Je,naweza kukaa kivyangu?

Pdidy

JF-Expert Member
Nov 22, 2007
50,906
22,023
Je,naweza kukaa kivyangu?



Je, kutengana kati ya mke na mume bila kupeana talaka ni jambo linaloruhusiwa kibiblia hasa kama kuna matatizo ya ndoa kama kupigana au mmoja kutokuwa mwaminifu?

Kwa kuwa kuendelea kwa ndoa ni mapenzi ya Mungu bado kutengana kwa muda huweza kusaidia hasa pale wanandoa walio katika wakati mgumu kuendelea kupewa ushauri na usuluhishi ili warudiane bila kuumizana.

Kutengana kwa aina hii husaidia hasa kwa mwanamke ambaye ameolewa na mwanaume violent, mlevi au mwingi wa habari na hii ni kwa ajili ya safety ya mke na mke au mume haruhusiwi kuwa na partner mwingine kwani kuwa na miadi (dating, outing) na mwanaume mwingine kama ni mwanamke au mwanamke mwingine kama ni mwanaume huweza kusababisha mahusiano na ki-emotions na feeling na kusababisha kurudiana na mke au mume wake kuwa vigumu zaidi.
Na mtazamo mkubwa unatakiwa ni kulenga wanandoa kurudiana na kuendelea na ndoa yao na si vinginevyo.

(Kwa maelezo zaidi soma 1Wakorintho 7:10 - 11)
 
Back
Top Bottom