hilbajojo2009
Member
- May 25, 2009
- 46
- 1
Siku za karibuni tumeshuhudia matokeo mabovu katika ngazi mbalimbali za elimu, kidato cha nne, sita na kidato cha pili. Pia matokeo ya mtihani wa darasa la saba hayaridhishi. Pia tumeshuhudia vijana wengi wanaohitimu elimu katika ngazi mbalimbali wakikosa ajira. Wahitimu pia wameshindwa kujiajiri. Wasomi waliobahataika kupata ajira katika sekta binafsi au serikali hawajasidia kiasi cha kutosha katika kuleta maendeleo kwa taifa letu.
wasomi wameshindwa kuleta ugunduzi wa kweli, badala yake wameishia kupata shahada mbalimbali ambazo ugunduzi wake ni wa makaratasi tu.
Je hali hii inasababishwa na uhaba wa walimu nchini? au mfumo mbovu wa elimu. Unafikiri elimu yetu inaweza kuwa bora bila kuwa na walimu bora?
wasomi wameshindwa kuleta ugunduzi wa kweli, badala yake wameishia kupata shahada mbalimbali ambazo ugunduzi wake ni wa makaratasi tu.
Je hali hii inasababishwa na uhaba wa walimu nchini? au mfumo mbovu wa elimu. Unafikiri elimu yetu inaweza kuwa bora bila kuwa na walimu bora?