jouneGwalu
JF-Expert Member
- Apr 11, 2011
- 2,687
- 1,780
Leo, mida fulani hivi nasikiliza wimbo wa Mzee Cosmass Chidumule, "Neema"
Kutoka kwenye huo wimbo napata tafakuri fulani juu ya alichokuwa anakilalamikia mwimbaji, mtoto Neema.
Binafsi nimekuwa na bahati sana ya kukutana na mabinti wenye majina ya Neema, na wengi wao ni wazuri niliokutana nao mimi.
Hapa naomba niwe mkweli, Neema wa kwanza kukutana naye alikuwaga house gal wetu enzi hizo na naanza kupata ile "foolish age", nikataka nijifunzie kwake. Du mtoto alinitosa mbaya kabisa, pamoja na juhudi zote za "walimu" wangu, basi nikajikaza tu na kuendelea kumuita dada japo kwa shingo upande na siku alipoondoka home nilifurahi sana.
Sekondari nilikutana na Neema, mwingine..... nacho kilikuwa kifaa, basi nilikimbizia weee, yalikuwa mapozi juu ya mapozi hadi nikakata tamaa, form III nikahama darasa nikaachana nae, moyoni nilifurahi sana bila kumuona.
Wakati nipo college (diploma), nilikutana na Neema, mwingine... yakawa ni yaleyale ahadi juu ya ahadi, sikutaka kufika nae mbali nikakumbuka hawa watoto wakina Neema sina nao bahati, nikamtema, toka siku ile nikasema sitahangaika na binti yoyote mwenye jina la Neema.
Nilipoingia chuo kikuu, kazi ikaja kwa ndugu yangu sasa..... naye akakutana na Neema wake huko, kijana wangu nae alipata wakati mgumu yule mtoto ni alimpa mapozi hasa hadi tunakuja kumaliza chuo hakuweza kumpata yule mtoto Neema,
Wakati amekata tamaa ya kumpata, ndio siku hiyo akawa ananiambia kuwa hata hivyo alikuwa anajaribu kwa mara ya mwisho tu kwani hajawahi kukutana na wakina Neema na wakamkubalia, naye akanipa mikasa yake na wakina Neema.
Wakati naendelea kusikiliza huu wimbo, ndio najiuliza na naomba wanadau wa MMU mnisaidie hivi haya majina (hata inaweza kuwa jina lolote tofauti na Neema) yana maana kweli kwenye mahusiano?
We kisa chako na haya majina ni nini?
Kuna ishu ya majina ishawahi kujitokeza kwenye mikasa ya mahusiano yako?
Kutoka kwenye huo wimbo napata tafakuri fulani juu ya alichokuwa anakilalamikia mwimbaji, mtoto Neema.
Binafsi nimekuwa na bahati sana ya kukutana na mabinti wenye majina ya Neema, na wengi wao ni wazuri niliokutana nao mimi.
Hapa naomba niwe mkweli, Neema wa kwanza kukutana naye alikuwaga house gal wetu enzi hizo na naanza kupata ile "foolish age", nikataka nijifunzie kwake. Du mtoto alinitosa mbaya kabisa, pamoja na juhudi zote za "walimu" wangu, basi nikajikaza tu na kuendelea kumuita dada japo kwa shingo upande na siku alipoondoka home nilifurahi sana.
Sekondari nilikutana na Neema, mwingine..... nacho kilikuwa kifaa, basi nilikimbizia weee, yalikuwa mapozi juu ya mapozi hadi nikakata tamaa, form III nikahama darasa nikaachana nae, moyoni nilifurahi sana bila kumuona.
Wakati nipo college (diploma), nilikutana na Neema, mwingine... yakawa ni yaleyale ahadi juu ya ahadi, sikutaka kufika nae mbali nikakumbuka hawa watoto wakina Neema sina nao bahati, nikamtema, toka siku ile nikasema sitahangaika na binti yoyote mwenye jina la Neema.
Nilipoingia chuo kikuu, kazi ikaja kwa ndugu yangu sasa..... naye akakutana na Neema wake huko, kijana wangu nae alipata wakati mgumu yule mtoto ni alimpa mapozi hasa hadi tunakuja kumaliza chuo hakuweza kumpata yule mtoto Neema,
Wakati amekata tamaa ya kumpata, ndio siku hiyo akawa ananiambia kuwa hata hivyo alikuwa anajaribu kwa mara ya mwisho tu kwani hajawahi kukutana na wakina Neema na wakamkubalia, naye akanipa mikasa yake na wakina Neema.
Wakati naendelea kusikiliza huu wimbo, ndio najiuliza na naomba wanadau wa MMU mnisaidie hivi haya majina (hata inaweza kuwa jina lolote tofauti na Neema) yana maana kweli kwenye mahusiano?
We kisa chako na haya majina ni nini?
Kuna ishu ya majina ishawahi kujitokeza kwenye mikasa ya mahusiano yako?