Je, unataka kulima mazao ya mbogamboga na matunda lakini unakosa maarifa sahihi? Karibu tushauriane

Status
Not open for further replies.
NZI WA MATUNDA, Hushambulia matikiti, machungwa, apple, peas, parachichi na nyanya
upload_2016-10-1_21-38-1.png
 
CHUKUA TAHADHARI WAKATI UNAPOWEKA MBOLEA AU KUPIGA DAWA ZA WADUDU SHAMBANI

1. Hakikisha kabla ya kuweka mbolea shambani, kwanza unamwagia shamba maji KWANZA, Weka mbolea na uifukie na udongo, kama ni mbolea ya kukuzi miche iweke umbali wa sm 5 kutoka shina kutegemea na aina ya zao.
=Usipokuwa makini utakausha mazao yako, weka mbolea kwa kipimo sahihi
2. Hakikisha kabla ya kupiga dawa za wadudu , shamba liwe limemwagiwa maji/lina unyevu wa kutosha
=Weka dawa kwa kipimo sahihi
3. Usitumie dawa ya wadudu bila kujua kilichokuwemo ndani (Kiambata aminifu/Guarentee)
4. Kama umeazima bomba la kupulizia dawa, kabla ya kulitumia lioshe kwa maji safi na sabuni mara tatu kabla ya kulitumia, kwani kuna uwezekano linamabaki ya sumu za kukaushia nyasi kama Round up, utakausha mazao yako kwa uzembe
5.Epuka kuweka maji shambani, yanayoweza kulala shambani kwa siku 3-5 mfululizo. Maji yakituama kwa wingi, husababisha mizizi kushindwa kupumua, na pia huleta fangasi, na kuoza mizizi.

 
MPYA......12/10/2016
NJIA RAHISI YA KUWEZESHA MBEGU KUOTA HARAKA (HASA MBEGU ZA HOHO)


Hoho ni moja wapo ya zao ambalo mbegu zake huchelewa sana kuota, huchukua siku 14 hadi 28 kuota

Zifuatzo ni njia unazoweza kufanya ili kuwezesha mbegu zako kuota mapema kaba ya kuzisia kitaluni.

1. Chukua mbegu zako toka katika kikopo/kifungashio chake, weka mbegu hizo katika kitambaa laini kisha zifunge humo
2. Andaa maji masafi katika chombo kama beseni, au ndoo kisha weka zile mbegu zilizofungwa ndani ya kitambaa ziweke katika hayo maji,
3.Ziloweke humo, Funika chombo hicho/ kiweke mbali na watoto sehemu tulivu isiwe juani, ziache humo hadi baada ya siku 4
4. Baada ya siku 4 kupita (Yaani siku ya tano) zichukue zile mbegu bado zikiwa zimefungwa katika kitambaa chake, sasa zihamishie zile mbegu bado zikiwa zimefungwa na kitambaa chake, ziweke katika mfuko wa lailoni wa rangi yoyote ile, iwe rangi nyeusi au bluu, ziweke humo hizo mbegu kisha funga huo mfuko, na zifunike na chombo chochote kama ndoo, au beseni, sifuria au chungu, zifunike kwa muda wa siku 4, siku ya tano ukizifunua, ukafungua mfuko (lailoni) na kitambaa utakuta zile mbegu tayari zimeanza kuota kama vile mbegu za mtama/ulezi (kimea)
5. Kisha chukua mbegu hizo, njoo uzisie katika kitalu chako ulichokuwa umekiandaa mapema (Ni vyema kitalu kikawa kimeandaliwa mapema wiki 2-3 kabla ya kusia mbegu), mbegu hizo utazimwaga katika vimifereji vilivyoachana umbali wa sentimita 5-10, utasia mbegu hizo kwa kudondosha kidogo kidogo kisha kuzifukia na tabaka laini la udongo. Weka matandazwa (Nyasi kavu) juu yake, kisha Mwagia maji kiasi kwa muda wa siku 3-4 mfulululizo, Baada ya siku 3-4 mbegu zitakuwa zimechipuka/kuota. Mbegu zitakaa kitaluni siku 14-28 kisha utazihamishia shambani.
===
upload_2016-10-12_11-52-24.png

