Je ni halali kwa walinzi wa jadi (sungusungu) kuwa watu wenye itikadi?

Josephine

JF-Expert Member
Sep 5, 2010
786
812
Kwa hakika nimeshtuka sana,kuona walinzi wa jadi kuwa ni watu ambao wanajibainisha kama wana CCM.

Wana JF,

Wengi wetu tunapenda mabadiliko ya sera ili kuirudisha Tanganyika yetu katika mfumo ambao ilikuwa ni ndoto ya Mwl. Nyerere na waasisi wa enzi hizo.

Lakini kwa yale niliyosikia toka kwa mwenyekiti,ni kweli Nyenzo wanazo,rasilimali watu wanayo,na hivyo wanajipanga kuendeleza ukoloni mweusi.

napozungumzia rasilimali watu,sizungumzi wananchi kama wananchi,bali ninaongelea Jeshi la polisi,maafisa wa serikali,maafisa usalama,Jeshi la wananchi,walinzi wa jadi na wafanyabihashara wakubwa na wadogo.

Kundi hili la watu limekuwa ni tishio,kwani linatumia nguvu,ubabe,mabavu na pesa katikakutekeleza adhima zao.Niukweli uliodhahiri kwamba kama sisi wananchi ambao tunapenda mabadiliko kwa manufaa ya kizazi chetu,ni lazima tujipange kwa hoja nzito na si kuendekeza ushabiki katika mijadala mingi.kwani mabishano na kiburi havijengi bali hubomoa na kuleta kushindwa.

kwa maana hiyo ni vema tukubali kubadili kufikiri kwetu na kutenda kwetu kwa pamoja kama kundi linalotaka mabadiliko na si kutegemea nguvu ya vyama pekee,Wote tunatambua chama pia kinapata ushindi kupitia sisi wananchi na wakereketwa.

Tuamke ndugu zangu kusambaza propaganda kwa ndugu zetu,marafiki na wote tunaowajua ambao leo bado fikira na mawazo yao yako kifungoni.

Kazi hii tuifanye mimi na wewe ili mabadiliko yatokane na sisi wenyewe.
 
Mkuu mimi wasiwasi wangu ni kuwa CCM huenda ikabadili mbinu baada ya kuona green gurds wamebeba sura ya kigaidi wakawageukia sungusungu kwenye kuadhibu watu wanaowapinga hasa vijijini.
 
Kuna mambo mengi sana bado yanafuata mfumo wa chama kimoja mfano huwezi kupata mafunzo ya mgambo kama hauna kadi ya chama kikongwe
 
Wewe nae hiyo Tanganyika iko wapi? Rais wake nani? au Slaa?

Walinzi wa Jadi, sungu sungu waliokwenda pale wote ni CCM wa chadema hawajaingia pale. Kinachokuchukiza ni nini?
 
Wewe nae hiyo Tanganyika iko wapi? Rais wake nani? au Slaa?

Walinzi wa Jadi, sungu sungu waliokwenda pale wote ni CCM wa chadema hawajaingia pale. Kinachokuchukiza ni nini?

Rafiki FF,am only thinking of the solution,am not ready for argument and abuse in any way.

Nilichosema ni tatizo lililo wazi tunatakiwa kuongelea suluhisho la ukombozi na si Chadema.

Mfumo wa Chama cha mapandizi hauna uhalali ndani ya siasa za leo.ndiyo maana tunahitaji kutafata chakufanya.

Tanzania jina zuri nalipenda,lakini naitambua Tanganyika,iliyofunikwa na mkoloni mweusi.
 
Hivi hawa Sungusungu wanatambulika kisheria?......

Sungusungu wanatambuliwa kisheria kama,Parimentary service.

Ndiyo maana hawapaswi kuwa sehemu au ndani ya Chama flani.

Wasiwasi wangu ni kwanamna wanavyobebwa watatumiwa vibaya sana kufanya vitisho vya hali ya juu katika ngazi za vijiji na jamii kwa ujumla.
 
ni halali kwa sungusungu,wanajeshi,polisi,usalama wa taifa n.k kuwa na itikadi lakini sio halali kwa wao kufanya kazi kwa misingi ya itikadi zao ziwe za dini au siasa.kitendo cha leo kinaleta mashaka kwa sungusungu kwa sababu wanaonyesha itikadi zao waziwazi.
 
ni halali kwa sungusungu,wanajeshi,polisi,usalama wa taifa n.k kuwa na itikadi lakini sio halali kwa wao kufanya kazi kwa misingi ya itikadi zao ziwe za dini au siasa.kitendo cha leo kinaleta mashaka kwa sungusungu kwa sababu wanaonyesha itikadi zao waziwazi.

Asante kwa ufafanuzi mzuri.

Natamani tujadili hilo ulilolifafanua,kwani mwisho wa siku tutapata suluhu.
 
Rafiki FF,am only thinking of the solution,am not ready for argument and abuse in any way.

Nilichosema ni tatizo lililo wazi tunatakiwa kuongelea suluhisho la ukombozi na si Chadema.

Mfumo wa Chama cha mapandizi hauna uhalali ndani ya siasa za leo.ndiyo maana tunahitaji kutafata chakufanya.

Tanzania jina zuri nalipenda,lakini naitambua Tanganyika,iliyofunikwa na mkoloni mweusi.

Tatizo lako nini Sungu sungu au uwepo wa Tanganyika? Tanganyika ilifutwa na Nyerere zamani sana, kama tatizo lako ni hilo.

Na sungu sungu ilianzisha na Nyerere zamani sana kama tatizo lako ni hilo.

