Je ni haki kuipa CHADEMA kura 2020?

Testar

JF-Expert Member
May 30, 2015
7,461
12,216
Wakuu wa JF amani kwenu!
Kuna jambo nimelifikiri kwa muda sasa, nami nikaona ni vema kulileta hapa jukwaani ili tulijadili.Jambo lenyewe ni kuhusu kuipa CHADEMA kura kwenye uchaguzi mkuu ujao wa 2020.Ingawa 2020 inaonekana ni mbali lakini ni miaka minne tu kutoka sasa, hivyo kitu kizuri kinahitaji maandalizi na mikakati ya muda mrefu.

Litakuwa jambo la ajabu kwangu kudhani kwamba kuna chama kingine cha siasa kitakachoweza kuiondoa CCM madarakani tofauti na CHADEMA. CHADEMA ndicho chama kikuu cha upinzani kwa sasa, kimevipita vyama vingine vya upinzani kwa kuwa na mtaji mkubwa wa rasilimali watu hadi fedha.Hivyo nimeona niizungumzie CHADEMA kama possible successor wa CCM kwenye kushika dola kwa mwelekeo wa wakati huu.

HISTORIA YA CHADEMA KATIKA CHAGUZI KUU:
Kwa mbio za urais CHADEMA kimeshiriki chaguzi kuu tatu, yaani chaguzi za 2005, 2010 na 2015.Kwenye chaguzi za 1995 na 2000 CHADEMA kilinga mkono vyama vya NCCR Mageuzi na CUF, kwenye ngazi ya urais.Hawakusimamisha mgombea wa urais kwenye chaguzi tajwa(unaweza kunisahihisha kama nipo kinyume).Kwa maana hiyo mbio za kusaka mlango wa Ikulu kwa CHADEMA zilianza 2005.

CHADEMA NA UCHAGUZI MKUU 2005:
Hapa alisimama F.Mbowe kama mgombea wa kiti cha urais kwa CHADEMA.Kwa mtazamo wangu walijitahidi sana, Mbowe alipata kura 668000 na kitu sawa na 5% na kujinyakulia nafasi ya tatu.Kwenye uchaguzi wa kwanza wa chama kama hiki mbele ya miamba ya siasa kama CCM na CUF ukijumlisha na mitazamo ya watanzania kwa wakati huo, CHADEMA walijitahidi kwa kupata walau zaidi ya kura nusu milioni.Huwezi kuwalaumu hata kidogo zaidi ya kuwapongeza.

CHADEMA NA UCHAGUZI MKUU 2010:
Hapa alisimamishwa Dr.Slaa kama mgombea wa urais.2010 CHADEMA kilishakuwa maarufu karibu maeneo yote ya nchi.Kilishajiimarisha kifedha pamoja na idadi ya wanachama, ushahidi upo kwani Dr.Slaa alipata zaidi ya kura 2000,000.Kutoka kura laki 6 hadi kura milioni 2 na zaidi ilikuwa hatua kubwa ya maendeleo ya kichama.Hata hivyo CHADEMA kilitoa manung'uniko ya kuibiwa kura na CCM.

Dr.Slaa alilalamika sana akidai alipata kura zaidi ya zilizotangazwa na kutaka zoezi la kuhesabu kura lirudiwe.Sii haba kwani wabunge wa CHADEMA waliongezeka maradufu kulinganisha na chaguzi za nyuma.Morali iliyotokana na matokeo ya 2010 ukijumlisha na kuongezeka kwa wabunge, kuliipa CHADEMA nguvu ya kufanya operesheni mbalimbali zilizokitangaza chama nchi nzima.Hata hivyo gear ya kushindwa uchaguzi ilikuwa kuibiwa kwa kura zao na Dr.Slaa hakusaini matokeo ya urais wala kuhudhuria sherehe za kuapishwa kwa mshindi wa urais.

CHADEMA NA UCHAGUZI MKUU 2015:
Huu ndio ulikuwa uchaguzi wa kihistoria tangu tuanze kupiga kura.Hapa alisimamishwa mtu mzima, Edward Lowasa.Ukweli usiopingika watu waliamini CCM ilikuwa hoi sana, hasa kutokana na kashfa za ufisadi zilizopamba sura ya CCM, wachache sana walikuwa na imani nacho.Kuwepo kwa UKAWA,idadi kubwa ya wafuasi wa CDM, nguvu ya Lowasa kisiasa, kulisababisha watu waamini mambo mawili, yaani mwisho wa CCM na mwanzo wa CHADEMA kwenye dola au CCM warudi tena kwa mkono wa chuma.

