Je Wassira ni Mzushi au Muongo wa kutupwa?

GIB

JF-Expert Member
Mar 2, 2012
336
92
Soma kwa makini kisha toa maoni yako.
KATIBU Mkuu wa Chadema, Dk Willibrod Slaa jana alitua Arumeru Mashariki na kuhutubia mkutano uliotikisa eneo la Kwapole – Soko la Ndizi, huku wazazi wa mgombea wa chama hicho, Joshua Nassari wakipanda jukwaani kujibu matamshi yaliyotolewa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Uhusiano na Uratibu), Steven Wassira(TYSON) dhidi ya mtoto wao.

Mchungaji Samuel Nassari na mkewe, waliwaambia mamia ya watu waliofika kwenye uwanja huo kuwa walitoa baraka kwa Joshua kugombea nafasi hiyo wakisema mtoto wao ni mwadilifu anayefaa kuwawakilisha wananchi wa Arumeru Mashariki bungeni.

Kauli ya Mchungaji Nassari inatokana na matamshi ambayo yamekuwa yakitolewa na Wassira katika kampeni za kumnadi mgombea wa CCM, Sioi Sumari kwamba mgombea wa Chadema hana nidhamu na kwamba amewachosha wazazi wake kwa kutokuwa na nidhamu.

Lakini jana, baba wa mgombea huyo akiwa na mkewe jukwaani alisema: "Mimi siyo mwanasiasa, lakini nimelazimika kupanda jukwaani leo kutokana na matamshi yaliyotolewa na Wassira, napenda kusema hivi Joshua alipata baraka za familia."

Alisema kabla ya kugombea, Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe alifika nyumbani kwake Songoro na kuwaeleza kuwa wanamtaka Nassari kugombea tena na kusema kwamba familia ilikubali na kumpa baraka zote ikiwa ni pamoja na kuwaita wachungaji kumwombea.

Mchungaji Nassari pia alikanusha madai kwamba mwanaye alikuwa jeuri tangu shule akisema hajawahi kufukuzwa wala kusimamishwa masomo kwa utovu wa nidhamu tangu akiwa shule ya msingi hadi alipohitimu masomo ya shahada, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.

Mchungaji huyo alisema, mtoto wake alisoma katika shule ya msingi, Sekondari ya Bagamoyo kidato cha kwanza hadi cha nne na Shule ya Sekondari ya Wavulana Tabora kidato cha tano na sita.

"Alipokuwa chuo kikuu, ninatambua kwamba alikuwa mtetezi wa wenzake, hivyo ndugu zangu Joshua Nassari anafaa kuwa mbunge na suala kuwa hajaoa halina msingi kwani mke bora mtu anapewa na Mungu na siyo utashi wake au hamu yake, kwani mke siyo kitunguu cha kununua sokoni," alisema Mchungaji Nassari

source : gazeti la mwananchi jumatatu
 
Kuna mambo mengine ya ajabu, Mtu kama wasira (a.k.a. TYSON), anapewa wizara ya mahusiano ambayo mtu anatakiwa kuwa na diplomasia ya hali ya juu ili kukuza mahusiano, lakini yeye wakati wowote anasababisha mahusiano kuharibika. Mimi binafsi simshangai wasira kutamka maneno hayo na labda niwaulize wana JF je tangu huyu TYSON alipoteuliwa katika nafasi hiyo ameshafanya kitu gani ambacho mnafikiri amekuza mahusiano???
 
Kuna mambo mengine ya ajabu, Mtu kama wasira (a.k.a. TYSON), anapewa wizara ya mahusiano ambayo mtu anatakiwa kuwa na diplomasia ya hali ya juu ili kukuza mahusiano, lakini yeye wakati wowote anasababisha mahusiano kuharibika. Mimi binafsi simshangai wasira kutamka maneno hayo na labda niwaulize wana JF je tangu huyu TYSON alipoteuliwa katika nafasi hiyo ameshafanya kitu gani ambacho mnafikiri amekuza mahusiano???