Hiyo Tanganyika unayoitambuwa wewe iko wapi? ilikuwepo na kwa sasa ni historia, labda itokee tena kufutwa kwenye historia Tanzania na irudi Tanganyika, lakini kwa sasa haipo hata ukiitambuwa, iko wapi? Rais wake nani? labda Slaa, maana nasikia wengine wanamuita Rais. Sasa kama wewe hulipendi hilo, kazi ni kwako. Kwa sasa tuna Tanzania, jina alilotoa Muhindi wa Tanga, na tuna Dar Es Salaam jina alilotowa Mwaarabu. yatawachaje kuwa mazuri? ulisikia jina la kihindi likawa baya? baniani tu ndio mbaya lakini kiatu chake dawa!
 
Sungusungu wa Mwanza kuanzia sasa hawaaminiki tena. hawafai kulinda kura za uchaguzi (2015) kwa sababu wana magamba.
 
Tatizo lako nini Sungu sungu au uwepo wa Tanganyika? Tanganyika ilifutwa na Nyerere zamani sana, kama tatizo lako ni hilo.

Na sungu sungu ilianzisha na Nyerere zamani sana kama tatizo lako ni hilo.

Hiyo Tanganyika unayoitambuwa wewe iko wapi? ilikuwepo na kwa sasa ni historia, labda itokee tena kufutwa kwenye historia Tanzania na irudi Tanganyika, lakini kwa sasa haipo hata ukiitambuwa, iko wapi? Rais wake nani? labda Slaa, maana nasikia wengine wanamuita Rais. Sasa kama wewe hulipendi hilo, kazi ni kwako. Kwa sasa tuna Tanzania, jina alilotoa Muhindi wa Tanga, na tuna Dar Es Salaam jina lailotwa Mwaarabu. yatawachaje kuwa mazuri? ulisikia jina la kihindi likawa baya? baniani tu ndio mbaya lakini kiatu chake dawa!

Nimekupata kwa kiwango chako,naomba tuendelee kujadili Uhalali wa sungusungu kuendelea kuwa na itikadi ya chama waziwazi,hasa leo tunapokuwa na mfumo wa vyama vingi.
 
Sungusungu wanatambuliwa kisheria kama,Parimentary service.

Ndiyo maana hawapaswi kuwa sehemu au ndani ya Chama flani.

Wasiwasi wangu ni kwanamna wanavyobebwa watatumiwa vibaya sana kufanya vitisho vya hali ya juu katika ngazi za vijiji na jamii kwa ujumla.

Wasiwasi wako ndio maradhi yako. Sungu sungu ndio wapo, na ndio leo umeona gwaride lao, na umeona walivyopendeza, sasa kama una zaidi, si una Mbunge wako hapo unapoishi? kalalamike kule mwambie apeleke hoja Bungeni, kuwa CCM wanatumia askari wa jadi kufanya sherehe zao, na hilo mimi Josephine silipendi kabisa, ili lifutwe.

Lakini leo ndio imetoka hiyo, na wamependeza sana na nguo zao za kijani na njano. Hongera CCM kwa besdei iliyofana.
 
Nimekupata kwa kiwango chako,naomba tuendelee kujadili Uhalali wa sungusungu kuendelea kuwa na itikadi ya chama waziwazi,hasa leo tunapokuwa na mfumo wa vyama vingi.

Sungu sungu ndio wapo, na hao waliokuja hawakulazimishwa, kama kati yao wapo wa magwanda na wakaamuwa kwenda pale, basi ni ulofa wao uliowapeleka. Sidhani kama kuna aliyelazimishwa pale, au hawa sungu sungu wanalipwa na serikali?
 
Sungusungu wanatambuliwa kisheria kama,Parimentary service.

Ndiyo maana hawapaswi kuwa sehemu au ndani ya Chama flani.

Wasiwasi wangu ni kwanamna wanavyobebwa watatumiwa vibaya sana kufanya vitisho vya hali ya juu katika ngazi za vijiji na jamii kwa ujumla.
Ndio kitu gani hicho?(hapo penye nyekundu iliyokolea)
 
Ndio kitu gani hicho?(hapo penye nyekundu iliyokolea)

sorry typing error nili takakuandika Paramilitary service,am sorry i was busy with another issue inayoelekea na neno nililoandika lakini maana yake nisawa na mgambo.
 
Wakati tunafanya Mchakato wa Katiba Mpya madudu kama haya yanatakiwa kuondolewa mara moja.
Tabia na mwenendo huu wa Kila Taasisi kuwa na Walinzi wake ni hatari kwa ustawi wa jamii hasa kati vyama Vya Siasa.

Kama kweli Jeshi la Polisi lina mahitaji ya rasilimali watu linatakiwa kuajiri moja kwa moja askari hawa wa Sungu Sungu kwa masharti na kanuni zilizopo za jeshi la Polisi na sivinginevyo.
 
Wakati tunafanya Mchakato wa Katiba Mpya madudu kama haya yanatakiwa kuondolewa mara moja.
Tabia na mwenendo huu wa Kila Taasisi kuwa na Walinzi wake ni hatari kwa ustawi wa jamii hasa kati vyama Vya Siasa.

Kama kweli Jeshi la Polisi lina mahitaji ya rasilimali watu linatakiwa kuajiri moja kwa moja askari hawa wa Sungu Sungu kwa masharti na kanuni zilizopo za jeshi la Polisi na sivinginevyo.
Hata binafsi naliona hili.
Naungana na ww ktk ushauri hui kwa serikali
 
Back
Top Bottom