Maeneo mengi huku mikoani walikoweka repeater za redio free Africa (RFA) yamekuwa yakikosa matangazo yao kwa ufasaha. Nichukulie mfano Iringa, matangazo ya RFA kwa mwaka 2011 yamepatikana kwa chini ya 50%. Imekuwa iki-scratch sana na kukata kwa muda mrefu na kurudi kwa muda mfupi kabla ya kukata tena, na hakuna marekebisho yoyote yanayofanyika.Ni kero hasa pale unapokuwa na ratiba ya kutaka kusikiliza kipindi fulani. Zamani haikuwa hivi kiasi kwamba imenifanya niamini kuwa wako hoi kifedha. Ninakaribisha maoni.