Je kwa kosa hili NI SAHIHI KWA MKE KUMUITA MUMEWE MJINGA?

Kima mdogo

JF-Expert Member
Sep 17, 2011
303
46
Kuna familia mbili wake na waume zao walikua marafiki sana kwa bahati mbaya mume wa mke m1 akafariki, yule mke mjane akawa anaendeleza urafiki na kuomba misaada kwa rafiki zake hao na mume wa familia rafiki akawa anamsaidia, mke wa hy mume hakufurahia na alimweleza mumewe kw anawasiwasi kw mumewe anatembea na mjane huyo. JANA MJANE HUYO AKAMWALIKA MUME HUYO KWNY SHEREHE NYUMBANI KWAO LKN HAKUMWALIKA MKEWAKE, MUME AKAENDA NA AKARUDI SA 2 USIKU, MKE AKAMWAMBIA MUMEWE KW HAKUJUA KUWA NI MJINGA KIAS HICHO. mume akaamua kuhama chumba. JE ALIVYOFANYA MUME KWENDA KWENYE SHEREHE BILA MKEWAKE NI SAWA? NA JE MKE KUMUITA MUMEWE MJINGA NI SAWA? NA MUME KUCHUKUA UAMUZI WA KUHAMA CHUMBA NI SAHIHI?
 
Mmmmhh kweli ndoa sio jambo la mzaha.
Wote wana makosa,
1. Hakuwa na haja ya kuchukia huyo mjane coz hana mume, ni rafiki yake kipenzi, ni mtu aliye karibu naye na ni mshauli wake mkubwa, hivyo suala la kumzuia mumewe asimsaidie alikupaswa kuwepo alikosea, nini maana ya ushoga.
Mume naye asingepaswa kuwa karibu sana na huyo mjane, mpaka wanakaribishana kwenye sherehe kisiri siri, huyo mjane angemkaribisha mume na mke na wote kwa pamoja wakahudhuria, hata kama mjane alimkaribisha mume, mume angekuwa na busara, angeongozana na mkewe kwenye hiyo sherehe. Na huyo mjane hakupaswa kuwa karibu sana na mme wa mtu. Mwanamke huenda alitamka hivyo kwa hasira, hivyo mume amsamehe na maisha yaendelee, Ila mume safari zingine aongozane na mumewe panapobidi kufanya hivyo.
 
Haya mambo yanahitaji busara zaidi ya mihemko!
unavyosema ni kweli mkuu, pmj na kumsihi sn huyu mume asichukue uamuzi wwt mpaka hasira zishuke kakataa katakata anadai haendi nymbn sk 3 na siku atakapokwenda ataendelea kulala chumba kingne. imekaa sawa hii wakuu?
 
Kwanini mjane hakumwalika mwanamke mwenzie?je huyo mwanaume alimweleza kuwa mwenzio hapendi nikusaidie?kama alimweleza pengine hicho ndio kikwazo ila angepaswa kwenda na mkewe . ni vizuri kusaidia wajane na yatima( Neno linasema) hata yeye hajui kama atamaliza safari yake bila kuwa mjane......Kumtukana mume/mke ni kosa la jinai ....hatuna sababu za kutosha mpaka ifikie kutukanana...mweleze shemeji yako aombe msamaha kwa mumewe...amejifungulia lango mwenyewe...mwanamke mwenye busara huijenga nyumba kwa hekima bali mpumbavu huibomoa kwa mikono yake mwenyewe
 
mimi naona ni sahii kwa huyu mwanaume kuitwa mjinga na mke wake maana na yeye alitakiwa amuulize yule mwanamke aliyemwalika umemwambia mke wangu?akimwambia ajamwalika amwambie basi mimi siwezi kwenda peke yangu.Maana kama yule mwanamke angekuwa na nia njema angewaalika wote. huyo mjane lazima atakuwa na hila.
 
