KIBONGOMKUTI
JF-Expert Member
- Nov 9, 2010
- 1,425
- 605
Wanajamvi me nafagilia mila na desturi za Kibantu ambazo ziko bomba,mathalani hii ya kulipa mahari kwa maana ya kutoa shukrani japo kiduchu kwa wazazi/walezi wa mtarajiwa wako (mke). Lakini baadhi ya watu (ndugu na rafiki) niliongea nao kwa uchache wanadai/kushauri kuwa mahari kwa kawaida huwa hailipwi yote ili kulinda na kutunza heshima kwa wazazi/walezi wa mtarajiwa? Wajameni tujuzane katika hili wenye uelewa katika nyaja hizi?