Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Sasa mbona hau'suggest neno unalohisi ni sahihi kulitumia...?Nimekuwa nikisikia watu wakitumia neno "kupoteza maisha" kumaanisha mtu amefariki dunia,mimi nafikiri si sahihi kwani inaonekana imetokana na maneno ya kiingereza " lost life". Naomba nisaidiwe.
Sasa mbona hau'suggest neno unalohisi ni sahihi kulitumia...?
Mtu anapokuwa katika kufani, anakuwa na tabia ya kustruggle fulani hata kwa kumtazama physically...hivyo kule ni kupigania maisha..hivyo akifa ni kupoteza!..by my opinion its just ok!
Una habari wazungu wanasemaje mtu akinusurika kufa...?, wanasema "PakaJimmy has cheated death"!...Sasa kwa lugha hiyo ya wenzetu sijui ungesemaje!
Sarufi za lugha hutofautiana, kupoteza maisha huwa na maana ya kutokuwa na ile karama ya uhai, ambayo tunaipata kwa Mungu. Ni neno lenye mahadhi ya kishairi zaidi...
Ushauri wangu tuendelee kutumia neno kufariki dunia kwa kuwa ndio neno sahihi,tuachane na kasumba ya kutafakari kwa kiingereza alafu unasema kwa kiswahili.
Jee amefariki haijitoshelezi - bila kuongeza 'dunia' mbele yake?
neno la msingi ni "kufa" na ni neno muafaka la mzizi kwa tendo husika kwa nayakati na nafsi mbalimbali. maneno mengine yote yakiwemo kupoteza maisha, kumwaga damu, kukata roho, kusalimu roho, kufariki, kufariki dunia nk. ni ya kishairi tu.
Nyamanoro umependekeza tutumie neno kufariki dunia, alakini maana halisi ya "kufariki" ni "kutengana" yaani "separate" kwa kiingereza na limetokana na neno la mzizi la "faraka" na maneno mengine ya jamii hii ni pamoja na farakana, mifarakano farakanisha nk. soma kitabu cha Isaya 59:2 utaona neno "kufarikisha" limetumika.
pmwasyoke, unauliza ikiwa kusema kufariki pekee bila kuongeza "dunia" mbele yake kunakamilisha maana iliyokusudiwa. jibu ni kuwa haikamilishi maana ya kufa. kama nilivyomjibu nyamanoro hapo, kufariki ni kutengana au "to be separated" kwa kiingereza. mtu anaweza kujifarikisha au kufarikishwa na familia, marafiki, dunia, Mungu nk. kwa hiyo kama una maana kuwa huyo fulani katengana na dunia au maisha ni muhimu kuongezea hayo maneno mbele yake ili tujue katengana na nini, vinginevyo utatuacha bila kujua katengana au kafarakana na nini. mfano mtu akitumbukia dhambini huwa amefarakana na Mungu au dhambi zake zimemfarikisha na Mungu wake kwa maana kuwa zimemtenga (zimem-separate) na Mungu wake na si kuwa amekufa. kwa hiyo ni muhimu kusema amefariki dunia au amfariki maisha.
stay blessed.
Glory to God
Maelezo haya YAMEENDA SHULE.
Thanks, Miss J and be blessed!
neno la msingi ni "kufa" na ni neno muafaka la mzizi kwa tendo husika kwa nayakati na nafsi mbalimbali. maneno mengine yote yakiwemo kupoteza maisha, kumwaga damu, kukata roho, kusalimu roho, kufariki, kufariki dunia nk. ni ya kishairi tu.
Nyamanoro umependekeza tutumie neno kufariki dunia, alakini maana halisi ya "kufariki" ni "kutengana" yaani "separate" kwa kiingereza na limetokana na neno la mzizi la "faraka" na maneno mengine ya jamii hii ni pamoja na farakana, mifarakano farakanisha nk. soma kitabu cha Isaya 59:2 utaona neno "kufarikisha" limetumika.
pmwasyoke, unauliza ikiwa kusema kufariki pekee bila kuongeza "dunia" mbele yake kunakamilisha maana iliyokusudiwa. jibu ni kuwa haikamilishi maana ya kufa. kama nilivyomjibu nyamanoro hapo, kufariki ni kutengana au "to be separated" kwa kiingereza. mtu anaweza kujifarikisha au kufarikishwa na familia, marafiki, dunia, Mungu nk. kwa hiyo kama una maana kuwa huyo fulani katengana na dunia au maisha ni muhimu kuongezea hayo maneno mbele yake ili tujue katengana na nini, vinginevyo utatuacha bila kujua katengana au kafarakana na nini. mfano mtu akitumbukia dhambini huwa amefarakana na Mungu au dhambi zake zimemfarikisha na Mungu wake kwa maana kuwa zimemtenga (zimem-separate) na Mungu wake na si kuwa amekufa. kwa hiyo ni muhimu kusema amefariki dunia au amfariki maisha.
stay blessed.
Glory to God
neno la msingi ni "kufa" na ni neno muafaka la mzizi kwa tendo husika kwa nayakati na nafsi mbalimbali. maneno mengine yote yakiwemo kupoteza maisha, kumwaga damu, kukata roho, kusalimu roho, kufariki, kufariki dunia nk. ni ya kishairi tu.
Nimekuwa nikisikia watu wakitumia neno "kupoteza maisha" kumaanisha mtu amefariki dunia,mimi nafikiri si sahihi kwani inaonekana imetokana na maneno ya kiingereza " lost life". Naomba nisaidiwe.
Mimi nilidhani 'kufa' ni kifupisho tu cha neno kufariki (kufariki dunia):embarassed2:!
hapana, siyo kifupisho chake. kufariki ni kutengana au separate kwa kiingereza. rejea maelezo yangu katika post #8 hapo juu
Nimesoma vizuri tu maelezo yako. ....................Mimi naamini .........................