Sheria ya Tanzania imeweka utaratibu wa kugoma katika Sheria za Kazi za Mwaka 2004.
Sheria za Tanzania pia zimeweka wazi utaratibu wa wafanyakazi wanaotoa huduma muhimu (Essential services) kama madaktari, waongozaji wa ndege wanaotaka kugoma.
Je utaratibu wa madaktari kugoma umefuatwa?
Kwa nini watanzania tumejenga tabia za kutumia siasa na malumbano ili kutatua maswala ambayo ni ya kimikataba wa kazi, kisheria ?
Kila daktari ana mkataba wake binafsi wa kazi. Kila daktari alipoajiriwa alisoma masharti yake ya kazi. Hayo masharti yanasemaje?
Ajabu moja hapa Tanzania tunashabikia migomo bila kuuliza maswali ya msingi:
Wanasheria wa Serikali wanaosimamia sekta ya afya mnawajibu wa kwenda mahakamani kupata kuulizia uhalali wa mgomo husika na kama hauna uhalali hatua za kisheria zichukuliwe.
Katiba mpya haitakuwa na maana yoyote endapo Sheria zilizotungwa na Bunge au kwa idhini ya Bunge hazitumiki kutuongoza.
Sheria za Tanzania pia zimeweka wazi utaratibu wa wafanyakazi wanaotoa huduma muhimu (Essential services) kama madaktari, waongozaji wa ndege wanaotaka kugoma.
Je utaratibu wa madaktari kugoma umefuatwa?
Kwa nini watanzania tumejenga tabia za kutumia siasa na malumbano ili kutatua maswala ambayo ni ya kimikataba wa kazi, kisheria ?
Kila daktari ana mkataba wake binafsi wa kazi. Kila daktari alipoajiriwa alisoma masharti yake ya kazi. Hayo masharti yanasemaje?
Ajabu moja hapa Tanzania tunashabikia migomo bila kuuliza maswali ya msingi:
- Je sheria na taratibu zimefuatwa?
- Je kila daktari anayegoma amesoma barua yake ya ajira na masharti yake ya kazi aliyoyakubali? Je wanaoshabikia migomo ya madaktari wamesoma masharti yao ya kazi?
- Je? Chama Cha Madaktari (MAT) ni chama cha wafanyakazi kinachoweza kutangaza mgogoro wa kazi na kuwahamasisha wanachama wake wasiende kazini?
Wanasheria wa Serikali wanaosimamia sekta ya afya mnawajibu wa kwenda mahakamani kupata kuulizia uhalali wa mgomo husika na kama hauna uhalali hatua za kisheria zichukuliwe.
Katiba mpya haitakuwa na maana yoyote endapo Sheria zilizotungwa na Bunge au kwa idhini ya Bunge hazitumiki kutuongoza.