Aliyekosea ni aliyempa wizara hiyo, bora angemuacha kule kule wizara ya chakula.
Huyu mzee hana busara kabisa, ndio sababu kapewa jina la Tyson. Jiulize kwa nini alikimbia NCCR na kurudi magamba?
 
Huyu mzee naona anazeeka vibaya . Sera zimemuisha imebaki kutukana tu. Ashindwe na alegee , tena ashindwe kupotosha
 

Aliyekosea ni aliyempa wizara hiyo, bora angemuacha kule kule wizara ya chakula.
Huyu mzee hana busara kabisa, ndio sababu kapewa jina la Tyson. Jiulize kwa nini alikimbia NCCR na kurudi magamba?

WASIRA is hope less.Unakuza mahusiano kwa kuweka chuki na fitina kwenye jamii!

Lakini siyo makosa yake ULEVI ni NOMAAAAAAAAAAAAAAAAA................
 
Huyu mzee naona anazeeka vibaya . Sera zimemuisha imebaki kutukana tu. Ashindwe na alegee , tena ashindwe kupotosha

Huyu Tyson alikuwa anasinzia jukwaani, kule kuropoka ni ndoto zile alikuwa usingizini. Halafu sura ya huyu mshikaji ipo poa kinoma,vitani huhitaji kupaka masizi!
 
Soma kwa makini kisha toa maoni yako.
KATIBU Mkuu wa Chadema, Dk Willibrod Slaa jana alitua Arumeru Mashariki na kuhutubia mkutano uliotikisa eneo la Kwapole – Soko la Ndizi, huku wazazi wa mgombea wa chama hicho, Joshua Nassari wakipanda jukwaani kujibu matamshi yaliyotolewa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Uhusiano na Uratibu), Steven Wassira(TYSON) dhidi ya mtoto wao.

Mchungaji Samuel Nassari na mkewe, waliwaambia mamia ya watu waliofika kwenye uwanja huo kuwa walitoa baraka kwa Joshua kugombea nafasi hiyo wakisema mtoto wao ni mwadilifu anayefaa kuwawakilisha wananchi wa Arumeru Mashariki bungeni.

Kauli ya Mchungaji Nassari inatokana na matamshi ambayo yamekuwa yakitolewa na Wassira katika kampeni za kumnadi mgombea wa CCM, Sioi Sumari kwamba mgombea wa Chadema hana nidhamu na kwamba amewachosha wazazi wake kwa kutokuwa na nidhamu.

Lakini jana, baba wa mgombea huyo akiwa na mkewe jukwaani alisema: "Mimi siyo mwanasiasa, lakini nimelazimika kupanda jukwaani leo kutokana na matamshi yaliyotolewa na Wassira, napenda kusema hivi Joshua alipata baraka za familia."

Alisema kabla ya kugombea, Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe alifika nyumbani kwake Songoro na kuwaeleza kuwa wanamtaka Nassari kugombea tena na kusema kwamba familia ilikubali na kumpa baraka zote ikiwa ni pamoja na kuwaita wachungaji kumwombea.

Mchungaji Nassari pia alikanusha madai kwamba mwanaye alikuwa jeuri tangu shule akisema hajawahi kufukuzwa wala kusimamishwa masomo kwa utovu wa nidhamu tangu akiwa shule ya msingi hadi alipohitimu masomo ya shahada, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.

Mchungaji huyo alisema, mtoto wake alisoma katika shule ya msingi, Sekondari ya Bagamoyo kidato cha kwanza hadi cha nne na Shule ya Sekondari ya Wavulana Tabora kidato cha tano na sita.

"Alipokuwa chuo kikuu, ninatambua kwamba alikuwa mtetezi wa wenzake, hivyo ndugu zangu Joshua Nassari anafaa kuwa mbunge na suala kuwa hajaoa halina msingi kwani mke bora mtu anapewa na Mungu na siyo utashi wake au hamu yake, kwani mke siyo kitunguu cha kununua sokoni," alisema Mchungaji Nassari

source : gazeti la mwananchi jumatatu
Hawa magamba bado hawajapata pointi ya kuwateka watu wa Arumeru kwa hiyo bado wanapapasa gizani kutafuta cha kuwaambia wana Arumeru, maana Igunga walitumia udini sasa huko pamekuwa pagumu zaidi ya kuongea matusi tu.
 