upload_2016-10-12_11-52-43.png


Miche ya hoho, ikiwa na wiki moja kitaluni tangu ziote. Kitalu kiliandaliwa wiki 2 kabla ya kusia mbegu, ambapo udongo ulichanganywa na samadi ng'ombe iliyopoa miezi 3 kabla ya kutumika.Upana wa kitalu ni mita 1, kwenye kila eneo la mraba la mita 1, kuliwekwa samadi debe 1. Mbegu zilizotumika ni jamii ya OPV, aina ya Pop vried vegetable seed-Kampuni ya Kiholanzi
 
Habari mkuu.. naomba ushauri wa mambo mawili..

1. Nimepanda mbegu za tikiti na baada ya siku nne zimeota kama 70% hivi. Hizi ambazo hazijatoka niendelee kungoja au nirudishie mbegu zingine..

2. Naomba nishauri nini hii kwenye hizi papai ni ungojwa au? Mwanzo zilikua na wadudu weupe hivi nikatumia Confidor wakaisha wote lakini sielewi huu ni mnyauko wa nini..
1476509677629.jpg
1476509696001.jpg
 
KARIBU
1. KUHUSU MBEGU ZA TIKITI KUOTA
=Kwa kawaida tikiti zinapaswa kuota ndani ya siku 7. Subiri kwa ziada ya siku 5 kutoka leo, ikifika maximum siku ya 10 tangu ulipozisia na zikawa hazijaota, basi pita katika yale mashimo ambapo hazijaota, kisha fukua kuangalia kama zipo hizo mbegu na zina hali gani, mara nyingi huwa tayari zimebunguliwa na wadudu au ukungu. Hivyo itakupasa kurudia kupanda tena

SWALI; Je ulizitibu hizi mbegu zako kabla ya kuzipanda?? Kuna dawa ambazo ni muhimu kumix na mbegu kabla ya kupanda, ili kuzuia changamoto za nematodes, au wadudu au fanagasi kuzishambulia kabla ya kuota

2.KUHUSU MICHE YA PAPAI
Tutakuuliza maswali kadhaa hapo chini, LAKINI

=Kuna baadhi ya matatizo yako wazi

i. Picha ya kwanza ya juu kuna miche majani ya chini (OLder leaves) ni ya Njano, hiyo ni dalili ya wazi kabisa ya upungufu wa Nitrogen (N), na utaona inaanza kuwa ya njano nchani (Tip) mwa jani kushuka chini, angalia miche miwili ya mstari wa mwisho kwenye hiyo picha ya kwanza angalia huo unjano umekolea sana hapo nchani mwa jani kuja chini huku katika kikonyo/mwanzo mwa tawi/jani

ii. Pia kuna miche inaonekana baadhi ya majani yamekauka kabisa, mfano mstari wa pili kutoka kaskazini kuja kusini, angalia mche wa kwanza, wa pili na wa tatu kutoka kulia kuja kushoto, utaona majani yamekauka kwa kuanzia katika ncha kuja chini. Hiyo ni dalili ya wazi kabisa ya upungufu wa Potassium (K). Na utaona hata ukuaji wa hiyo miche si mzuri imedumaa.

ANGALIA PICHA YA PILI (AMBAYO MAJANI YAKE HAYAKO VIZURI-YAMEJIKUNJA/Filiform)
Muda si mrefu sana hayo majani yatakuwa hivi (Unjano katika vena za majani)

upload_2016-10-15_12-39-28.png

Huo ni ugonjwa huitwa Papaya Ringspot diseases/Papaya Ringspot Virus

Huenezwa na wadudu waitwao Aphids/Wadudu mafuta
Mche wa namna hiyo hata ukizaa matunda yake huwa na mabaka baka/mashiringi
upload_2016-10-15_12-42-50.png
upload_2016-10-15_12-51-45.png


