Gwaje
JF-Expert Member
- Nov 4, 2010
- 299
- 85
Imenilazimu niongelee hali ya siasa hapa tanzania kwani kuna haya yanayonitatiza, nami naamini ndani ya jamvi hili nitapata kuelimishwa ipaswavyo.
Miezi ya hapo kati maalimu seif sharif hamad alifanya mazungumzo ya siri na aliyekuwa rais wa zanzibar aman karume, matokeo ya mazungumzo yao ikawa ni muafaka yaani walikubariana. Msingi wa mazungumzo ulikuwa ni siri baina yao.
31 october 2010 wazanzibar walipiga kura wakiwa na kiu ya kuchagua viongozi wapya. Akiwemo seif, cha ajabu kwangu huyu seif aliye kuwa akikataa matokeo mara nyingi amekubali haraka wakati huu. Kitendo hiki kimenipa kujiuliza yafuatayo:-
1. Je muafaka wa zanzibar ni wa seif na karume ama muafaka wa ccm na cuf? Ama ni maridhiano ya wazanzibar iliwajenge nchi yao? Je wazanzibar hawa wamekuwa wanahusika kweli kwenye malidhiano haya?
2. Miaka iliyopita seif alikuwa anatumia mbinu gani kujua kwamba ameibiwa kura? Je wananchi wapo piga kura kura hizo huwa ni za nani? Mgombea au waliopiga kura?
3. Je huyu seif vigezo gani amabavyo vimemridhisha aone kashindwa kweli awamu hii?
4. Kwanini seif asishitakiwe kwenye mahakama ya kivita kwa mauaji ya 2000?
5. Haya maMbo ya vyama je yako kwa ajili ya mwanachama ama kwa maslahi ya viongozi kama seif?
Yapo maswali mengi naomba nijengewe uwezo walau kwa hayo.
Miezi ya hapo kati maalimu seif sharif hamad alifanya mazungumzo ya siri na aliyekuwa rais wa zanzibar aman karume, matokeo ya mazungumzo yao ikawa ni muafaka yaani walikubariana. Msingi wa mazungumzo ulikuwa ni siri baina yao.
31 october 2010 wazanzibar walipiga kura wakiwa na kiu ya kuchagua viongozi wapya. Akiwemo seif, cha ajabu kwangu huyu seif aliye kuwa akikataa matokeo mara nyingi amekubali haraka wakati huu. Kitendo hiki kimenipa kujiuliza yafuatayo:-
1. Je muafaka wa zanzibar ni wa seif na karume ama muafaka wa ccm na cuf? Ama ni maridhiano ya wazanzibar iliwajenge nchi yao? Je wazanzibar hawa wamekuwa wanahusika kweli kwenye malidhiano haya?
2. Miaka iliyopita seif alikuwa anatumia mbinu gani kujua kwamba ameibiwa kura? Je wananchi wapo piga kura kura hizo huwa ni za nani? Mgombea au waliopiga kura?
3. Je huyu seif vigezo gani amabavyo vimemridhisha aone kashindwa kweli awamu hii?
4. Kwanini seif asishitakiwe kwenye mahakama ya kivita kwa mauaji ya 2000?
5. Haya maMbo ya vyama je yako kwa ajili ya mwanachama ama kwa maslahi ya viongozi kama seif?
Yapo maswali mengi naomba nijengewe uwezo walau kwa hayo.