Soma kwa makini kisha toa maoni yako.
KATIBU Mkuu wa Chadema, Dk Willibrod Slaa jana alitua Arumeru Mashariki na kuhutubia mkutano uliotikisa eneo la Kwapole – Soko la Ndizi, huku wazazi wa mgombea wa chama hicho, Joshua Nassari wakipanda jukwaani kujibu matamshi yaliyotolewa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Uhusiano na Uratibu), Steven Wassira(TYSON) dhidi ya mtoto wao.

Mchungaji Samuel Nassari na mkewe, waliwaambia mamia ya watu waliofika kwenye uwanja huo kuwa walitoa baraka kwa Joshua kugombea nafasi hiyo wakisema mtoto wao ni mwadilifu anayefaa kuwawakilisha wananchi wa Arumeru Mashariki bungeni.

Kauli ya Mchungaji Nassari inatokana na matamshi ambayo yamekuwa yakitolewa na Wassira katika kampeni za kumnadi mgombea wa CCM, Sioi Sumari kwamba mgombea wa Chadema hana nidhamu na kwamba amewachosha wazazi wake kwa kutokuwa na nidhamu.

Lakini jana, baba wa mgombea huyo akiwa na mkewe jukwaani alisema: "Mimi siyo mwanasiasa, lakini nimelazimika kupanda jukwaani leo kutokana na matamshi yaliyotolewa na Wassira, napenda kusema hivi Joshua alipata baraka za familia."

Alisema kabla ya kugombea, Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe alifika nyumbani kwake Songoro na kuwaeleza kuwa wanamtaka Nassari kugombea tena na kusema kwamba familia ilikubali na kumpa baraka zote ikiwa ni pamoja na kuwaita wachungaji kumwombea.

Mchungaji Nassari pia alikanusha madai kwamba mwanaye alikuwa jeuri tangu shule akisema hajawahi kufukuzwa wala kusimamishwa masomo kwa utovu wa nidhamu tangu akiwa shule ya msingi hadi alipohitimu masomo ya shahada, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.

Mchungaji huyo alisema, mtoto wake alisoma katika shule ya msingi, Sekondari ya Bagamoyo kidato cha kwanza hadi cha nne na Shule ya Sekondari ya Wavulana Tabora kidato cha tano na sita.

"Alipokuwa chuo kikuu, ninatambua kwamba alikuwa mtetezi wa wenzake, hivyo ndugu zangu Joshua Nassari anafaa kuwa mbunge na suala kuwa hajaoa halina msingi kwani mke bora mtu anapewa na Mungu na siyo utashi wake au hamu yake, kwani mke siyo kitunguu cha kununua sokoni," alisema Mchungaji Nassari

source : gazeti la mwananchi jumatatu
Asingekuwa mwanasiasa asingepanda Jukwaani, angeongelea kwenye media.
 
Asingekuwa mwanasiasa asingepanda Jukwaani, angeongelea kwenye media.

Nahisi harufu ya magamba! Yani kijana wako achafuliwe kwenye jukwaa la siasa alafu wewe kukanusha uende kwenye media wakati anatafuta kura na ana baraka zako!¿ Huo ni uvivu wa kufikiri na ndilo tatizo kubwa la utawala wetu.
 
3961196263_cc5c8a2753_o.jpg
 
Wasira bado yupo usingizini jamani naomba mwenye ile picha anayokoroma bungeni. Unategemea ataongea nini? Kachoka hana hata moja kichwani.
 

Aliyekosea ni aliyempa wizara hiyo, bora angemuacha kule kule wizara ya chakula.
Huyu mzee hana busara kabisa, ndio sababu kapewa jina la Tyson. Jiulize kwa nini alikimbia NCCR na kurudi magamba?

Mkuu, huko NCCR alienda kwa kazi maalum alipoikamilisha akarudi kwa aliyemtuma kazi!
 
Back
Top Bottom