KABLA HATUJAKUSAHURI CHA KUFANYA, TUNAOMBA KUFAHAMU YAFUATAYO

1. Maganement/Matunzo ambazo tayari umeshayafanya shambani, yaani tangu kuandaa mashimo mpaka sasa umefanya nini na nini, ie. Ulipandia mbolea gani??, umeshaweka mbolea zipi tena mpaka sasa, JE UKIACHA CONFIDOR kuna viuatilifu gani umeshapiga hapo shambani?/

2. Je umewahi kupiga booster zozote??

3. Hizo dawa za wadudu unapiga kila baada ya muda gani??

4.Napsack Sprayer (Bomba) unalotumia kupulizia dawa ni lako?/ au unaazima kwa jirani (Eleza ukweli)

5.Uwekaji wako wa maji ukoje, unaweka mara ngapi maji kwa wiki, na ni wastani wa lita ngapi kwa mche kwa siku/wiki?? etc

KARIBU

===================================

Habari mkuu.. naomba ushauri wa mambo mawili..

1. Nimepanda mbegu za tikiti na baada ya siku nne zimeota kama 70% hivi. Hizi ambazo hazijatoka niendelee kungoja au nirudishie mbegu zingine..

2. Naomba nishauri nini hii kwenye hizi papai ni ungojwa au? Mwanzo zilikua na wadudu weupe hivi nikatumia Confidor wakaisha wote lakini sielewi huu ni mnyauko wa nini..View attachment 418291View attachment 418293
 
KARIBU
1. KUHUSU MBEGU ZA TIKITI KUOTA
=Kwa kawaida tikiti zinapaswa kuota ndani ya siku 7. Subiri kwa ziada ya siku 5 kutoka leo, ikifika maximum siku ya 10 tangu ulipozisia na zikawa hazijaota, basi pita katika yale mashimo ambapo hazijaota, kisha fukua kuangalia kama zipo hizo mbegu na zina hali gani, mara nyingi huwa tayari zimebunguliwa na wadudu au ukungu. Hivyo itakupasa kurudia kupanda tena

SWALI; Je ulizitibu hizi mbegu zako kabla ya kuzipanda?? Kuna dawa ambazo ni muhimu kumix na mbegu kabla ya kupanda, ili kuzuia changamoto za nematodes, au wadudu au fanagasi kuzishambulia kabla ya kuota NIMETUMIA MBEGU AMBAZO ZIKO TREATED ALREADY (SUGAR KING) KWAHIO SIKUONA HAJA YA KUZITIBU MBEGU TENA SABABU NIMESOMA MOJA YA MAANDIKI YAKO UMESHAURI HILI

2.KUHUSU MICHE YA PAPAI
Tutakuuliza maswali kadhaa hapo chini, LAKINI

=Kuna baadhi ya matatizo yako wazi

i. Picha ya kwanza ya juu kuna miche majani ya chini (OLder leaves) ni ya Njano, hiyo ni dalili ya wazi kabisa ya upungufu wa Nitrogen (N), na utaona inaanza kuwa ya njano nchani (Tip) mwa jani kushuka chini, angalia miche miwili ya mstari wa mwisho kwenye hiyo picha ya kwanza angalia huo unjano umekolea sana hapo nchani mwa jani kuja chini huku katika kikonyo/mwanzo mwa tawi/jani

ii. Pia kuna miche inaonekana baadhi ya majani yamekauka kabisa, mfano mstari wa pili kutoka kaskazini kuja kusini, angalia mche wa kwanza, wa pili na wa tatu kutoka kulia kuja kushoto, utaona majani yamekauka kwa kuanzia katika ncha kuja chini. Hiyo ni dalili ya wazi kabisa ya upungufu wa Potassium (K). Na utaona hata ukuaji wa hiyo miche si mzuri imedumaa.

