzi yenyewe. Tukatae tukubali wakati mwingine wivu unaendana na kuchunguzana na huwezi kumpangia mwenzio akuchunguze vipi..sana sana itetegemea na 'angle' atakayoangukia.
Lakini wakati wengine wanasema wivu ni 'sunna' wengine pia husema kuna wivu na wivu..i mean kuna wivu wenye mantiki na WIVU WA KIJINGA..wanaotetea wivu wa mantiki wanasema 'ni sahihi kumuonyesha wivu mwenzio ili akuone kama unamjali'..na halikadhalika kuna wanaosema binadamu hachungwi..na kumuonyesha wivu mwenzio ni UJINGA na kutomuamini katika kila afanyalo..Kiukweli inawezekana hakuna 'rule of thumb' ya namna wivu unavyotakiwa uwe.
But pamoja na hayo..wivu upo na ndoa/mahusiano yanavunjika kila siku kwa sababu ya wivu..Sasa nilichokuwa naomba kushea na ninyi wadau ni hiki..Je? Wivu ni tokeo la kumpenda mtu kwa sana au ukimpenda mtu sana unamuamini na wivu unapungua kwa hiyo wivu huja baada ya mapenzi kukupungukia?..au kuna sababu nyinginezo?..twende pamoja basi!!!!
Wewe huna wivu??..kwa nini unampenda mwenye wivu aisee..