Mchuwano ulikuwa mkali, watu waliamini EL ndiye rais wa JMT, hata baadhi ya wafuasi wa CCM waliamini hivyo.Ile hofu ya kuibwa kwa kura haikuwepo kwani EL aliwataka watu wampigie kura na kuwaaminisha kuwa hakuna hata kura moja itakayo ibwa.Siku hazigandi mara 25 Oct. ikafika na watu kupanga foleni vituoni kupiga kura.Matokeo ya uchaguzi yanafahamika kwa kila mtu, madiwani, wabunge wa kutosha na kura milioni sita, sii haba kwani hata ushindi wa JK 2010 haukuwa wa kura 6M.

Lakini ukichunguza kwa umakini utagundua kwamba CDM waliangukia pua kwenye uchaguzi wa 2015 kuliko chaguzi zilizopita.Nguvu iliyotumika na matokeo yaliyopatikana haviendani, hawakushinda urais, wabunge wakuchaguliwa hawakufika walau 100 wala mikoa mingine hawakupata wabunge na kupoteza wabunge makini bungeni.Hili jambo lilikatisha watu tamaa juu ya CDM...CDM wamekuwa wakijifariji na vitu kama kupata meya wa JJ la Dar na kuongeza idadi ya wabunge tufauti na ile ya 2010.

Kama ilivyo kwa mbaazi kukauka kisha kusingizia jua, CDM hawakuishiwa na lawama.Walilalamikia tume yenyewe, vyombo vya dola, pamoja na katiba kwa kutokuruhusu kupingwa kwa matokeo ya urais mahakamani.Walifika mbali zaidi na kudai kura ziliibwa na wengine wakadai ''pengine'' EL alishinda kwa 62%.Hizi lawama zimekuwa zikitolewa na CDM mara baada ya kushindwa kwenye uchaguzi, hata 2010 nilizisikia pia.

KUELEKEA UCHAGUZI MKUU 2020:
Itakapofika 2020 CDM watapanda majukwaani tena kuomba kura huku wakiwaaminisha wananchi kwamba wanakwenda kutwaa dola.Kwa mazingira yale yale ya 2010 na 2015, Tume ile ile, na katiba ile ile au watakayoona mbovu zidi(katiba pendekezwa), CDM wata wajaza wananchi matumaini ya kutwaa dola lakini baada ya uchaguzi kupita wanakuja na gear ya lawama

SASA NAULIZA:
Hivi kuelekea 2020 CDM wanafanya maandalizi yapi kutatua lawama zao?

Wana mpango gani kuhakikisha wanapata katiba mpya na tume huru itakayoleta uchaguzi huru?

Watafanya nini kurudisha matumaini na imani ya wananchi juu ya chama na hatimaye kupata kura?

Je kama hali itakuwa kama ilivyo ifikapo 2020, nikiipa CDM kura yangu nitakuwa tofauti na mtu anaye piga pedo baiskeli isiyo na mnyororo huku akiwa na matumaini ya kupanda kilima? au mtu anayejaribu kumpa mimba mwanamke asiye na kizazi kwa matarajio ya kupata mtoto?

NAWASILISHA HOJA KARIBUNI KWA MAJADILIANO.
 
Katiba Mpya wala Tume huru sio vitu vya kutarajia chini ya JPM!Huyu kwake hakuna jema litakalosemwa na wapinzani akalisikia na ndio maana akasema wapinzani wasitegemee uteuzi kwenye awamu yake!Yeye anaaamini anajua kila kitu na wengine wote hawako sahihi!Ndio hivyo tu hamna namna,watu wa namna hii wamejawa visasi na chuki,ni ngumu kubadilika
 
Bado naona CDM wapo kimya, hawafanyi maandalizi ya uchaguzi 2020.Sidhani kama wapo tayari kuchukua nchi 2020.Pengine hawataki kutumia nguvu kubwa sababu wamekata tamaa ya ushindi na wanasubiri hadi 2025.
 
Katiba Mpya wala Tume huru sio vitu vya kutarajia chini ya JPM!Huyu kwake hakuna jema litakalosemwa na wapinzani akalisikia na ndio maana akasema wapinzani wasitegemee uteuzi kwenye awamu yake!Yeye anaaamini anajua kila kitu na wengine wote hawako sahihi!Ndio hivyo tu hamna namna,watu wa namna hii wamejawa visasi na chuki,ni ngumu kubadilika
Je kama CDM wamekata tamaa, nini kifanyike sasa? au wataunga CCM mkono indirectly?
Bado naona CDM wapo kimya, hawafanyi maandalizi ya uchaguzi 2020.Sidhani kama wapo tayari kuchukua nchi 2020.Pengine hawataki kutumia nguvu kubwa sababu wamekata tamaa ya ushindi na wanasubiri hadi 2025.
 
