Je, wivu ni tokeo la kumpenda mtu kwa sana?

nyumba kubwa nashukuru kwa hizi article nadhani pamoja na ile ya Mtambuzi kwa kiasi kikubwa zinaweza kusaidia. Kikubwa nilichoona kuna aina mbalimbali za wivu..sema kiswahili chetu nacho kinashindwa kutofautisha 'envy' na 'jealous'. Na kingine nilichoona ni kuwa mtu kuwa na wivu sio ujinga na pia sometimes ni ujinga (ugly jealous). Zaidi inategemea na 'intensity' ya wivu wenyewe na mazingira yanayokufanya uwe na wivu na mwenzio.

Ila nimeshindwa kuelewa kama wivu unakuja automatically au kuna mazingira yanaujenga??..
 
Last edited by a moderator:
Hata mimi napenda sana, tena sana mwanamke mwenye wivu jamani. Japokuwa sijaoa lakini nitafurahi sana kupata mwanamke atakaye kuwa na wivu kwangu.
 
Hata mimi napenda sana, tena sana mwanamke mwenye wivu jamani. Japokuwa sijaoa lakini nitafurahi sana kupata mwanamke atakaye kuwa na wivu kwangu.

Wewe huna wivu??..kwa nini unampenda mwenye wivu aisee..
 
Ni kawaida kwenye MAPENZI/MAHUSIANO watu kuwa na wivu..na ukifuatilia kwa karibu utaona kuwa watu wengi wanakuwa na wivu na wapenzi/wanandoa wenzao kwa sababu wanadai ni sehemu ya mapenzi yenyewe. Tukatae tukubali wakati mwingine wivu unaendana na kuchunguzana na huwezi kumpangia mwenzio akuchunguze vipi..sana sana itetegemea na 'angle' atakayoangukia.

Lakini wakati wengine wanasema wivu ni 'sunna' wengine pia husema kuna wivu na wivu..i mean kuna wivu wenye mantiki na WIVU WA KIJINGA..wanaotetea wivu wa mantiki wanasema 'ni sahihi kumuonyesha wivu mwenzio ili akuone kama unamjali'..na halikadhalika kuna wanaosema binadamu hachungwi..na kumuonyesha wivu mwenzio ni UJINGA na kutomuamini katika kila afanyalo..Kiukweli inawezekana hakuna 'rule of thumb' ya namna wivu unavyotakiwa uwe.

But pamoja na hayo..wivu upo na ndoa/mahusiano yanavunjika kila siku kwa sababu ya wivu..Sasa nilichokuwa naomba kushea na ninyi wadau ni hiki..Je? Wivu ni tokeo la kumpenda mtu kwa sana au ukimpenda mtu sana unamuamini na wivu unapungua kwa hiyo wivu huja baada ya mapenzi kukupungukia?..au kuna sababu nyinginezo?..twende pamoja basi!!!!

Ukishapenda mtu,hutataka kusheya nae na watu wengine,wivu unakuepo kama unampenda mtu,lakini sio wivu uliopitiliza.Wivu uliopitiliza hapo kutakua na another agenda.
 
Wewe huna wivu??..kwa nini unampenda mwenye wivu aisee..

Kiukweli hata mimi najihisi ni mtu mwenye wivu mkuu, na siamini kama inawezekana watu kupendana kwa dhati bila kila mmoja kuwa na wivu kwa mwenziwe
 
Wivu ni hali ya kutokuamini yakwamba yule umpendae atakuwa wako nyakati zoote kwasababu tu kile unachodhani anahitaji kupewa huna uwezo wa kumpa kwa anavyostahili na unaamini kuna mtu anaweza kumpa zaidi ya kile unachompa kwa nyakati hizo hivyo akawa sio wako au akaonjwa. Huo ndio wivu BHAAAAAAAASSSS

Nadhani nimeeleweka kiduchu. kama unaweza ongeza au punguza
 
hakuna mtu asiyekuwa na vivu kwa kile akipendacho na kama hauna vivu na mkeo/mmeo basi ujue ndoa yenu haitadumu kwa maana hakuna upendo na wivu huendana naupendo
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom