Katika kuongea na wadogo zangu kilimu nimepata kusikia mhitimu mmoja wa Kidato cha Sita akiilalamikia TCU kwa kumpeleka chuo na programu asiyopendekeza. Amedai ya kwamba amechaguliwa UDSM kusoma Sheria ilihali hajaomba kusoma Sheria katika Chuo chochote kile, pia hajaomba kusoma chochote UDSM.
Pia amedai ya kwamba kuna rafiki yake amechaguliwa IFM kusoma Computer ilihali hajasoma masomo ya Sayansi, yeye amsoma HGK.
Naomba kuuliza, je kuna mtu aliyechaguliwa kusoma chuo na kozi isiyo chaguo lake?
Pia amedai ya kwamba kuna rafiki yake amechaguliwa IFM kusoma Computer ilihali hajasoma masomo ya Sayansi, yeye amsoma HGK.
Naomba kuuliza, je kuna mtu aliyechaguliwa kusoma chuo na kozi isiyo chaguo lake?