ANGALIA PICHA YA PILI (AMBAYO MAJANI YAKE HAYAKO VIZURI-YAMEJIKUNJA/Filiform)
Muda si mrefu sana hayo majani yatakuwa hivi (Unjano katika vena za majani)

View attachment 418426
Huo ni ugonjwa huitwa Papaya Ringspot diseases/Papaya Ringspot Virus

Huenezwa na wadudu waitwao Aphids/Wadudu mafuta
Mche wa namna hiyo hata ukizaa matunda yake huwa na mabaka baka/mashiringi
View attachment 418428View attachment 418436

KABLA HATUJAKUSAHURI CHA KUFANYA, TUNAOMBA KUFAHAMU YAFUATAYO

1. Maganement/Matunzo ambazo tayari umeshayafanya shambani, yaani tangu kuandaa mashimo mpaka sasa umefanya nini na nini, ie. Ulipandia mbolea gani??, umeshaweka mbolea zipi tena mpaka sasa, JE UKIACHA CONFIDOR kuna viuatilifu gani umeshapiga hapo shambani?/
KWAKWELI NIMETAFUTA SANA MASOMO YA KILIMO CHA PAPAI SIJAPATA KWAHIO NLIKUA NAFANYA TU MAJARIBIO. NLIPANDIA SAMADI YA NG'OMBE TOKA HAPO NAPIGA TU MAJI MARA MBILI KWA WIKI. SINA BOOSTER WALA DAWA ZOZOTE NAZOTUMIA ZAIDI YA CONFIDOR NLIPIGA BAADA YA KUONA APHIDS.

2. Je umewahi kupiga booster zozote?? HAPANA

3. Hizo dawa za wadudu unapiga kila baada ya muda gani?? SIPIGI ZAIDI YA CONFIDOR NLIPIGA MARA MBILI

4.Napsack Sprayer (Bomba) unalotumia kupulizia dawa ni lako?/ au unaazima kwa jirani (Eleza ukweli) LA KWANGU

5.Uwekaji wako wa maji ukoje, unaweka mara ngapi maji kwa wiki, na ni wastani wa lita ngapi kwa mche kwa siku/wiki?? etc
KILA SHINA NDOO MOJA YA LITA 10 MARA MBILI KWA WIKI
KARIBU

===================================
 
Bonge
SALAMU KIONGOZI
KARIBU
Ni kweli jamii za Marigold (African marigold (Tagetes erecta Linn.) and French marigold (Tagetes patula Linn). Zinatumika kama fly repellent/kufukuza wadudu hasa Aphids na Thrips, pamoja na fruit flies.

Lakini pia mahali yanapoota Marigold wale Minyoo fundo (Nematodes, wasababishao kuoza kwa mizizi, Root knot Nematodes) hupungua sana. Marigold yanamatumizi mengi sana , baadhi ya nchi kuna namna wanayatumia kuongeza virutubisho kwa chakula cha mifugo na kukiknga mifugo dhidi ya minyoo.

Hakuna uthibitisho wa kisayansi wa 100% kuwa ukitumia Marigold basi uache kutumia dawa za viwandani, Kuna baadhi ya wadudu kama Tuta absoluta (Kanitangaze wa nyanya, au Bakteria i,e Bacteria Wilt, au Fungus (Kuvu/Fangasi)) bado hakuna uthibitisho wa kutosha kuwa wanaweza zuiwa kwa kutumia Marigold.

Lakini ni vyema ukayapanda, yatakupunguzia kiasi fulani gharama za madawa. Hushauriwa kutumika katika kilimo cha Organic (Kilimo hai), maana sumu yake huisha nguvu ndani ya siku 7.

kuna kajistory hapa, unaweza kapitia kutoka kwa mkulima Kenya hapo

Marigold is all I use to stop pests and diseases


kilimomaarifa.tajiri ni kweli African marigold ikipandwa kuzunguka shamba/bustani inasaidia kupambana na wadudu na unaweza acha kutumia dawa za wadudu za viwandani?
 
