Je, ushindi wa Albashir Sudan ni goli la kisigino kwa ICC??!!...

Sajenti

JF-Expert Member
Apr 24, 2008
3,651
412
Tume ya uchaguzi nchini Sudan imemtangaza Rais Omar Albashir kuwa mshindi katika uchaguzi uliogomea na baadhi ya vyama vya upinzani nchini humo. Albashir ambaye amekuwa akituhumiwa kwa makosa ya kukiuka haki za binadamu na hasa katika eneo la Darfur nchini Sudan amewabeza wale wote waliosusia uchaguz huo na kuwaita ni vibaraka wa nchi za magharibi. Mahakama ya kimataifa ya makosa ya jinai (ICC) ilitoa hati ya kukamatwa kwa Omar Albashir. Je kutangazwa kuwa mshindi kunafuta uhalali wa hati ya kukamatwa kwake??
 
Tume ya uchaguzi nchini Sudan imemtangaza Rais Omar Albashir kuwa mshindi katika uchaguzi uliogomea na baadhi ya vyama vya upinzani nchini humo. Albashir ambaye amekuwa akituhumiwa kwa makosa ya kukiuka haki za binadamu na hasa katika eneo la Darfur nchini Sudan amewabeza wale wote waliosusia uchaguz huo na kuwaita ni vibaraka wa nchi za magharibi. Mahakama ya kimataifa ya makosa ya jinai (ICC) ilitoa hati ya kukamatwa kwa Omar Albashir. Je kutangazwa kuwa mshindi kunafuta uhalali wa hati ya kukamatwa kwake??

Mkuu Sajenti,

Ushindi wa uchaguzi wa ndani ni kitu kimoja na mashtaka ya ICC ni kitu kingine. Kuchaguliwa kwake katika mazingira ya uchaguzi wenyewe ulivyoendeshwa hakuleti picha halisi hata kidogo ya kuonyesha kwamba serikali yake haikuendesha mauaji ya Raia kule Darfur kupitia kundi la Janjaweed.

Kwa chaguzi zetu katika nchi nyingi za Africa, hata ukiweka "gogo la mti" kama mgombea linaweza kutangazwa kuwa limeshinda!!!!

Tiba
 
Tiba, nakubaliana na wewe katika hilo ingawa bado kiasi fulani napata mashaka na ufanisi wa ICC katika utendaji wake. Kama uamuzi wa kukamata viongozi waliofanya mauaji ya kimbari ni kwa viongozi wa afrika tu au vipi. Bado najiuliza mpaka leo jinsi Marekani na washirika wake chini ya utawala wa Bush walivyoivamia Iraq, kabla ya kumkamata Saddam wananchi wengi waliuwawa kwa kisingizio cha kutafuta silaha za maangamzi ambazo hazikuwepo na mwishowe hata Tonny Blair alikiri kuwa alipotoshwa na washauri wake kiasi cha kubanwa na bunge la Uingereza kwa nini aliingiza nchi kwenye vita bila ya kuwa na detailed information. So kwa maoni yangu nadhani hata kama ICC bado itamkamata Albashir sioni kama ni haki ukizingatia hii migogoro katika nchi nyingi za kiafrika mingi ina mkono wa nchi za magharibi..
 
slobodan milosevic, ronadan caradcic etc si waafrika though i aree with you kuna double standard kiasi flan
 
Uchaguzi ulisusiwa na wapinzani wake hivyo kama wapinzani wamesusia na akapata 68% wangeshiriki si angepata kidogo zaidi? Bado ametumia dola katika uchaguzi huo na hata 70% hajapata na wapinzani wa urais waliususia, je wangeshiriki na ungekuwa free and fair elections, nahisi angepata wakati mgumu sana kupata ushindi.
 
Uchaguzi ulisusiwa na wapinzani wake hivyo kama wapinzani wamesusia na akapata 68% wangeshiriki si angepata kidogo zaidi? Bado ametumia dola katika uchaguzi huo na hata 70% hajapata na wapinzani wa urais waliususia, je wangeshiriki na ungekuwa free and fair elections, nahisi angepata wakati mgumu sana kupata ushindi.
..That's very interesting Nanu, Nakubaliana na wewe kabisa. Unajuwa watu wengi hawaelewi kuwa njia ya kumtoa mtu madarakani kidemokrasia si kugomea uchaguzi bali wanatakiwa wapige kura na kumpa kura za hapana ili kumtoa. Lakini kususia uchaguzi ni kumpa urahisi wa ushindi. But ninachojaribu kudodosa ni kuhusiana na huu ushindi wa Albashir na sakata la kutakiwa kukamatwa na ICC, hata jana niliona kwenye TV akijinadi kuwa ushindi wake ni ishara tosha kuwa wananchi wa Sudan wanamkubali na ni fundisho kwa ICC kutaka kuingiza ubeberu Sudan na jana alisafiri kwenda Misri na kuonana na Raisi Mubarak.....Unasemaje hapo??
 
ICC role is very interesting, It is double sword. On one hand it is good for those who commits or think to commit atrocities to their own people to know that there is reckoning, on the other hand ICC is used as by big powers to punish those leaders they don’t like while no leader of these big powers or their favourite dictators can be brought to justice. ICC together with UN and WTO are colonialist tools to rule the world without being seen to rule. One veto at UN is enough to si ence 190 other countries !!
 
Back
Top Bottom