Je nimerogwa? Uko uchawi kweli? Naomba usaidizi tafadhali, dada yenu kutoka Ujerumani

henkel

New Member
Oct 17, 2011
4
1
Assallamu Aleikum!

Nimekuwa na bwanangu miaka 13 bila shida na watoto wawili.
Mara si mara, tulihamia mombasa na bwanangu kapata msichana wa kikamba.
Nikapata mimba na huyo msichana kasema nitaona kama utazaa.
Nilizaa mtoto akafariki. Kisha bwana kanifukuza na watoto, na isitoshe nikaambiwa nina maradhi ya moyo, figo mbovu, ini mbovu, sukari na pumu. Hivi napewa madawa mengi sana siptali ujerumani na wala sioni nafuu.
Mimi ni mtu ambaye pia nimeshika dini sana na siamini kuna uchawi, lakini watu wengi wasema kuwa miye nilitupiwa jini na huyo msichana.

Jamani naomba muniambiye kama haya mambo yako kweli na wapi tanzania nitapata mwalimu maarufu mzuri kwa kiislamu ?

Shukran.
 
Assallamu Aleikum!

Nimekuwa na bwanangu miaka 13 bila shida na watoto wawili.
Mara si mara, tulihamia mombasa na bwanangu kapata msichana wa kikamba.
Nikapata mimba na huyo msichana kasema nitaona kama utazaa.
Nilizaa mtoto akafariki. Kisha bwana kanifukuza na watoto, na isitoshe nikaambiwa nina maradhi ya moyo, figo mbovu, ini mbovu, sukari na pumu. Hivi napewa madawa mengi sana siptali ujerumani na wala sioni nafuu.
Mimi ni mtu ambaye pia nimeshika dini sana na siamini kuna uchawi, lakini watu wengi wasema kuwa miye nilitupiwa jini na huyo msichana.

Jamani naomba muniambiye kama haya mambo yako kweli na wapi tanzania nitapata mwalimu maarufu mzuri kwa kiislamu ?

Shukran.

hapana, hujarogwa....wasiwasi wako tu ndio wakufanyisha uone maruweruwe hayo...!
 
Kama upo kwenye dini basi ng'ang'ania huko huko maana shirki ni dhambi kubwa sana,kama upo huku apaa abaa apaaa,yupo mtoto wa sheikh yahya amekabidhiwa mikoba ya baba yake
 
hapana, hujarogwa....wasiwasi wako tu ndio wakufanyisha uone maruweruwe hayo...!
Pole sana mpendwa kwa matatizo ya maisha. We amini umepona tayari nautaona vile mambo yataanza kuongoka. usisemi utapona (future) sema tu nimepona na kila kitu kitarudi sawa kuanzia dakika hili sababu mimi namtegemea Mungu wangu.
 
Bila shaka hujalogwa, ila uchawi upo na ndio maana Maanndiko Matakatifu Biblia yanatahadharisha bayana kwamba WACHAWI hawataurithi uzima wa milele. Lakini mimi mlokole hawezi kuniloga mchawi yeyote, hata akikusanya majini ya dunia nzima!
 
Haukulogwa aisee! ondoa hofu, halaf daktari kasemaje? ,muulize vizuri akueleze, maana isje ikawa jamaa alikuwekea sabuni ya kufulia kwenye ugali! halaf ndo akajiamini kukupa huo mkwala, si unajua bana kuna watu na viatu.
eniwei pole aisee.
 
Waleikum Salam...

Pole saana na matatizo yoote yalokutokea dear... Hamna kitu kina nguvu kama "Iman"... Imani hutufanya tuweze achieve ama kukusa kitu... Hivo basi yawezekana kua ulitilia saana maanani alipokutisha huyo mwanamke wa kikamba mpaka imeku affect psychologically na hata physically saa ingine ukute imechangia hata maradhi ulonayo sasa.... Bahati nzuri saana umesema kua umeshika saana dini, Nakushauri endelea kumshika Mungu na uache kutafuta watu ambao kweli kabisa waweza poteza mda, energy na hata pesa nyingi saana kwao.... Best of Luck katika kutatua matatizo yako....
 
Pole sana mwaya kwa yaliyokufika. Muombe Mungu wako akuondolee yanayokusibu kama kweli unaimani atakusaidia
 
pole sana .. cha msingi jitahidi kuwa na imani yako kama kawaida na uamini hakuna jambo la kurogwa au uchawi kwani inaonyesha unaishi kwa hofu sana
 
lol..........ukitaka kuwafaidi watanzania anzisha topic za ushirikina.....

unaweza jiuliza sasa wale wanao enda kwa waganga ni akina nani?????
 
mtoto kufariki ni kawaida
kuhusu kuumwa umepima hospital? kama ndio ugonjwa wa majini au ushirikana
nijuavo hospitali hawawezi ona kama unaumwa
ila kama waliona basi endelela kutumia daw ahuku ukimtumain Mungu,
sitachelea kusema damu ya YESU NDIO DAWA YAKO hakuna ingine hakuna mponyaji zaidi yake.
mtafute mchungani akuombee si lazima ubadili dini yako ila mwmaini yesu pekee
hao wengine wa kisomo na mashaka kwani watataka hela.
 