ASHA NGEDELE
SALAMU SANA
ASANTE KWA MAJIBU YAKO
KUNA VITU TUNAKUSHAURI

1. Kuhusu hiyo mbegu yako ya tikiti, ipe muda angalau siku 5 mbele tuone. Zisipooota itabidi urudie kupanda, LAKINI hatuisemi vibaya ila kuna takribani wakulima 15 pia wameilalamikia inaota taratibu, na haiko haraka katika ukuaji. Sijui tatizo liko wapi, au labda watu wameanza kuichakachukua hatujui. Ni vyema hizo mbegu mpya ukaziongezea nguvu kwa kuzitibu zaidi (siku 2 kabla ya kupanda) na moja wapo ya dawa kama Cluiser, Mortano, Seed care, Seed plus, Seed treat, Broad hactare etc, kwa sababu mbegu nyingi hata hiyo uliyotumia naamini iko na Thiram tu ambayo ni non-systemic dimethyl dithiocarbamate fungicide, haina nguvu sana dhidi ya baadhi ya bacteria, na magonjwa mengine (Inafanya kazi vizuri kama Contact fungicides), hivyo bado mbegu inaweza kushambuliwa kabla ya kuota.

2. Tukirudi katika Miche yako ya papai
i. Iongezee lishe, tafuta NPK (17:17:17) ambayo itasaidia kuboost ukuaji, mizizi na kuimarisha afya ya majani
2. Ni muhimu ukatumia tena cofidor ndani yake mix na dawa ya ukungu kama Multi Power 78wp au Azoxtrobin, au Agrifos400, au Ebony 72, ndani yake weka booster kama Supergrow, au Multi K,au Murphy foliar fertilizer au Omex. Lengo ni kusaidia kama kutakuwa na baridi usiku/unyevu mwingi basi mmea usiathirike (Fungus), na pia kuna dalili ya upungufu wa micro elements kama Boron, na Magnesium, hizo utazipata kwa kupitia booster.

ii. Kabla ya kuweka mbolea ile NPK mwagia kwanza maji, kisha weka NPK, kila mche unapaswa kupata gram 300, unaweka pembeni ya shina huku yalipo ya majani (Plant Canopy), huko ndipo root hair ziliko fika, tumia rato kutengeneza sahani kisha weka hizo gram 300 (sawa na maganda 6 ya viberiti, kule kunako kaa njiti,) ukiweka mbolea hiyo unafukia na udongo au kuweka matandazwa,

ii. Kwa upande wa maji si mbaya sana kiwango unachoweka, kwa kuwa bado haijaanza kuzaa angalau lita 25 kwa mche inatosha, ila ikianza kuzaa walau kila mche upate lita 50 za maji kwa wiki 1.

KILA LAKHERI


KABLA HATUJAKUSAHURI CHA KUFANYA, TUNAOMBA KUFAHAMU YAFUATAYO

1. Maganement/Matunzo ambazo tayari umeshayafanya shambani, yaani tangu kuandaa mashimo mpaka sasa umefanya nini na nini, ie. Ulipandia mbolea gani??, umeshaweka mbolea zipi tena mpaka sasa, JE UKIACHA CONFIDOR kuna viuatilifu gani umeshapiga hapo shambani?/
KWAKWELI NIMETAFUTA SANA MASOMO YA KILIMO CHA PAPAI SIJAPATA KWAHIO NLIKUA NAFANYA TU MAJARIBIO. NLIPANDIA SAMADI YA NG'OMBE TOKA HAPO NAPIGA TU MAJI MARA MBILI KWA WIKI. SINA BOOSTER WALA DAWA ZOZOTE NAZOTUMIA ZAIDI YA CONFIDOR NLIPIGA BAADA YA KUONA APHIDS.