Je kama CDM wamekata tamaa, nini kifanyike sasa? au wataunga CCM mkono indirectly?
Inachotakiwa CDM iwahamasishe wananchi wao ndio wadai haya mambo!Umma ukiwasikia ndio suluhu yaweza patikana,tatizo hata kwenda kwa wananchi wamezuiwa!Huyu Rais anamatatizo sana
 
Inachotakiwa CDM iwahamasishe wananchi wao ndio wadai haya mambo!Umma ukiwasikia ndio suluhu yaweza patikana,tatizo hata kwenda kwa wananchi wamezuiwa!Huyu Rais anamatatizo sana
Sitegemei CDM kudai hivyo vitu peke yao, la hasha...wao wanatakiwa kuwaelimisha watu na kuwahamasisha ili wajue haki zao na kuzidai....sasa watawezaje kama issue ndogo like Ukooter ilifail?
 
Hakuna nchi ya kupewa wakwepa kodi Chadema.

Hiki kizazi kishindwe na kilegee
 
Hakuna nchi ya kupewa wakwepa kodi Chadema.

Hiki kizazi cha Nyumbu kishindwe na kilegee
Naona hasira za mafao ya kujitoa umezileta hapa....jadili issue kwa hoja mkuu...weka hisia pembeni.
 
Wakuu wa JF amani kwenu!
Kuna jambo nimelifikiri kwa muda sasa, nami nikaona ni vema kulileta hapa jukwaani ili tulijadili.Jambo lenyewe ni kuhusu kuipa CHADEMA kura kwenye uchaguzi mkuu ujao wa 2020.Ingawa 2020 inaonekana ni mbali lakini ni miaka minne tu kutoka sasa, hivyo kitu kizuri kinahitaji maandalizi na mikakati ya muda mrefu.

Litakuwa jambo la ajabu kwangu kudhani kwamba kuna chama kingine cha siasa kitakachoweza kuiondoa CCM madarakani tofauti na CHADEMA. CHADEMA ndicho chama kikuu cha upinzani kwa sasa, kimevipita vyama vingine vya upinzani kwa kuwa na mtaji mkubwa wa rasilimali watu hadi fedha.Hivyo nimeona niizungumzie CHADEMA kama possible successor wa CCM kwenye kushika dola kwa mwelekeo wa wakati huu.

HISTORIA YA CHADEMA KATIKA CHAGUZI KUU:
Kwa mbio za urais CHADEMA kimeshiriki chaguzi kuu tatu, yaani chaguzi za 2005, 2010 na 2015.Kwenye chaguzi za 1995 na 2000 CHADEMA kilinga mkono vyama vya NCCR Mageuzi na CUF, kwenye ngazi ya urais.Hawakusimamisha mgombea wa urais kwenye chaguzi tajwa(unaweza kunisahihisha kama nipo kinyume).Kwa maana hiyo mbio za kusaka mlango wa Ikulu kwa CHADEMA zilianza 2005.

CHADEMA NA UCHAGUZI MKUU 2005:
Hapa alisimama F.Mbowe kama mgombea wa kiti cha urais kwa CHADEMA.Kwa mtazamo wangu walijitahidi sana, Mbowe alipata kura 668000 na kitu sawa na 5% na kujinyakulia nafasi ya tatu.Kwenye uchaguzi wa kwanza wa chama kama hiki mbele ya miamba ya siasa kama CCM na CUF ukijumlisha na mitazamo ya watanzania kwa wakati huo, CHADEMA walijitahidi kwa kupata walau zaidi ya kura nusu milioni.Huwezi kuwalaumu hata kidogo zaidi ya kuwapongeza.

CHADEMA NA UCHAGUZI MKUU 2010:
Hapa alisimamishwa Dr.Slaa kama mgombea wa urais.2010 CHADEMA kilishakuwa maarufu karibu maeneo yote ya nchi.Kilishajiimarisha kifedha pamoja na idadi ya wanachama, ushahidi upo kwani Dr.Slaa alipata zaidi ya kura 2000,000.Kutoka kura laki 6 hadi kura milioni 2 na zaidi ilikuwa hatua kubwa ya maendeleo ya kichama.Hata hivyo CHADEMA kilitoa manung'uniko ya kuibiwa kura na CCM.

