Richard
JF-Expert Member
- Oct 23, 2006
- 14,939
- 20,399
Hili swali limenijia baada ya kuona majaribio kadhaa ya baadhi ya watanzania kama vile bwana Mwakalinga alipojaribu kugombe jimbo la Kyela kwa kushindana na Dr Harrison Mwakyembe, pia Dr Shayo na juzijuzi bwana William Malecela ambao wamejaribu kugombea nafasi ya ubunge kwenye bunge la Afrika Mashariki.
Ni mategemeo ya watanzania wengi ambao wengine wamediriki kujiingiza katika nafasi mbalimbali za uongozi katika matawi ya CCM yalizagaa nje ya nchi hususan Ulaya na Marekani.
Je ni sababu zipi ambazo zinawafanya watanzania hawa kushindwa kuingia kwenye mfumo wa siasa wa Tanzania ukizingatia kwamba wao ni watanzania na ni wanachama wa CCM na wamezaliwa nchini Tanzania kusoma hapo na kwenda tu nje ili kuongeza maarifa katika fani zao mbalimbali?
Mimi kama Richard sina uanachama wowote katika chama chochote cha siasa na nnapenda kuendelea kuwa "analyst" tu au mfuatiliaji wa mambo mbalimbali lakini nimekuwa nikitatizwa na jambo hili kuhusu kutokubalika kwa watanzania waishio nje kutoka kwa watanzania wenzao.
Je wanaonekana si watanzania, ni wageni na siasa za Tanzania, je watabadilisha mambo mengi ambayo watu wengi hawatapenda kwa nia njema tu au ndio wamekwishapotea kwa wao kuamua kuishi nje ya nchi.
Ningependa kuona hoja mbalimbali zinatolewa kutoka kwa watanzania wenzangu wale walio nyumbani Tanzania na wale wanaoishi nje kwamba nini tatizo hapa.
Nini maoni yako, karibu.
Ni mategemeo ya watanzania wengi ambao wengine wamediriki kujiingiza katika nafasi mbalimbali za uongozi katika matawi ya CCM yalizagaa nje ya nchi hususan Ulaya na Marekani.
Je ni sababu zipi ambazo zinawafanya watanzania hawa kushindwa kuingia kwenye mfumo wa siasa wa Tanzania ukizingatia kwamba wao ni watanzania na ni wanachama wa CCM na wamezaliwa nchini Tanzania kusoma hapo na kwenda tu nje ili kuongeza maarifa katika fani zao mbalimbali?
Mimi kama Richard sina uanachama wowote katika chama chochote cha siasa na nnapenda kuendelea kuwa "analyst" tu au mfuatiliaji wa mambo mbalimbali lakini nimekuwa nikitatizwa na jambo hili kuhusu kutokubalika kwa watanzania waishio nje kutoka kwa watanzania wenzao.
Je wanaonekana si watanzania, ni wageni na siasa za Tanzania, je watabadilisha mambo mengi ambayo watu wengi hawatapenda kwa nia njema tu au ndio wamekwishapotea kwa wao kuamua kuishi nje ya nchi.
Ningependa kuona hoja mbalimbali zinatolewa kutoka kwa watanzania wenzangu wale walio nyumbani Tanzania na wale wanaoishi nje kwamba nini tatizo hapa.
Nini maoni yako, karibu.