je !ni vyema mtu kutafutiwa mke au mume wa kuoa au kuolewa

kilimasera

JF-Expert Member
Dec 2, 2009
3,068
268
Mwenzenu jana nilikuwa na mjadala hapa nyumbani, na mada kuu ilikuwa ni juu ya namna nzuri ya kupata mwenza.

Dada yangu mkubwa ndiye aliyeanzisha huo mjadala kwa kumuuliza mama kama ni vyema mtu kutafutiwa mke au mume wa kuoa au kuolewa, au kila mtu anawajibika kujitafutia mwenyewe mwenza wake na kuanza maisha?

Mama alikuwa na haya ya kusema. Alisema kuwa kimsingi hapo zamani wazazi walikuwa wakiwatafutia watoto wao wenza wa kuoa au kuoelwa na lengo kuu lilikuwa ni kutaka mtoto wao aangukie katika mikono salama na mojawapo ya vigezo vikuu vilivyokuwa vikiangaliwa ilikuwa ni historia ya ukoo husika, kwa mfano, je ukoo huo unaanguka kifafa? Je ni ukoo wa wachapa kazi kwa maana ya kujituma kwa kufanya kzi kwa bidii ( Ikumbukwe kuwa zamani kazi kuu ilikuwa ni kilimo). Je Sio ukoo wenye mkono mrefu, yaani sio wezi ( Sijui kwa nyakati hizi kuna haja pia ya kuwajumuisha na mafisadi yaani kama ukoo una hulka ya ufisadi)

Jambo lingine lilikuwa ni kuangalia kama ukoo unashambauliwa na magonjwa sugu, kama vile anemia (Upungufu wa damu wa mara kwa mara) Kansa, kisukari na maradhi mengine yaliyokuwa yakitafsiriwa kuwa yanaweza kuushambulia ukoo.

Sina hakika kama vigezo hivyo bado vinazingatiwa kwani kule vijijini bado utaratibu a kutafutiana wenza upo lakini sio kwa kiwangom kama cha zamani kwa sababu ya mabadiliko yaliyoikumba jamii, kwani kila mtu sasa na lwake.
 
Back
Top Bottom