Dr.Slaa alilalamika sana akidai alipata kura zaidi ya zilizotangazwa na kutaka zoezi la kuhesabu kura lirudiwe.Sii haba kwani wabunge wa CHADEMA waliongezeka maradufu kulinganisha na chaguzi za nyuma.Morali iliyotokana na matokeo ya 2010 ukijumlisha na kuongezeka kwa wabunge, kuliipa CHADEMA nguvu ya kufanya operesheni mbalimbali zilizokitangaza chama nchi nzima.Hata hivyo gear ya kushindwa uchaguzi ilikuwa kuibiwa kwa kura zao na Dr.Slaa hakusaini matokeo ya urais wala kuhudhuria sherehe za kuapishwa kwa mshindi wa urais.

CHADEMA NA UCHAGUZI MKUU 2015:
Huu ndio ulikuwa uchaguzi wa kihistoria tangu tuanze kupiga kura.Hapa alisimamishwa mtu mzima, Edward Lowasa.Ukweli usiopingika watu waliamini CCM ilikuwa hoi sana, hasa kutokana na kashfa za ufisadi zilizopamba sura ya CCM, wachache sana walikuwa na imani nacho.Kuwepo kwa UKAWA,idadi kubwa ya wafuasi wa CDM, nguvu ya Lowasa kisiasa, kulisababisha watu waamini mambo mawili, yaani mwisho wa CCM na mwanzo wa CHADEMA kwenye dola au CCM warudi tena kwa mkono wa chuma.

Mchuwano ulikuwa mkali, watu waliamini EL ndiye rais wa JMT, hata baadhi ya wafuasi wa CCM waliamini hivyo.Ile hofu ya kuibwa kwa kura haikuwepo kwani EL aliwataka watu wampigie kura na kuwaaminisha kuwa hakuna hata kura moja itakayo ibwa.Siku hazigandi mara 25 Oct. ikafika na watu kupanga foleni vituoni kupiga kura.Matokeo ya uchaguzi yanafahamika kwa kila mtu, madiwani, wabunge wa kutosha na kura milioni sita, sii haba kwani hata ushindi wa JK 2010 haukuwa wa kura 6M.

Lakini ukichunguza kwa umakini utagundua kwamba CDM waliangukia pua kwenye uchaguzi wa 2015 kuliko chaguzi zilizopita.Nguvu iliyotumika na matokeo yaliyopatikana haviendani, hawakushinda urais, wabunge wakuchaguliwa hawakufika walau 100 wala mikoa mingine hawakupata wabunge na kupoteza wabunge makini bungeni.Hili jambo lilikatisha watu tamaa juu ya CDM...CDM wamekuwa wakijifariji na vitu kama kupata meya wa JJ la Dar na kuongeza idadi ya wabunge tufauti na ile ya 2010.

Kama ilivyo kwa mbaazi kukauka kisha kusingizia jua, CDM hawakuishiwa na lawama.Walilalamikia tume yenyewe, vyombo vya dola, pamoja na katiba kwa kutokuruhusu kupingwa kwa matokeo ya urais mahakamani.Walifika mbali zaidi na kudai kura ziliibwa na wengine wakadai ''pengine'' EL alishinda kwa 62%.Hizi lawama zimekuwa zikitolewa na CDM mara baada ya kushindwa kwenye uchaguzi, hata 2010 nilizisikia pia.

KUELEKEA UCHAGUZI MKUU 2020:
Itakapofika 2020 CDM watapanda majukwaani tena kuomba kura huku wakiwaaminisha wananchi kwamba wanakwenda kutwaa dola.Kwa mazingira yale yale ya 2010 na 2015, Tume ile ile, na katiba ile ile au watakayoona mbovu zidi(katiba pendekezwa), CDM wata wajaza wananchi matumaini ya kutwaa dola lakini baada ya uchaguzi kupita wanakuja na gear ya lawama

SASA NAULIZA:
Hivi kuelekea 2020 CDM wanafanya maandalizi yapi kutatua lawama zao?

Wana mpango gani kuhakikisha wanapata katiba mpya na tume huru itakayoleta uchaguzi huru?

Watafanya nini kurudisha matumaini na imani ya wananchi juu ya chama na hatimaye kupata kura?

Je kama hali itakuwa kama ilivyo ifikapo 2020, nikiipa CDM kura yangu nitakuwa tofauti na mtu anaye piga pedo baiskeli isiyo na mnyororo huku akiwa na matumaini ya kupanda kilima? au mtu anayejaribu kumpa mimba mwanamke asiye na kizazi kwa matarajio ya kupata mtoto?

