Je, unakumbuka ulivyokuwa ukifikiria ulipokuwa mtoto?

Nakumbuka nilipokuwa mtoto kila nilipokwenda stesheni (Tbr) nilikuta injini za tren zipo on muda wote, pia mabehewa yakisukumwa kwenda mbele na nyuma. Hapo nilidhani kwamba injini ya treni ikizimwa basi haiwaki tena, na mabehewa yakikaa muda mrefu bila kupelekwa mbele na kurudishwa nyuma (shanting) hupata kutu na kusababisha injini kushindwa kuyavuta. Je wewe unakumbuka nini ulipokuwa mtoto?

Zamani enzi za RTD kabla ya taarifa ya habari zilipigwa ngoma za Mzee Moris Nyunyusa basi mie nilidhani kuwa Mzee yule yuko ndani ya redio yetu aina ya Memory Q. Siku moja nilisafiri na wazazi wangu kwenda Lindi, siku moja tukiwa na mwenyeji wetu kabla ya taarifa ya habari, nilisikia zile ngoma. Nilishangaa sana kuwa Moris Nyunyusa amefikaje kule Lindi tena kwenye redio nyingine isiyo ya kwetu!
 
mwlimu wa sayansi alifundisha matumizi ya darubini.
akasema moja ya hayo ni kuangalia kitu kilichombali,
kukivuta na kukiona kwa ukaribu kama vile kiko karibu zaidi.
Mimi nikadhani ni umbali wowote. kaka yangu flani akatoka nairobi,
akawa anapiga story kua darubini yake imeharibika. me nikajua bro hua anatuangalia
tokea nairobi hadi hom (moshi).


Mkuu umenichekesha..ila umenikumbusha miaka ya karibuni tu kuna mtu alikuwa Dsm aliwasha bluetooth kwenye cm yake akampigia cm rafiki yake alikuwa Mbeya kwamba amrushie wimbo
 
mi nlidhani mlio wa honi za gari unatoka kwenye taa"headlight" za gari,afu ili gari iende spid unanyonga zaidi usukani
 
Jamani sina mbavu hapa. Mimi nakumbuka nikiwa Class One nilikuwa nafikiri mwalimu wangu wa kike hana kovu lolote sehemu ya mwili kwahiyo kila siku namchunguza akifundisha nikaona ni msafi na hivyo nika conclude that walimu hawana scars.
 
nilikuwa nadhani majambazi ni jamii ya watu,nikawa natamani siku moja wavamie kwetu afu mi nikamate kitoto chao ndo nipambane nacho
 
Mimi nilikua najua kwamba ukipiga picha mbele ya ukuta, picha yako inatokea ukutani wakati huohuo.
 
Mimi nilikua najua kwamba mtu anayeendesha gari kubwa ana nguvu sana kuliko anayeendesha gari ndogo
 
nikiwa darasa la tano[watoto wa siku hizi tofauti kabisa dah] nakumbuka nilifuatwa shule niende nyumbani kumsalimia broo ambae alikuwa anatoka uk baaada ya kukaa miaka minne; ilikuwa patashika kwani kwanza nilijua jamaa keshageuka kuwa mzungu halafu hajui tena kiswahili wala lugha ya nyumbani!!ukizingatia nilikuwa sijui zaidi ya zis,zat ,no na yes! Nilipata wakati mgumu mno kurudi home siku hiyo..:......
 
Mkuu usihangaike reference ya mbali sana, im a case study. Nimenunua simu ya memory card mwaka juzi nikampigia simu rafiki yangu aliyeko Tanga anitumie wimbo wa machozi kwa bluetooth mie nipo Ludewa.
Mkuu umenichekesha..ila umenikumbusha miaka ya karibuni tu kuna mtu alikuwa Dsm aliwasha bluetooth kwenye cm yake akampigia cm rafiki yake alikuwa Mbeya kwamba amrushie wimbo
 
Mkuu usihangaike reference ya mbali sana, im a case study. Nimenunua simu ya memory card mwaka juzi nikampigia simu rafiki yangu aliyeko Tanga anitumie wimbo wa machozi kwa bluetooth mie nipo Ludewa. Nikikumbuka nashindwa kujishangaa!!!
Mkuu umenichekesha..ila umenikumbusha miaka ya karibuni tu kuna mtu alikuwa Dsm aliwasha bluetooth kwenye cm yake akampigia cm rafiki yake alikuwa Mbeya kwamba amrushie wimbo
 
kumi hili nilisahau kulinukuu mwanzo mm wakati niko totoo nilikuwa najua ukipaka pafyumu na ukibana makwapa harufu haisikiki kwa wengine ila ukiachia mikono au ukokaa kawaida ndo harufu inaruka kwa wengine basi bana,
sikui ya siku nakumbuka ilikuwa usiku nishaoga nimevaa night dress mama akanituma rum kwake nikalete kalamu na gazeti coz mum alikuwa anapenda kujaza puzzle games kwene magazeti sasa kwa ufinyu wangu wa akili nikaona pafyum kwene dressing table wajua ilikuwa pafyum gani bana ilikuwa yolanda kopo la bati la rangi ya pinki we acha nikapuliza makwapa yote halafu nikabana makwapa kwanguvu nikapeleka gazeti na kalamu kwa mama huku mikono imebana kwapani kwanguvu ili asisikie harufu nikashangaa akaniambia nani kakwambia upake pafyum yangu weee nilitahayari nikaomba msamaha haraka kabla cjashushiwa kofi coz mum alikuwa mkali balaa lol nikaondoka ila nikajiuliza alijuaje wakati nilibana makwapa sana jibu ckupata now najiona very fun

Mkuu, umenikumbusha Yolanda! Akina Lulu hawajui hii kitu.
 
Mie utotoni nilikuwa nadhania samaki hulimwa kama mazao(nafaka) basi kila nikimaliza kula nilikuwa nakusanya mifupa nakwenda kuotesha shambani cha ajabu ilikuwa haichepui ndipo bibi akaja kunitoa tongotongo!
 
Mimi nilikua najua kwamba ukipiga picha mbele ya ukuta, picha yako inatokea ukutani wakati huohuo.
Khaaa !? Aiseeh ! Mie huwezi amini, niliishusha saa kubwa ya ukutani ile ya kizamani, nikaifumua yote nijue kulikoni. Aaaah ! Kimbembe ikawa kurudishia kama ilivyokuwa, aaaah........................wapi ! Nikaikusanya nikaitupia juu ya dari ! Nyumbani iliaminika imeibiwa !
 
kila mmoja wenu alijuwa kuwa watoto wananunuliwa.
Na kama hukupatwa hapo basi mlikuwa mnajuwa kuwa watoto wanazaliwa kutokea kwenye matumbo ya mama zao ambayo yanakuwa yanachanwa.
Kuna mtoto alimuona mama yake mdogo ni mjamzito, kisha akaenda kujifungua. Aliporudi na mtoto, ndipo yule mtoto akadai ufafanuzi watoto wanapatikanaje !? Akajibiwa kuwa wananunuliwa Hospitali. Mtoto akaendelea kuliza: Je inakuwaje kwa Ng'ombe ? Hupata wapi pesa !? Kisha akasema Yeye ameshuhudia Ng'ombe wa Babu alipompitishia mtoto wake ! Watu wazima wakatoa mimacho kodo kwa uongo wao !
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom