Je, viongozi wa Afrika wana matatizo ya vinasaba?

The Planner

JF-Expert Member
Dec 1, 2010
357
118
Professor Watson, mtaalam aliyebobea katika mambo ya vinasaba (DNA), alitueleza kuwa watu weusi tunavinasaba inferior kulinganisha na watu weupe, ilizua mjadala ambao ulijikita katika mazingira ya ubaguzi wa rangi kwa kiwango kikubwa, kwanza ukitafakari kuwa tuna wataalam wenye ngozi nyeusi waliobobea wagunduzi wa mifumo mbalimbali mfano kina EMEAGWALI, kina IMHOTEP na wengineo tuna viongozi wenye rangi nyeusi mfano Nkrumah, Nnandi Azikiwe, Mwl. Nyerere na Obama yani tunamengi ya kumprove wrong Watson, BUT kuna watu ndani ya hii ngozi nyeusi wanafanya findings za huyu bwana zionenye ni Significant, Baadhi ya viongozi wa Africa kwa mfano huyu Laurent Gbagbo anataka jumuia ya kimataifa ituone vipi zaidi ya kuproove kilichosemwa na Watson. Kuna gwiji mwingine pale Senega anayeitwa Wade huyu alitoa wazo la kujengwa sanamu kubwa kwa pesa za serikali yake ili sanamu hiyo itumike kama sehemu ya utalii na kuliingizia pato taifa, ghafla akazuka na kutaka 30% ya mapato iwe mali yake na familia yake, simply because yeye ndo aliyetoa wazo. Watson anahitaji nini zaidi?
 
Sahihisho;

Huyo EMEAGWALI umekosea, siyo kichwa kama anavyojitangaza mwenyewe.
 
Back
Top Bottom