Chief lubengulla
Member
- Oct 16, 2012
- 15
- 2
Nimeanza na swali nikiwa sielewi maana halisi ya Umoja Wa wanawake Tanzania hasa ukuzingatia muda tulio nao kwa sasa tupo kwenye vyama vingi lakini cha kushangaza mama zetu ukiangalia siku ya uchaguzi wao walivalia nguo zenye rangi ya chama cha CCM yaani kijani na njano wengine mnaweza mkaleta utani mkasema pia hata timu ya Yanga wanatumia rangi hizo hizo. Maana yangu kuleta habari hii ni kuwakumbusha akina mama wa Tanzania waende na wakati itafika kipindi umoja wao utaishiwa wanachama wabadilike maana halisi ya Uomoja wao wanaupotosha labda wangeliita Umoja Wa Wanawake CCM Tanzania hapo tungelienda sawa sawia kabisa.