mpayukaji
JF-Expert Member
- Oct 31, 2010
- 940
- 349
Habari zilizorushwa na kituo cha Televisheni cha Al Jazeera ni kwamba kiongozi wa muda wa Libya Mustaafa Abdul Jalil amekiri kushindwa kuimiliki Libya baada ya kumwangusha na kumuua imla wa zamani Muamar Gaddafi. Je kwa mara nyingine tutashuhudia Irak nyingine? Je mataifa ya Magharibi yaliyompindua Gaddafi yako wapi? Taarifa zilizopo ni kwamba yameshindwa hata kuuamini utawala mpya!