Jatropha
JF-Expert Member
- Apr 9, 2009
- 1,151
- 199
Kifungu cha 63 cha Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kinaanisha wazi majukumu ya Mbunge kuwa "Kuisimamia na Kuishauri Serikali". Maana yake ni kuwa haiwezekani watanzania wote tukaende bungeni kuismiamia serikali.
Hivyo kila jimbo hutoa mwakilishi mmoja ili kwenda kuisimamia serikali
katika ukusanyaji wa mapato wa serikali ili fedha nyingi zaidi ziweze kupatikana kutoka vyanzo mbali mbali kama vile kodi za iana mbali mbali, raslimali, madini, utalii, biashara n.k;na kutunzwa vyema. Na pia mwakilishi huyo wa wananchi wa jimbo aweze kuisimamia serikali katika matumizi ili fedha nyingi zaidi ziweze kuelekezwa katika miradi ya maendeleo yenye tija kwa wananchi badala ya hali ilivyo sasa ambapo kiwango kikubwa cha fedha zinazokusanywa na serikali hutumika kugharimia mishahara, posho, safari, warsha, semina, mikutano na gharama zingine za uendshaji zisizo za lazima kama vile serikali kununua magari makubwa na mengi sana ya kifahari n.k. Hii inatokana na serikali ya Tanzania kukosa kusimamiwa na wawakilishi wa wananchi baada ya wawakilishi wetu (wabunge) kugeuka ni wabunge majimbo yaani wasaka maendeleo ya majimbo badala ya wabunge Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wenye dhamana ya kuisiamamia serikali.
Ili Mbunge mwenye jukumu la kuisimamia serikali aweze "kuisimamia na kuishauri serikali" ni lazima awe mtafiti na mfuatiliaji ili aweze kuja bungeni akiwa na taarifa sahihi na zilizotafitiwa vyema. Shughuli hiyo ni lazima itatumia muda mwingi wa Mbunge kuliko anavyoweza kushughulikia masuala ya jimbo lake pekee.
Kwa ilivyo sasa ndani ya Bunge letuili Mbunge aweze kupata miradi mbali mbali ya maendeleo kwa jimbo lake ni lazima ajikombe na kujibembeleza kwa mawaziri wa serikali ambayo anatakiwa kuwasimamia katika ukusanyaji na matumizi ya fedha. Hali inayodhoofisha dhana nzima ya wabunge kuwa wawakilishi wa wananchi wenye dhamana ya kuisimamia serikali.
Athari za kuwa na wabunge majimbo yaani wale wanaojishughulisha na kutafuta maendeleo ya majimbo yao pekee na sio maendeleo ya kitaifa ni kuiacha serikali bila usimamizi hivyo viongozi na watendaji wa serikali kujifanyia wapendavyo katika ukusanyaji na matumizi ya fedha za serikali; matokeo yake ni nchi na wananchi wake kuendelea kugubikwa katika lindi la umaskini katika nchi ya maziwa na asali hata baada ya miaka 50 kutokea tupate uhuru.
Serikali kukosa kusimamiwa kushamirisha ufisadi baada ya viongozi na watendaji wa serikali kutumia nyadhifa zao kujinufaisha hivyo kuhujumu mapato ya serikali; na fedha kidogo zilizokusanywa kufujwa bila kuwaletea wananchi maendeleo yaliyokusudiwa mifano halisi ya hali hiyo ni miradi sub-standard iliyotapakaa nchi nzima na kuwakosesha wananchi huduma zilizotarajiwa. Baada kufisadi mapato na na fedha za serikali wabunge majimbo wanaojikomba kwa viongozi na watendaji wa serikali mafisadi humegewa fedha kidogo kati ya nyingi zilizoibiwa kutoka serikalini kwa ajili ya kupeleka miradi kiduchu ya maendeleo katika majimbo yao ili waweze kuchaguliwa tena ili waendeleze kuunga mkono ufisadi ndani ya chombo cha wananchi cha kuismiama serikali.