2. Je umewahi kupiga booster zozote?? HAPANA

3. Hizo dawa za wadudu unapiga kila baada ya muda gani?? SIPIGI ZAIDI YA CONFIDOR NLIPIGA MARA MBILI

4.Napsack Sprayer (Bomba) unalotumia kupulizia dawa ni lako?/ au unaazima kwa jirani (Eleza ukweli) LA KWANGU

5.Uwekaji wako wa maji ukoje, unaweka mara ngapi maji kwa wiki, na ni wastani wa lita ngapi kwa mche kwa siku/wiki?? etc
KILA SHINA NDOO MOJA YA LITA 10 MARA MBILI KWA WIKI
KARIBU
 
ASHA NGEDELE
SALAMU SANA
ASANTE KWA MAJIBU YAKO
KUNA VITU TUNAKUSHAURI

1. Kuhusu hiyo mbegu yako ya tikiti, ipe muda angalau siku 5 mbele tuone. Zisipooota itabidi urudie kupanda, LAKINI hatuisemi vibaya ila kuna takribani wakulima 15 pia wameilalamikia inaota taratibu, na haiko haraka katika ukuaji. Sijui tatizo liko wapi, au labda watu wameanza kuichakachukua hatujui. Ni vyema hizo mbegu mpya ukaziongezea nguvu kwa kuzitibu zaidi (siku 2 kabla ya kupanda) na moja wapo ya dawa kama Cluiser, Mortano, Seed care, Seed plus, Seed treat, Broad hactare etc, kwa sababu mbegu nyingi hata hiyo uliyotumia naamini iko na Thiram tu ambayo ni non-systemic dimethyl dithiocarbamate fungicide, haina nguvu sana dhidi ya baadhi ya bacteria, na magonjwa mengine (Inafanya kazi vizuri kama Contact fungicides), hivyo bado mbegu inaweza kushambuliwa kabla ya kuota.

2. Tukirudi katika Miche yako ya papai
i. Iongezee lishe, tafuta NPK (17:17:17) ambayo itasaidia kuboost ukuaji, mizizi na kuimarisha afya ya majani
2. Ni muhimu ukatumia tena cofidor ndani yake mix na dawa ya ukungu kama Multi Power 78wp au Azoxtrobin, au Agrifos400, au Ebony 72, ndani yake weka booster kama Supergrow, au Multi K,au Murphy foliar fertilizer au Omex. Lengo ni kusaidia kama kutakuwa na baridi usiku/unyevu mwingi basi mmea usiathirike (Fungus), na pia kuna dalili ya upungufu wa micro elements kama Boron, na Magnesium, hizo utazipata kwa kupitia booster.

ii. Kabla ya kuweka mbolea ile NPK mwagia kwanza maji, kisha weka NPK, kila mche unapaswa kupata gram 300, unaweka pembeni ya shina huku yalipo ya majani (Plant Canopy), huko ndipo root hair ziliko fika, tumia rato kutengeneza sahani kisha weka hizo gram 300 (sawa na maganda 6 ya viberiti, kule kunako kaa njiti,) ukiweka mbolea hiyo unafukia na udongo au kuweka matandazwa,

ii. Kwa upande wa maji si mbaya sana kiwango unachoweka, kwa kuwa bado haijaanza kuzaa angalau lita 25 kwa mche inatosha, ila ikianza kuzaa walau kila mche upate lita 50 za maji kwa wiki 1.

KILA LAKHERI


KABLA HATUJAKUSAHURI CHA KUFANYA, TUNAOMBA KUFAHAMU YAFUATAYO

1. Maganement/Matunzo ambazo tayari umeshayafanya shambani, yaani tangu kuandaa mashimo mpaka sasa umefanya nini na nini, ie. Ulipandia mbolea gani??, umeshaweka mbolea zipi tena mpaka sasa, JE UKIACHA CONFIDOR kuna viuatilifu gani umeshapiga hapo shambani?/
KWAKWELI NIMETAFUTA SANA MASOMO YA KILIMO CHA PAPAI SIJAPATA KWAHIO NLIKUA NAFANYA TU MAJARIBIO. NLIPANDIA SAMADI YA NG'OMBE TOKA HAPO NAPIGA TU MAJI MARA MBILI KWA WIKI. SINA BOOSTER WALA DAWA ZOZOTE NAZOTUMIA ZAIDI YA CONFIDOR NLIPIGA BAADA YA KUONA APHIDS.

