Nahory Mwendi
New Member
- Mar 11, 2012
- 1
- 0
Nimekuwa nikiangalia mwenendo mzima wa siasa za hapa nyumbani, na kulinganisha na siasa za nje, kusema ukweli siasa za hapa nyumbani zinalenga masilahi binafsi na wala si masilahi ya Taifa. Inauma sana unapoona kiongozi mliemchagua huku mkiwa na imani kubwa kuwa atawaondolea kero mlizonazo, mwisho wa siku akipata uongozi hata kurudi kuja kuwashukuru kwa kumuweka madarakani anashindwa. Je hii ni haki kweli? Ni lini wanasiasa watamuokoa mwananchi wa hali ya chini? Nini kifanyike kuinusuru nchi yetu kwani inamegwa kila siku na hao ambao tuliwapa dhamana kutuletea maendeleo?