Je wewe mwana JF ungependa Mbunge wako awe ni Mbunge Jimbo au Mbunge Taifa?
Hivyo kila jimbo hutoa mwakilishi mmoja ili kwenda kuisimamia serikali
katika ukusanyaji wa mapato wa serikali ili fedha nyingi zaidi ziweze kupatikana kutoka vyanzo mbali mbali kama vile kodi za iana mbali mbali, raslimali, madini, utalii, biashara n.k;na kutunzwa vyema. Na pia mwakilishi huyo wa wananchi wa jimbo aweze kuisimamia serikali katika matumizi ili fedha nyingi zaidi ziweze kuelekezwa katika miradi ya maendeleo yenye tija kwa wananchi badala ya hali ilivyo sasa ambapo kiwango kikubwa cha fedha zinazokusanywa na serikali hutumika kugharimia mishahara, posho, safari, warsha, semina, mikutano na gharama zingine za uendshaji zisizo za lazima kama vile serikali kununua magari makubwa na mengi sana ya kifahari n.k. Hii inatokana na serikali ya Tanzania kukosa kusimamiwa na wawakilishi wa wananchi baada ya wawakilishi wetu (wabunge) kugeuka ni wabunge majimbo yaani wasaka maendeleo ya majimbo badala ya wabunge Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wenye dhamana ya kuisiamamia serikali.
Ili Mbunge mwenye jukumu la kuisimamia serikali aweze "kuisimamia na kuishauri serikali" ni lazima awe mtafiti na mfuatiliaji ili aweze kuja bungeni akiwa na taarifa sahihi na zilizotafitiwa vyema. Shughuli hiyo ni lazima itatumia muda mwingi wa Mbunge kuliko anavyoweza kushughulikia masuala ya jimbo lake pekee.
Kwa ilivyo sasa ndani ya Bunge letuili Mbunge aweze kupata miradi mbali mbali ya maendeleo kwa jimbo lake ni lazima ajikombe na kujibembeleza kwa mawaziri wa serikali ambayo anatakiwa kuwasimamia katika ukusanyaji na matumizi ya fedha. Hali inayodhoofisha dhana nzima ya wabunge kuwa wawakilishi wa wananchi wenye dhamana ya kuisimamia serikali.
Athari za kuwa na wabunge majimbo yaani wale wanaojishughulisha na kutafuta maendeleo ya majimbo yao pekee na sio maendeleo ya kitaifa ni kuiacha serikali bila usimamizi hivyo viongozi na watendaji wa serikali kujifanyia wapendavyo katika ukusanyaji na matumizi ya fedha za serikali; matokeo yake ni nchi na wananchi wake kuendelea kugubikwa katika lindi la umaskini katika nchi ya maziwa na asali hata baada ya miaka 50 kutokea tupate uhuru.
Serikali kukosa kusimamiwa kushamirisha ufisadi baada ya viongozi na watendaji wa serikali kutumia nyadhifa zao kujinufaisha hivyo kuhujumu mapato ya serikali; na fedha kidogo zilizokusanywa kufujwa bila kuwaletea wananchi maendeleo yaliyokusudiwa mifano halisi ya hali hiyo ni miradi sub-standard iliyotapakaa nchi nzima na kuwakosesha wananchi huduma zilizotarajiwa. Baada kufisadi mapato na na fedha za serikali wabunge majimbo wanaojikomba kwa viongozi na watendaji wa serikali mafisadi humegewa fedha kidogo kati ya nyingi zilizoibiwa kutoka serikalini kwa ajili ya kupeleka miradi kiduchu ya maendeleo katika majimbo yao ili waweze kuchaguliwa tena ili waendeleze kuunga mkono ufisadi ndani ya chombo cha wananchi cha kuismiama serikali.
Je wewe mwana JF ungependa Mbunge wako awe ni Mbunge Jimbo au Mbunge Taifa?