Mwanamayu
JF-Expert Member
- May 7, 2010
- 11,338
- 6,463
Katiba ya jamhuri ya muungano wa Tanzania imetoa utaratibu wa kutangaza hali ya hatari (state of emergency) kama kuna vita au vurugu ndani ya nchi katika ibara ya 32 (1), (2) na (3). Ni Rais peke yake mwenye mamlaka ya kufanya hivyo, na uamuzi huo mpaka upitiwe na Bunge na kukubaliwa. Sasa kipindi cha uchaguzi hatuna Bunge, je itakuwaje? Au ndio JK amekwisha kabidhi madaraka kwa Lt. Gen. Abdulahaman Shimbo? TPDF wanatakiwa kuwa kimya mpaka watakapo pokea amri na sio kutoa tahadhari kama wao ni jeshi la polisi ambalo liko chini ya waizara ya mambo ya ndani.
Hapa naona kama JK amevunja katiba. Hivi ndio maana JK alitaka li baraza la usalama liwe dude kubwa?
Hapa naona kama JK amevunja katiba. Hivi ndio maana JK alitaka li baraza la usalama liwe dude kubwa?