Usichanganye din na serikal mamy,hata kwenye maandiko wanasema wachawi wapo,ila serkal ndio haiamn,maombi yanahusika sana na pole kwa yaliyokukuta.
 
Nenda Lagos Nigeria; SCOAN kwa TB Joshua, uwe umerogwa au hujarogwa utapona na haijalishi uwe na imani gani! Google SCOAN au waandikie info@scoan.org ili kufanya booking!
 
Mshike YESU na njoo ufanyiwe maombi hakuna jini linalomshinda yeye ni mwaminifu na ana upendo na uponyaji wa kweli utapona lakini siyo kushika dini maana Dini ni mpango wa mwanadamu kumtafuta Mungu na uzima wa milele lakini dini siyo suluhisho la kila kitu na ndiyo maana hata viongozi wa dini wana mapungufu yake.
 
Pole sana dada,amini kile akiaminicho mtu ndicho humtokea,achana na iman za kichawi hata km zipo,fuatilia matibabu ya hospital na kumwomba mungu wako,na siku moja utapona na kuwa mzima,toa hofu ya kulogwa uliyona nayo na uamin kwa uwezo wa dawa unazotumia hutakufa kabla ya wakati aliokupangia mungu.
 
mpendwa pole kwa kupoteza mtoto na kwa matatizo yanayokupata.
sisi wakristo biblia yetu inatuambia kwamba uchawi upo lkn ni kitu kisichompendeza Mungu.Lkn kama kweli umeshika dini hakuna mchawi wa aina yeyote yule anaweza kukudhuru.Maradhi mengi uliyonayo yanaweza kuwa yanasababishwa na wewe kuwaza sana juu ya matatizo ya kusalitiwa na mumeo.Kuwaza sana juu ya mambo yanayoumiza ni hatari kwa afya ya mwili.Mpendwa ningekushauri kwa ajili ya afya yako punguza mawazo ukiweza acha kabisa kuwaza juu ya hayo matatizo,jaribu kuwaza vitu vinavyofurahisha,isitaki uache wanao wawili wngali wanakuhitaji.Kama kweli wewe ni mtu uliyeshika dini basi nikufananishe na Petro wakati ule alipokua kwenye boti kisha Yesu akamuita kuwa amfuate kwenye maji,Petro mwanzoni alianza kutembea kwenye maji lkn aliposita tu akaanza kuzama, labda mawimbi na kina cha maji kilimtisha.Sasa wewe nawe ni mshika dini mzuri,kwa miaka 13 na tatu Mungu amekuepushia matatizo na watoto wawili kakupa,kumbuka kuna wenzio waliachika hata mwaka haujaisha kwenye ndoa,kuna wengine matatizo yalianzia honeymoney na wengine hadi wamezeeka hata mtoto hawamjui lkn wewe kwa miaka kumi na tatu hujaona hayo ni vyema utambue ni kwa sababu wewe ulikua umeshika dini aka ulimkabidhi Mungu maisha yako ndo maana mambo yakaenda vizuri.Sasa hayo yaliyokupata Mombasa,kupoteza mtoto na maradhi wakristo tunayaita majaribu, ambayo yamekufanya uanze kusita juu ya msimamo wako wakumngangania Mungu,Petro aliogopeshwa na mawimbi akapata hofu akasita akazama,wewe mawimbi yako ni haya yote unayopitia.Mim kwa upendo ninakuomba achana na mambo ya kuulizia mtaalamu sijui mwalimu maana naona umeshaanza kuzama.Hakuna mwalimu ,mganga wala mtaalamu katika dunia hii mwenye nguvu kuliko Mungu.Endelea kushika dini na kumtumainia Mungu.Nakusihi sana ukianza kufanya ushirikina katika maisha yako nuksi,mikosi na mabalaa havitaisha katika maisha.Mungu anakupenda sana,labda ameruhusu ujaribiwe kidogo kama alivyoruhusu Ayubu ajaribiwe lakini ninachojua na kuamini ni kuwa ukiendelea kumtumainia hata uambiwe una maradhi ya aina gani hutakufa maana hata kwa Ayubu Mungu alimruhusu shetani amjaribu Ayubu kwa kila aina ya pigo lakini akamwambie roho yake usiiguse.Hivyo mpendwa wangu usiende kwa washirikina maana Mungu anatosha kuhakikisha kuwa hakuna kitakachotoa uhai wako wala kukudhuru kwa namna yeyote ile.Simama imara ushinde jaribu lako.
 
yesu ndiye jibu la maisha yako muamini yeye amini umekwisha pona mwambie akuumbe kwa upya na akufinyange viungo vyako kwa upya pole mama
 
Back
Top Bottom