2. Je umewahi kupiga booster zozote?? HAPANA

3. Hizo dawa za wadudu unapiga kila baada ya muda gani?? SIPIGI ZAIDI YA CONFIDOR NLIPIGA MARA MBILI

4.Napsack Sprayer (Bomba) unalotumia kupulizia dawa ni lako?/ au unaazima kwa jirani (Eleza ukweli) LA KWANGU

5.Uwekaji wako wa maji ukoje, unaweka mara ngapi maji kwa wiki, na ni wastani wa lita ngapi kwa mche kwa siku/wiki?? etc
KILA SHINA NDOO MOJA YA LITA 10 MARA MBILI KWA WIKI
KARIBU
ASANTE SANA MKUU. MUNGU ATAKUJAALIA KWA ELIMU HII YA BURE UNAYOTOA KWA WAKULIMA WACHANGA KAMA SIE
 
Bonge
SALAMU KIONGOZI
KARIBU
Ni kweli jamii za Marigold (African marigold (Tagetes erecta Linn.) and French marigold (Tagetes patula Linn). Zinatumika kama fly repellent/kufukuza wadudu hasa Aphids na Thrips, pamoja na fruit flies.

Lakini pia mahali yanapoota Marigold wale Minyoo fundo (Nematodes, wasababishao kuoza kwa mizizi, Root knot Nematodes) hupungua sana. Marigold yanamatumizi mengi sana , baadhi ya nchi kuna namna wanayatumia kuongeza virutubisho kwa chakula cha mifugo na kukiknga mifugo dhidi ya minyoo.

Hakuna uthibitisho wa kisayansi wa 100% kuwa ukitumia Marigold basi uache kutumia dawa za viwandani, Kuna baadhi ya wadudu kama Tuta absoluta (Kanitangaze wa nyanya, au Bakteria i,e Bacteria Wilt, au Fungus (Kuvu/Fangasi)) bado hakuna uthibitisho wa kutosha kuwa wanaweza zuiwa kwa kutumia Marigold.

Lakini ni vyema ukayapanda, yatakupunguzia kiasi fulani gharama za madawa. Hushauriwa kutumika katika kilimo cha Organic (Kilimo hai), maana sumu yake huisha nguvu ndani ya siku 7.

kuna kajistory hapa, unaweza kapitia kutoka kwa mkulima Kenya hapo

Marigold is all I use to stop pests and diseases
Asante kwa majibu...hii issue ya marigold ni maelezo ya jamaa wa JKT kwenye banda lao wakati wa nanenane...kwenye shamba darasa lao walisema wametumia african marigold tuu bila dawa yeyote hasa katika kilimo cha kabichi.
 
Shukrani kwa Mrejesho mkuu

Karibu


Asante kwa majibu...hii issue ya marigold ni maelezo ya jamaa wa JKT kwenye banda lao wakati wa nanenane...kwenye shamba darasa lao walisema wametumia african marigold tuu bila dawa yeyote hasa katika kilimo cha kabichi.
 
NEWS, NEWS, (MPYA).....16/10/2016
Wataalamu wa kilimomaarifa.tajiri, wanayo furaha kubwa kuwa fahamaisha kuwa PDF (s)/Soft copy ya zao la Bamia (Okra/Ladie Finger,/Abelmoschus esculentus) Imekamilika. Inauzwa kwa Tsh 30,000. Ina kurasa 19 (Malipo ni kupitia Mpesa 0744302645/Tigo pesa 0717041222)
YALIYOMO.
1.Hali ya hewa ya kustawisha bamia (Joto, mvua, udongo, PH)
2.Aina za mbegu (OPV, Hybrid)
3.Kiasi cha mbegu utakachohitaji kwa eka 1, nafasi ya kupanda, na mbolea za kutumia pamoja na vipimo
4.Madawa utakayohitaji (Ya wadudu, ukungu, booster,dawa za kutibu mbegu etc)
5.Jumla ya gharama utakazo ingia tangu kukodi shamba, mbegu, vibarua, mafuta ya pump, mbolea, madawa (ya wadudu/Ukungu), mbolea mpaka kuvuna
6.Maelezo ya msimu mzuri wa kulima, na mchanganuo wa gharama na faida/hasara
7.Wadudu na magonjwa (Kwa njia ya picha), dalili za magonjwa, na namna ya kuyadhibiti

