zimmerman
JF-Expert Member
- Feb 17, 2011
- 1,628
- 3,155
Hili ni swali lililojitokeza indirectly katika kipindi cha majadiliano cha Star TV Tuongee Asubuhi kuhusiana na mustakabali wa pesa za Rada kurudi Tanzania. Lengo la Star TV lilikuwa ni kupata maoni ya mtanzania wa kawaida kuhusiana na suala hilo. Katika jopo la majadiliano alikuwepo pia Job Ndugai, naibu spika wa bunge la JMT. Huyu ndie aliyeongoza msafara wa wabunge kwenda UK kuzidai hizi hela na maoni yake yalikuwa muhimu ili kupata picha halisi ya kile kinachoendelea.
Sasa katika kuelezea yaliyojiri kwenye msafara wao, Job Ndugai akaulizwa na mwongozaji wa kipindi kuhusiana na wasiwasi walionao watanzania wa kawaida katika suala la hizi pesa kurudi kupitia mkono ule ule uliozipuyanga mwanzo. Na, oh, kitu kipya nilijokifahamu leo tu ni kuwa kumbe hizi pesa ni mkopo kutoka benki ya Barclays (yaani, unachukua mkopo wa riba kununua kifaa kisicho muhimu kwa maendeleo ya msingi ya nchi maskini, what a strange nation!). Tuendelee. Sasa Job akajibu, akasema hata yeye alishangaa pale alipoona analetewa makabrasha ya barua za wazi watanzania walizotuma kupitia mtandao kwa serikali ya UK na BAE kwamba hizo hela bila wasiwasi zitapuyangwa tena kwa sababu bado serikali ni ileile, ya chama kile kile, wezi wale wale waliosafishwa na bunge juzi juzi tu kwamba ni wasafi. Job akashangaa, akawaza, eti inawaezekana watanzania kweli wakakosa uzalendo kiasi hiki, yaani, cha kutoiamini serikali yao kiasi kwamba hata hela za kuwanufaisha watanzania bado hawataki zirudi Tanzania?
Well, kwa kifupi kila mmoja hapa anaweza akawa na majibu yake katika hili; wapo wengine kama Job wanaona ni kukosa uzalendo, na wapo wengine wenye maoni tofauti na Job.
Mimi kwa maoni yangu waliotuma hii barua ya wazi huko Uingereza ni wazalendo, tena sana. Baadhi yao ni watanzania walipa kodi sana tu, baadhi yao wanafanya kazi kwa bidii siku zote wakati mwingine hata Jumamosi na Jumapili na siku za sikukuu bila posho, baadhi yao ni wastaafu walioitumikia nchi hii pengine hata kuhatarisha maisha yao, na hawapingi hizi hela zisirudi Tanzania kuwanufaisha watanzania, ila wanapinga zisirudi kupitia mkono ule ule uliozitapanya. Kama Job Ndugai hawezi kulielewa hili naye ni naibu spika wa bunge, basi, Tanzania tujihesabu hatuna viongozi wanaoelewa mambo ya msingi kwanza.
Sasa katika kuelezea yaliyojiri kwenye msafara wao, Job Ndugai akaulizwa na mwongozaji wa kipindi kuhusiana na wasiwasi walionao watanzania wa kawaida katika suala la hizi pesa kurudi kupitia mkono ule ule uliozipuyanga mwanzo. Na, oh, kitu kipya nilijokifahamu leo tu ni kuwa kumbe hizi pesa ni mkopo kutoka benki ya Barclays (yaani, unachukua mkopo wa riba kununua kifaa kisicho muhimu kwa maendeleo ya msingi ya nchi maskini, what a strange nation!). Tuendelee. Sasa Job akajibu, akasema hata yeye alishangaa pale alipoona analetewa makabrasha ya barua za wazi watanzania walizotuma kupitia mtandao kwa serikali ya UK na BAE kwamba hizo hela bila wasiwasi zitapuyangwa tena kwa sababu bado serikali ni ileile, ya chama kile kile, wezi wale wale waliosafishwa na bunge juzi juzi tu kwamba ni wasafi. Job akashangaa, akawaza, eti inawaezekana watanzania kweli wakakosa uzalendo kiasi hiki, yaani, cha kutoiamini serikali yao kiasi kwamba hata hela za kuwanufaisha watanzania bado hawataki zirudi Tanzania?
Well, kwa kifupi kila mmoja hapa anaweza akawa na majibu yake katika hili; wapo wengine kama Job wanaona ni kukosa uzalendo, na wapo wengine wenye maoni tofauti na Job.
Mimi kwa maoni yangu waliotuma hii barua ya wazi huko Uingereza ni wazalendo, tena sana. Baadhi yao ni watanzania walipa kodi sana tu, baadhi yao wanafanya kazi kwa bidii siku zote wakati mwingine hata Jumamosi na Jumapili na siku za sikukuu bila posho, baadhi yao ni wastaafu walioitumikia nchi hii pengine hata kuhatarisha maisha yao, na hawapingi hizi hela zisirudi Tanzania kuwanufaisha watanzania, ila wanapinga zisirudi kupitia mkono ule ule uliozitapanya. Kama Job Ndugai hawezi kulielewa hili naye ni naibu spika wa bunge, basi, Tanzania tujihesabu hatuna viongozi wanaoelewa mambo ya msingi kwanza.