Nimekuwa hapa Ughaibuni kwa muda sasa na nimepata bahati ya kukutana na watanzania wenzetu walio huku ughaibuni kwa muda mrefu.
Nimejifunza jambo moja kutoka kwa hao woote.
Watu hawaijui tena nchi yao!!!
Inaonekana wengi wamebaki kutegemea habari za blog mbali mbali kujua kinachoendelea nchini. Mtu atakuuliza jambo la mwaka arobaini na saba hadi unashangaa.... jambo lisilo katika internet basi halijulikani. chochote unachomuuliza mtu anataka Kusearch.... mambo ya ngangamfumuni huko moshi utayapata katika internet? Mambo ya Nkasi utayapata humo? Ni kweli hapa wenyeji hawatumii tena memory zao. hata ukiuliza duka la sukari li wapi anakuambia "go to the internet and google it, it must be around here...? Toba, siye hatujafika huko...
Mtu atakuambia vipi Beer bado ni za mgao huko? Au kwenda Arusha from Dar mabasi yanaondoka usiku? Au treni inaondoka muda gani from Dar to Moshi? etc
Ni vizuri kujua pia Tanzania pamoja na matatizo yetu, masuala ya ufisadi, mgao wa umeme unaondelea zipo hatua kadhaa ambazo nchi yetu imepiga kwa sasa, lazima kujivunia. Huduma kutoka ktk wizara mbali mbali imeimprove kwa kiasi kikubwa. Zipo Wizara ambazo ni za kupigiwa mfano. Customer care unayoipata pale inaridhisha. Jeshi letu la Polisi pamoja na matatizo yake ya asili, lina mabadiliko ya kutia moyo. Ni wazi bado wapo polisi wachache wasio waaminifu au walioamua kutobadilika, kama msemo usemavyo, msafara wa mamba kenge wamo....
Wengi bado wanaliwaziwa suala la uraia wa nchi mbili. Hili nadhani nami niungane na maoni ya watanzania wengi nyumbani si suala la kuendekeza. Kheri tuwe na watanzania wachache wenye moyo na nchi yao. Uraia wa nchi mbili si kwa manufaa ya nchi wala manufaa ya wananchi walio wengi.... kwanza ni watanzania wangapi wenye paspoti? hii itasababisha mafisadi wawe huru kuiba na kukimbia. najua wapo watz waaminifu wataofaidi na uraia wa nchi mbili lakini nadhaniwakati bado....
Vinginevyo niwashauri watz hawa walio huku ughaibuni kujenga mazoea ya kurudi mara kwa mara nyumbani na kujua hali inayoendelea. Kutegemea blogs kujua hali ya nyumbani si uzalendo.....
karibuni nyumbani, mimi nitaondoka kuelekea huko Krismas....
Nimejifunza jambo moja kutoka kwa hao woote.
Watu hawaijui tena nchi yao!!!
Inaonekana wengi wamebaki kutegemea habari za blog mbali mbali kujua kinachoendelea nchini. Mtu atakuuliza jambo la mwaka arobaini na saba hadi unashangaa.... jambo lisilo katika internet basi halijulikani. chochote unachomuuliza mtu anataka Kusearch.... mambo ya ngangamfumuni huko moshi utayapata katika internet? Mambo ya Nkasi utayapata humo? Ni kweli hapa wenyeji hawatumii tena memory zao. hata ukiuliza duka la sukari li wapi anakuambia "go to the internet and google it, it must be around here...? Toba, siye hatujafika huko...
Mtu atakuambia vipi Beer bado ni za mgao huko? Au kwenda Arusha from Dar mabasi yanaondoka usiku? Au treni inaondoka muda gani from Dar to Moshi? etc
Ni vizuri kujua pia Tanzania pamoja na matatizo yetu, masuala ya ufisadi, mgao wa umeme unaondelea zipo hatua kadhaa ambazo nchi yetu imepiga kwa sasa, lazima kujivunia. Huduma kutoka ktk wizara mbali mbali imeimprove kwa kiasi kikubwa. Zipo Wizara ambazo ni za kupigiwa mfano. Customer care unayoipata pale inaridhisha. Jeshi letu la Polisi pamoja na matatizo yake ya asili, lina mabadiliko ya kutia moyo. Ni wazi bado wapo polisi wachache wasio waaminifu au walioamua kutobadilika, kama msemo usemavyo, msafara wa mamba kenge wamo....
Wengi bado wanaliwaziwa suala la uraia wa nchi mbili. Hili nadhani nami niungane na maoni ya watanzania wengi nyumbani si suala la kuendekeza. Kheri tuwe na watanzania wachache wenye moyo na nchi yao. Uraia wa nchi mbili si kwa manufaa ya nchi wala manufaa ya wananchi walio wengi.... kwanza ni watanzania wangapi wenye paspoti? hii itasababisha mafisadi wawe huru kuiba na kukimbia. najua wapo watz waaminifu wataofaidi na uraia wa nchi mbili lakini nadhaniwakati bado....
Vinginevyo niwashauri watz hawa walio huku ughaibuni kujenga mazoea ya kurudi mara kwa mara nyumbani na kujua hali inayoendelea. Kutegemea blogs kujua hali ya nyumbani si uzalendo.....
karibuni nyumbani, mimi nitaondoka kuelekea huko Krismas....