Massenberg
JF-Expert Member
- Jun 4, 2011
- 1,173
- 1,370
Siasa za nchi nyingi duniani, Tanzania ikiwemo, ni za milengo au vyama tofauti, lakini pamoja na utofauti huu yapo mambo ambayo huwa yanafanana na si jambo la ajabu kukuta mtu wa upande mmoja akikubaliana hadharani na mambo fulani ya upande mwingine.
Tumemsikia Nape mara nyingi akikemea mambo kama rushwa na uongozi mbaya usio na manufaa kwa wananchi. Haya ni baadhi ya mambo ambayo Chadema pia mara zote inayakemea.
Swali ni kwamba je, Nape yuko tayari kutamka hadharani kwamba anakubaliana na Chadema katika kusisitiza ubaya wa rushwa na maovu mengineyo ambayo yanaliumiza taifa na kuahidi kushirikiana nao kuyatokomeza?
Tumemsikia Nape mara nyingi akikemea mambo kama rushwa na uongozi mbaya usio na manufaa kwa wananchi. Haya ni baadhi ya mambo ambayo Chadema pia mara zote inayakemea.
Swali ni kwamba je, Nape yuko tayari kutamka hadharani kwamba anakubaliana na Chadema katika kusisitiza ubaya wa rushwa na maovu mengineyo ambayo yanaliumiza taifa na kuahidi kushirikiana nao kuyatokomeza?