Je, ni kweli kizazi hiki wana hatari ya kuwa vipofu na viziwi?

Nzowa Godat

JF-Expert Member
Jun 15, 2011
2,783
819
Kuna shirika moja lisilo la kiserikali, la Rural Future Vision (RFVi), linadai kamba kwa sababu ya kutumia sana earpiece/headphone kusikiliza muziki wa kwenye simu baadhi ya vijana wa leo watapungukiwa na uwezo wa kusikia vizuri watakapofikisha umri wa miaka kuanzia 78 na kuemdelea.

Pia shirika, hilo limetabiri kwamba kwa sababu ya kutumia muda mwingi sana kutazama tv, kusoma kwenye kompyuta (kwa rahaja ya kihehe ni kombyuta), pamoja na kutumia simu kuchat hasa jf na fb, baadhi ya vijana wa leo watapata matatizo ya kutoona vizuri watakapo kuwa na umri wa miaka kuanzia miaka 86 na kuendelea. Kwa hiyo kizazi hiki kinaaswa kuwa na kiasi katika matumizi ya vitu hivyo.
 
Back
Top Bottom