GodfreyTajiri
JF-Expert Member
- Sep 26, 2010
- 981
- 652
sasa mbona hujawaeleza kama wale ambao tayari wanawatoto/mtoto
kama wanaweza kutoma maombi. maana hiyo range ya 18 -30
unaweza wakuta wenye vibebi lakini hawajaolewa.
kama wanaweza kutoma maombi. maana hiyo range ya 18 -30
unaweza wakuta wenye vibebi lakini hawajaolewa.
Habari zenu wana JF,
Mwaka huu nipo katika harakati za kutafuta mchumba katika mazingira ninayoishi na kwingineko, nimeona sio vibaya pia nikiweka wazi nia yangu hapa ili mwanamke yoyote anayedhani namfaa au ananifaa tuweze kuwasiliana, pengine hapa ndio mahali ambapo Mungu amepanga hasa tukutane.
Mimi ni mwanaume mwenye umri wa miaka 30 (kijana wa makamo), ninafanya kazi katika kampuni binafsi, mrefu kiasi, mweusi mwenye umbo la wastani. Ninaishi Arusha na Dar -es –Salaam.
Natafuta mchumba mwanamke mwenye umri kuanzia miaka 18 – 30. Elimu kuanzia ya sekondari na kuendelea, awe anafanya kazi au awe tayari kufanya kazi ya kujiajiri au kuajiriwa. Awe mkristu au kwa ambaye sio mkristu awe tayari kubadili dini. Awe mcha Mungu, anayejiheshimu, asiye na majivuno wala mwenye makuu, mwenye tabia nzuri na mpenda maendeleo kwa ujumla.
Kwa mwenye nia ya dhati tu, aniPM au kuniandikia e-mail kupitia onyango.alex@gmail.com
Maoni yanakaribishwa pia.