NAWASILISHA HOJA KARIBUNI KWA MAJADILIANO.
Hata mkiwapa kura kiti hawatapewa,, niko hapa Nrb kuna msemo wa kejeli wameanzisha wanasema "Kura kwa BABA, kiti kwa UHURU,,,
 
Bado naona CDM wapo kimya, hawafanyi maandalizi ya uchaguzi 2020.Sidhani kama wapo tayari kuchukua nchi 2020.Pengine hawataki kutumia nguvu kubwa sababu wamekata tamaa ya ushindi na wanasubiri hadi 2025.


siasa hakuna hadi 2020 hilo limekaaje na ukimya wao? maandano ya amani yalipingwa serikali iliandaa jeshi la polis na jwtz kwa kigezo cha usafi hapo kumekaaje?
 
Je kama CDM wamekata tamaa, nini kifanyike sasa? au wataunga CCM mkono indirectly?
Naona unaleta uchokozi au Lumumba wamekutuma!!
Eti CDM wanafanya nini wakati mikutano yote ya siasa imezuiliwa kwa woga wa kuambiwa ukweli!!
Watu sio wajinga hata mjitie kuruka sarakasi,mara kutisha wapinzani kuwaweka ndani watu wanaona, ukweli unajulilana!!
Hata mkikataa katiba mpya, tume huru ya uchaguzi, CDM imeimarika saana!!
Uongo na ulaghai umefika kikomo, mbivu na mbichi itajulikana siku itakapo fika!!
 
Ingekuwa ni Lumumba inashambuliwa hivi mngeita Uchochezi!!
Hapana Mkuu mimi nimeuliza tu, kama kila chaguzi wanasema wameibiwa kura kura, je 2020 kuna uhakika gani wa kutokuibiwa kura ili tuwape kura zetu?
 
Naona unaleta uchokozi au Lumumba wamekutuma!!
Eti CDM wanafanya nini wakati mikutano yote ya siasa imezuiliwa kwa woga wa kuambiwa ukweli!!
Watu sio wajinga hata mjitie kuruka sarakasi,mara kutisha wapinzani kuwaweka ndani watu wanaona, ukweli unajulilana!!
Hata mkikataa katiba mpya, tume huru ya uchaguzi, CDM imeimarika saana!!
Uongo na ulaghai umefika kikomo, mbivu na mbichi itajulikana siku itakapo fika!!
Nadhani hujaelewa dhamira yangu ipo wapi.Je kama kazi ya CDM ni siasa, alafu wanakatazwa kufanya siasa, ni sawa na kusema CDM wamekatazwa kufanya kazi nao wakakubali?...Pili CDM wanampango gani wa kupata katiba au tume huru ili 2020 kuwepo na uchaguzi huru?
 
siasa hakuna hadi 2020 hilo limekaaje na ukimya wao? maandano ya amani yalipingwa serikali iliandaa jeshi la polis na jwtz kwa kigezo cha usafi hapo kumekaaje?
Mkuu kwahiyo ndio kusema kwamba hakuna demokrasia ya vyama vingi? pia kama sep 1 ilikuwa busy, mbona wamepanga siku nyingine yaani oc t 1, je watafanya kweli?
 
Hata mkiwapa kura kiti hawatapewa,, niko hapa Nrb kuna msemo wa kejeli wameanzisha wanasema "Kura kwa BABA, kiti kwa UHURU,,,
Nionavyo hapo ni ukosefu wa tume huru....sasa wapinzani wana mpango gani wa kupata tume huru ili pawepo na uchaguzi huru?
 
Mkuu kwahiyo ndio kusema kwamba hakuna demokrasia ya vyama vingi? pia kama sep 1 ilikuwa busy, mbona wamepanga siku nyingine yaani oc t 1, je watafanya kweli?


Nasikia mkuu wa mikoa katangaza hiyo siku ni ya upandaji miti tanzania nzima jeshi limeombwa kushiriki tusubir tuone mkuu
 
Nasikia mkuu wa mikoa katangaza hiyo siku ni ya upandaji miti tanzania nzima jeshi limeombwa kushiriki tusubir tuone mkuu
Yaani nature ya upinzani tulionao ni shida sana, waoga na wasio na ujasiri wa kudai haki....nadhani bado tungekuwa chini ya utawala wa kikoloni kama hawa wapinzani wangekuwa ndio wapigania uhuru.
 
Bado hajatokea mpinzani wa kweli Tanzania...Chadema ya sasa ni kama tawi la mafisadi,vibaka na wakwepa kodi wakati kiasili nchi hii ni ya wakulima na wafanyakazi
 
Back
Top Bottom