DEVINE
JF-Expert Member
- Mar 11, 2011
- 536
- 86
....Baada ya mpenzi wako kutoka kwenda uwani,unafungua simu yake kama kumchunguza ktk (inbox) unakuta ujumbe huu... "...Honey am sorry,ukweli nilikosa jinsi ya kuwasiliana na wewe kwa kweli ,naogopa hata kuonana na wewe usoni najua ulikuwa ukinitafuta sana ila kwa sasa nimeamua kumrudia mungu na kujikaza kisabuni kukuandikia haya,ila nafsi inanisuta ninaomba sana msamaha wako,najua umeshtushwa na ujumbe huu.Ila Samahani nilijua nitakuumiza tu kwa taarifa hii yangu kwako. Naomba utambue nakupenda sana ila ishatokea pokea kama ilivyo,mimi kwa sasa ni muathirika wa virusi vya ukimwi.Najua hata wewe utakuwa navyo tu,kwani tumeshiriki tendo la ndoa mara nyingi sana na si ivyo tu wewe ndiye wa mwisho niliye shiriki nawe..Nisamehe kwani nilikuwa na wapenzi wengi pamoja nawe,ila wewe ndiye niliye kupenda sana ila ishatokea nimekupa gonjwa kwama malipo ya penzi lako kwangu.Nisamehe kwani yalishatokea na kupata virusi sio mwisho wa maisha..Nikushauri tu kawaone wataalam wa afya kama nilivyo fanya mimi,pia umrudie Mungu achana na ngono zembe...." .
=>wakati unausoma ujumbe huo ni dakika chache tu mmetoka ku-enjoy tendo bila kinga,je utafanya nini kama maamuzi yako ya awali?
=>wakati unausoma ujumbe huo ni dakika chache tu mmetoka ku-enjoy tendo bila kinga,je utafanya nini kama maamuzi yako ya awali?