KARIBUNI SANA
bamia Cover Page
upload_2016-10-16_13-1-51-png.419060
 
MUHIMU

1. Kabla ya kusia mbegu zako katika kitalu, ni vyema ukatibu udongo wa kitaluni, eiza kwa kuuchoma kwanza, au kutumia mchanganyiko wa dawa za wadudu na ukungu, ili kuua mazalia ya Minyoo Fundo (Nematodes), bakteria na kuvu/Ukungu

ii. Ni muhimu pia kuziongezea mbegu kinga kabla ya kuzipanda, ni vyema ukazichanganya na dawa kama vile seed care, seed treat au Apron star, au Marshall, kabla ya kuzipanda

iii.Kabla hujahamisha miche shambani, ni vyema kutibu udongo wa shambani, kwa kuspary katika mashimo utakapopanda miche dawa zenye mchanganyiko wa dawa za ukungu na wadudu, ili kuepuka uwezekano wa miche kushambuliwa mapema na wadudu au ukungu
 
BAADHI YA AINA ZA MAGONJWA YA MAZAO MBALI MBALI

1. Ubwiri Unga/Powdery Mildew
upload_2016-10-19_23-25-0.png
upload_2016-10-19_23-28-4.png

Chanzo kikubwa ni fangasi
Ugonjwa huenea zaidi wakati wa unyevu mwingi, majani/matunda huwa na vidoa doa vyeupe
TIBA. Tumia dawa zenye Metalaxyl au Azoxtrobin au Myoxin au Hexaconazole kutibu ugonjwa huu
Baadhi ya dawa hizo ni Ebony 72 WP, Amista Xtra, au Power 78WP, au Xantho
===========
2.Bacteria Angular Leaf spot (Madoa ya bakteria kwa majani)
upload_2016-10-19_23-30-13.png

Husababishwa na Bacteria (Pseudomonas Spp)
Bacteria Husababisha madoa doa ya rangi ya brown kwa majani,majani huchakaa, na kisha majani hufa na kisha mmea wote hufa pia
Hutokea zaidi wakati wa unyevu mwingi na katika udongo kichanga
Tiba tumia dawa za ukungu zenye Copper kuzuia mashambulizi zaidi
Dawa kama vile, Bluu Copper/Tan copper/Nordox/ Funguran etc
=================
3.Bacteria Fruit Blotch
upload_2016-10-19_23-36-40.png

upload_2016-10-19_23-38-16.png

Husababishwa na Bacteria
=Ugonjwa huenea zaidi wakati wa unyevu mwingi
Matunda hutobolewa, huwa na madoa doa na kuoza kwa ndani
Mashambulizi yakizidi hata matunda hupata nyufa (Fruit Cracking)

upload_2016-10-19_23-43-8.png

Tumia dawa zenye Calbendazim na copper mapema baada ya kupanda miche, kumbuka kutibu mbegu na udongo kabla ya kupanda mazao
=====================
4.Bacteria Wilt
upload_2016-10-19_23-45-45.png

upload_2016-10-19_23-46-59.png
upload_2016-10-19_23-47-43.png

Ugonjwa husababishwa na Bacteria
Huenezwa na Kobe wa Matunda (Erwinia Tracheiphila) wa mazao ya Tikiti/Tango/Maboga
Mmea huaanza kwa kushambuliwa majani machache, mmea husimama kukua, kisha majani yote huanza kunyauka, mmea hufa
Tumia dawa za kutibu mbegu (Seed plus, seed plus, Seed care etc), na udongo (Fungicides +Insecticides) mapema kabla ya kusia/kupanda mbegu/Miche
=================

Itaendelea.............
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom