Je, unapenda kufahamu sheria za kazi na maswala yanayo husiana na kazi?

omkude

New Member
Apr 11, 2012
2
5
Kuna NGO inatoa taarifa mbalimbali za maswala yanayo husiana na kazi hususani haki za mfanya kazi na mwajiri. Hii NGO inashirikiana na Association of Tanzania Employers (ATE) pamoja na Chama cha wafanyakazi (TUCTA). Zipo taarifa nyingi kama haki za maternity kwa wakina dada, termination of employment, leaves, mediation and arbitration, na nyingine nyingi. Pia wanatoa taarifa na maelekezo ya ushauri kuhusu career na wanafanya tafiti za viwango vya mishahara kwa watu wa elimu, kazi, ujuzi, uzoefu, jinsia mbalimbali nchini kote. Utafiti huu unafanyika online na questionnaire yao ipo katika tovuti yao, baada ya kupata washiriki wapatao 1000 wa survey hiyo watatoa matokeo katika mtandao huo, hivyo kama wewe ni mchumi wa degree ya kwanza na uzoefu wa miaka 3 utaweza kujua kwa wastani Tanzania watu wenye sifa kama zako wanalipwa kiasi gani, hivyo utaweza kufanya ulinganishi na pengine kufanya maamuzi ya kuomba nyongeza n.k
Nimeona ni tovyti nzuri kuwashirikisha wadau kwani tulio wengi tunapata mkate wetu wa kila siku kutokana na kazi tufanyazo kwa ujira, yaani tumeajiriwa. Hivyo taarifa za kwenye tovuti hii zitatupasha habari nzuri. Inapatikana kwa link hii hapa: Mywage.org/Tanzania - All about Income and Work in Tanzania, Minimum Wage Tanzania
au : AfricaPay.org/Tanzania - All about Pay, Income and Work in Tanzania, Minimum Wage Tanzania

Tuitembelee na kujifahamisha maswala kede kede. Naomba kuwakilisha wana jamii.
 
Back
Top Bottom