"Je? Rais ahutubie kila Kikao cha Bunge"

Arusha Mambo

Senior Member
Jan 27, 2011
174
150
Fahamu hili katika Katiba Mpya ya Kenya.

Bunge la Kenya linaendelea chini ya Katiba Mpya ambapo katika kila kikao cha Bunge ni lazima Rais aje ahutubie Bunge na kueleza utekelezaji wa Maadhimio ya Kamati za Bunge na maagizo ya Bunge kwa Serekali , jana Rais Mwai Kibaki wa Kenya alihutubia Bunge hilo ambapo pamoja na mambo mengine alisema Pwani ya Kenya haiwezi kujitenga na kuwa Nchi Huru.

Je tuige hili katika Katiba Mpya ili tupime utendaji wa Rais na Serekali yake katika kutekeleza maelekezo ya Bunge???

Wakazi wa Pwani ya Kenya wanataka kujitenga na kuwa Nchi huru kwa madai kwamba wamekuwa wakichangia kwa kiasi kikubwa uchumi wa Kenya lakini Serekali yao imekuwa haiwaletei maendeleo, jana mtu mmoja aliuwawa katika vurugu zilizotokea mahakamani wakati wa kusomwa kwa kesi ya wafuasi wa kundi linalosimamia madai hayo.

Sikiliza Bunge la Kenya LIVE kuanzia saa 3asubuhi Mpaka Sa6mchana na Sa8mchana mpaka Sa10jioni kupitia www.arushamambo.com click "Sikiliza Arusha Mambo FM...." tutafurahi uki LIKE Redio yetu kwenye TuneIN mara baada ya kufunguka.
 
Back
Top Bottom