a4afrika
JF-Expert Member
- Apr 13, 2012
- 1,386
- 1,316
- Thread starter
- #41
Mheshimiwa Jingalafalsafa inaelekea hujachukua muda wako mwingi kutafakari kunijibu. Kwa Afrika kuwa moja hiyo ni ndoto isiyoweza kutimia kwa sasa mpaka nchi mojamoja kutengeneza solid foundation katika nchi zao. Wawe womoja, wazalendo na wenye kujitambua kama Taifa moja moja wakifikia hatua hiyo ya kujitambua kwao kama Taifa hapo ndipo watakapo kuwa na uwezo wa kujiunga na kuwa kitu kimoja.
Huwa napenda kusema hivi "TEMESHAZIKWA HAI, SASA TUSIWAACHE WATOTO/VIJUKUU VYETU VIKUTWE NA HAYA YETU, TUWAFANYIE JAMBO"
Kamwe sijawahi kuamini kuwa Afrika inaweza kuungana leo au kesho! HATA SIKU MOJA! Na ikitokea hivyo, basi NITAKULA KIAPO CHA MIAKA 10 KAMA ITADUMU AU NIFE. Lakini...HILO HALITETERESHI UKWELI WA MAMBO KWAMBA, BILA AFRIKAMOJA, WATU WAKE WATAENDELEA KUWA WANYONGE KIZAZI HADI KIZAZI. Yupi ni mzazi bora? Je, si yule ampandiaye mnazi mwanae japo mwenyewe hatokula?
Napenda nijulikane kama Mwanaafrika, napaswa kujivunia Afrika kwanza kabla ya Tanzania! Mzalendo wa Afrika, ni tofauti sana na mzalendo wa Tanzania au Kenya! Mzalendo wa Uganda Amin alipigana vita na Mzalendo wa Tz, Nyerere 1978! Kumbe basi, "KADRI TUNAVYOWAFUNDISHA WATU WETU KUWA WAZALENDO WA VITAIFA VYAO,NDIVYO TUNAVYOUKIMBIA UMOJA NA KUJENGA MIPAKA YENYE UADUI, CHOYO, HILA, VISASI, TAMAA, n.k baina yetu WAAFRIKA, vinavyojengwa na dhana, SISI na WAO, UMIMI-UBINAFSI! Uzalendo wa Kenya au Tanzania Ukikomaa, ndivyo Uadui navyo unavyokomaa, mwishoe ndivyo Afrika inavyomeguka na ndio shuka la unyonge wetu hilo! TUTAFIKA KWELI!?
Uzalendo ni kumfundisha Mtanzania kwanza kuwa yeye ni Muafrika sawa na yule wa Kenya, Uganda, Ghana, Botswana, n.k Chochote afanyacho anatakiwa Atangulize Uafrika wake kwanza! Mkenya akiwa hivyo, Mtz na wengineo, Afrikamoja itajongea! Hilo ni suala la FIKRA, ni rahisi sana kubadili tabia ya mtu lakini sio FIKRA! Kwa kutambua hilo ndio maana nasema, SIO KAZI RAHISI...LAKINI NDIO NJIA PEKEE...NA INAWEZEKANA!
Sasa hivi imekuwa jambo la kawaida kusikia Nchi fulani ya Afrika imesaidia silaha waasi wa nchi nyingne ya Afrika! Wako sahihi, kwani wameapa kuitendea chochote nchi yao ni wazalendo, UAFRIKA UMEWEKWA PEMBENI, UTAZUIA VIPI HAYO?
Mungu wetu anaita sasa!