Je ni kweli yanafanyika kwa wakati huo?

TaiJike

JF-Expert Member
Dec 14, 2011
1,483
666
Natanguliza samahani kama ntakuwa nimewakwaza baadhi ya wasomaji, lengo langu ni kuelimishwa.

Kuna mama mmoja ameolewa na kukuta nyumbani hapo kwa mumewe kuna mtoto alizaliwa na mama yake kuachika. Kinachonishangaza ni mama huyu kila anapomwita binti huyu hutumia neno we mwanaharamu, laanakum, bimatrashamsi, nk. nk. ilimradi tu atumie majina yasiyofurahisha badala ya kutumia jina halisi la binti huyo. Na inapotokea amekosea huambiwa ni kwa kuwa hakupigiwa bismillah (wakati wa utungo wa mimba yake), au hakuadhiniwa kipindi anazaliwa.

Swali: Je ni kweli haya hufanyika wakati wa vitendo hivyo? (kupiga bismillah au kuadhini).
 
Heee... mimi si muumini wa kiislam hivyo sijui kama huwa wanapiga hiyo bismilahi, lakini hata kama ndivyo ilivyo mtoto huyo hatia yake iko wapi? Ni unyanyasaji wa watoto ambao unazungumzwa kila siku.
 
Natanguliza samahani kama ntakuwa nimewakwaza baadhi ya wasomaji, lengo langu ni kuelimishwa.

Kuna mama mmoja ameolewa na kukuta nyumbani hapo kwa mumewe kuna mtoto alizaliwa na mama yake kuachika. Kinachonishangaza ni mama huyu kila anapomwita binti huyu hutumia neno we mwanaharamu, laanakum, bimatrashamsi, nk. nk. ilimradi tu atumie majina yasiyofurahisha badala ya kutumia jina halisi la binti huyo. Na inapotokea amekosea huambiwa ni kwa kuwa hakupigiwa bismillah (wakati wa utungo wa mimba yake), au hakuadhiniwa kipindi anazaliwa.

Swali: Je ni kweli haya hufanyika wakati wa vitendo hivyo? (kupiga bismillah au kuadhini).

Hapo kwenye BOLD Kwa lugha ya kwetu ya kanbila la DONKHA linalopatikana kaskazini mashariki mwa TZ, hayo majini ni sifa anayopewa mtu jasiri, hodari, na anayemudu kuishi katika mazingira yoyote hata yakiwa magumu kiasi gani......LOL

:focus: Huyo mama hayuko sahihi na anachokifanya ni unyanyapaa kwa mtoto, na hiyo itamfanya mtoto asijiamini kabisa.....
Niliwahi kuandika hapa kwamba hakuna mtoto anayeitwa wa haramu wala kuadhiniwa......... Mtoto hawi mtoto eti mpaka sijui aadhiniwe, apigiwe bismilahi, au afanyiwe sijui mambo ya kimila au ya kidini........ huo ni utashi wa kibinadamu, lakini maumbile hayajui mtoto wa haramu wala wa halali.
 
Heee... mimi si muumini wa kiislam hivyo sijui kama huwa wanapiga hiyo bismilahi, lakini hata kama ndivyo ilivyo mtoto huyo hatia yake iko wapi? Ni unyanyasaji wa watoto ambao unazungumzwa kila siku.

Ni kweli huu ni ukiukwaji wa haki ya mtoto, hivyo mama huyo anachofanya ni kumuathiri kisaikologia mtoto huyo.
 
na baba wa mtoto anafurahia tu?

Huyo mwanamke anatabia mbaya tu....
BADILI TABIA Baba wa mtoto hana ajualo kama unavyoelewa wanaume wengi huwa muda wao mwingi huishia kwenye mihangaiko ya kutafuta mkate wa siku, na binti kutokana na hali ya kutishwa kila siku hana ujasiri wa kumweleza baba yake, au pengine ni ile kuhofia kuvunja ndoa ya baba yake hivyo ameamua kuwa kimya.
 
Last edited by a moderator:
Hapo kwenye BOLD Kwa lugha ya kwetu ya kanbila la DONKHA linalopatikana kaskazini mashariki mwa TZ, hayo majini ni sifa anayopewa mtu jasiri, hodari, na anayemudu kuishi katika mazingira yoyote hata yakiwa magumu kiasi gani......LOL

:focus: Huyo mama hayuko sahihi na anachokifanya ni unyanyapaa kwa mtoto, na hiyo itamfanya mtoto asijiamini kabisa.....
Niliwahi kuandika hapa kwamba hakuna mtoto anayeitwa wa haramu wala kuadhiniwa......... Mtoto hawi mtoto eti mpaka sijui aadhiniwe, apigiwe bismilahi, au afanyiwe sijui mambo ya kimila au ya kidini........ huo ni utashi wa kibinadamu, lakini maumbile hayajui mtoto wa haramu wala wa halali.

LOL... we Mtambuzi ni kiboko kwamba ni majini yenye sifa za uhodari, ujasiri nk.nk....
 
Last edited by a moderator:
BADILI TABIA Baba wa mtoto hana ajualo kama unavyoelewa wanaume wengi huwa muda wao mwingi huishia kwenye mihangaiko ya kutafuta mkate wa siku, na binti kutokana na hali ya kutishwa kila siku hana ujasiri wa kumweleza baba yake, au pengine ni ile kuhofia kuvunja ndoa ya baba yake hivyo ameamua kuwa kimya.

angalau majirani wazungumze na huyo baba.....kumwokoa huyo mtoto
 
Last edited by a moderator:
angalau majirani wazungumze na huyo baba.....kumwokoa huyo mtoto
BADILI TABIA hizi nyumba za siku hizi mageti mawili mawili na uzio mkubwa hakuna ajuaye isipokuwa wachache wanaoingia ndani nyumba hiyo ndo wanaoweza sadia, nina mpango wa kuzungumza na baba mdogo wa mtoto huyo ili afikishe taarifa kwa kaka yake.
 
Last edited by a moderator:
TaiJike una mpango wa kuzungumza na baba mdogo wa mtoto huyo labda we ndiye mama mdogo wa mtoto msaidie chalii atakushukuru sana kwani hana mtetezi.
 
Last edited by a moderator:
TaiJike una mpango wa kuzungumza na baba mdogo wa mtoto huyo labda we ndiye mama mdogo wa mtoto msaidie chalii atakushukuru sana kwani hana mtetezi.

Ni wajibu wangu kuwalinda watoto wa tanzania haijalishi ni mama mdogo au mkubwa kinachotakiwa ni haki ya mtoto itendeke kwani mama huyo alimkuta mtoto kabla ye hajaolewa na hata kama angezaliwa baada ya ndoa yake hastahili kutendwa hayo anayotendwa aise.
 
Back
Top Bottom