Mjane na mme wa mtu wana jamiana ndo maana mjane kathubutu kumualika mme wa mtu na kumbagua mke wa jamaa.WIZI MTUPU
 
Japo wote wana makosa lakini hilo la mke kumwambia mumewe ni mjinga halifai kabisa coz wangeweza kukalishana chini na wakazungumza yakaisha!! Anyways, waombane msamaha yaishe na itapendeza sana iwapo mke ndo awe wa kwanza kumuomba mumewe msamaha coz amemdiappoint sana!! (though its not bad hata mume akianza)
 
mke-mpumbaav kwa ku pre judge

mme- mpumbaav kwa kuhama chumba

mjane-mpumbaav kwa kumualika mme wa mwenzie pekee bila mkewe

my take:nakamata wote watatu then nafunga mtini afu naanza kuchalaaza viboko
 
kuna familia mbili wake na waume zao walikua marafiki sana kwa bahati mbaya mume wa mke m1 akafariki, yule mke mjane akawa anaendeleza urafiki na kuomba misaada kwa rafiki zake hao na mume wa familia rafiki akawa anamsaidia, mke wa hy mume hakufurahia na alimweleza mumewe kw anawasiwasi kw mumewe anatembea na mjane huyo. Jana mjane huyo akamwalika mume huyo kwny sherehe nyumbani kwao lkn hakumwalika mkewake, mume akaenda na akarudi sa 2 usiku, mke akamwambia mumewe kw hakujua kuwa ni mjinga kias hicho. Mume akaamua kuhama chumba. Je alivyofanya mume kwenda kwenye sherehe bila mkewake ni sawa? Na je mke kumuita mumewe mjinga ni sawa? Na mume kuchukua uamuzi wa kuhama chumba ni sahihi?

je na wewe ni sahihi kuileta stori ya famili mbili hapa jamvini???
 
Mke kumwita mume mjinga ni kosa ila mume alitakiwa ajishushe na amueleweshe mkewe kwa upole na wote waombane msamahaa kwa kuelewana vibaya, kukimbia chumba ni sawa na kukimbia kivuli chake siku zote haifai kukimbia matatizo bali ni kuyakabiliia chumba anazidi kumjengea wasi wasi mkewe na kuhisi ni kweli aliyohisi, Mume alivyofanya kukimb ila mjane ndo source ila yawezekana alikuwa na mazungumzo ya binafsi zaidi na alitaka ama kuomba ushauri kwa mambo yanayomtatiza baada ya msiba wa mumewe toka kwa huyo mwanaume, kwa hiyo inawezekana alitaka ufree zaidi kuwasilisha matatizo yake. Ila mwanaume kuepuka kadhia km hiyo alitakiwa kumuuliza aliyemwalika km ni lazima aende pekee yake na kwa nn maana yy ni mwanandoa.
Angalizo, huyo mwanaume isije ikawa ni Mpango wake wa Kando huyo Mjane (small hs), ongea naye akupe ukweli.
 
mhhh nahisi mtoa mada ndio yalomkuta anaogopa kusema kama ni yeye.pole mkuu nadhani mikatabafeki ameshakupa jibu nlotaka kukupa.
 
huyo mume amekuwa na mawasiliano na mjane ambayo yanatia mashaka,amealikwa kwenye sherehe na mjane na yeye akaenda bila kumshirikisha mkewe? hata kama ilikuwa ni kwa nia njema lakini hilo lakutomshirikisha mkewe linatia dosari na wasiwasi...., huyo mwanamke amepaniki na ameshindwa kucontrol hasira as a results akamwita mumewe mjinga na mume kuonyesha ni jinsii gani ni mjinga akahama chumba! two wrongs doesnt make it right..,on the face of it mume anamakosa coz alichokifanya kinacreate doubt kwa mkewe na mkewe alikuwa na haki ya kuuliza na kuhamaki, to wat level mke amehaki imeleta shida nyingine, but mume hakupaswa kuhama chumba,angejilalia zake the next morning aongeongea na mkewe akiwa ametulia, hope wangesolve tatizo ila anavyozidi kumkimbia mkewe na anavyozidi kudhihirisha kuwa huo mualiko ulikuwa ni zaidi ya mualiko wa kawaida.
 
kitendo tu cha mwanaume kumnunia mwanamke bila kujali sababu; ni ujinga.. Kitendo cha mwanaume kwenda kwenye sherehe ilhali anajua kwamba mkewe hakualikwa na bila kumshirikisha mkewe kwanza; pia ni ujinga... Mwanamke amekosea kumtusi jamaa, lakini mwanaume ana makosa zaidi kwa kumwekea bifu mkewe!!
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom