Je, jina lako/ID unalotumia JamiiForums lina maana yoyote?

Jina linajieleza. Niliamua kutumia jina hilo ili, kwanza kuuonesha umma kuwa hata katika nchi ambayo imejaa watu corrupt, bado tupo waadilifu wachache, na nimekuwa nikijitahidi siku zote (kwa msaada wa Mungu) kuishi sawa sawa na jina langu. Pili kuleta ladha ya tofauti, maana nimekuwa nikishuhudia majina yanayopendwa sana siku hizi, ni Fisadi(mtoto), Shetani, "mwaga ugali nimwage mboga"..etc. Tanzania yenye uadilifu inawezekana, usisubiri wawepo wengi, anza wewe wengine watafuata.
 
So many aliases so many arguments depending on the forum. Humu niliona bora niwe Juma Contena why? baada ya kusoma ya kwamba bandari ina 'nada' karibu makontena 8,000 kwa mwaka.

Kwa kujiuliza nikaona hayo yatakua ni ya wale walalahoi tu, na kwa sababu yanaishia mnadani nikajiuliza maana ya mnada ni ili mradi liende. Kwa mantiki hiyo yanaishia kuuzwa kwa bei ya chini zaidi kuliko waliyo mletea mwenye bidhaa.

Hivyo ni nani anayo nunua na lini unafanyikaga mnada wa bandari na how much loss inapatika baada ya kumkomoa mtanzania asiekua na connection. Ufisadi wa mali ya Umma ni kitu kingine lakini huu ni Uhuni wa hali ya juu kwani ni uporaji wa watu wanaotaka kujiinua kimaisha, kwa manufaa ya wachache na nina guarantee asilimia kubwa ya wahudhuriaji wa huo mnada ni wadosi.

Ndipo jina la Juma lilipoingia (Much associated with strugglers) and Contena (the stolen goods) of these people at the port.

hapo ndipo nilipoona umuhimu wa kujiunga na JF lakini still bado im trying to figure out how to start my battle having no particular political party na so far it has proven to be (JF) full of fantasies if im honest.

Na wengi humu naona matatizo ya walalahoi sio concern yao bali mafisadi tu, yes ni tatizo lakini mbona atu question the use of public funds how much ends in the hands of the administrators na how much kweli inafanya hiyo kazi. Tuna bajeti kila mwaka lakini maendeleo yetu ni stagnant sasa hiyo hela ina endega wapi.

I think we are asking the wrong questions, na tunapigana vita ya wengine opposition political parties ambazo sidhani kama wanamfikiria mtanzania bali hela ya tanzania. Evidence ni jinsi wanavyolumbana wenyewe kwa wenyewe all the time hii ni ishara there's more of a political interest than the woes of disadvantaged Tanzanians.

Thats my view and the battle I aim to bring (talking on behalf of these poeple) without endorsing a political party, they will hear me when im ready to take it to their doorsteps, watch this space. I understand my naivity.

Ps. I dont loose
 
Hajakosea kabisa hata kidogo, usijaze chochote ndio ukweli wenyewe?????? Lakini kuvuta bangi na kuibia maskini kipi afadhali, halafu elewa kuwa wanaovuta bangi wote ni shauri ya umaskini ili kupoteza mawazo ya kuonewa kunyanyaswa na kudhulumiwa. Wengine nanapoteza mawazo kama ifuatavyo Baada ya wavuta bangi wanafuata wanywa gongo na pombe za kienyeji baada ya hao wale wanokunywa bia kwenye kontainer, halafu hivyo hivyo upwards mpaka wale ambao wanatuibia na wakifurahia na kusherehekea kuiba huenda kujitakasa sehemu huku wakicheza gofu, kuvua samaki na maboti yao yenye baa ndani na au kunywa bia ya shs 4000/=, hela ambayo ambao ukimpa mvuta bangi ataenda kununulia watoto utumbo wa kuku ili wanae wasuuze matumbo yao yaliyochoka dagaa , mchunga na mnyavu.Lakini kabla ya wavuta bangi kuna wale wavuta petroli ambao hawana hamu ya kuishi wao wanatafuta njia ya mkato ya kwenda jehanamu na wako wengine wa unga hawa labda nisaidiwe nashindwa kuwaweka kwenye kundi muafaka.

Hawa tayari wako ahera ndio maana wanabembea kwa raha zao!
 
Fugwe, kikwetu ni Kobe. Kobe kwa asili yake ni mnyama mstaarabu sana, anapenda amani, na nimkaa kimya. Katika ukimya wake tunaamini kikwetu anautumia kutafakari mambo yaliyopo na yale yanayokuja. Ukimchokoza hawezi kulipiza kisasi bali anajificha kwa kutumia gamba lake gumu. Kuhusu 'Avatar' yangu, hilo ni kaburi alimozikwa Baba wa Taifa hayati MWL NYERERE, napenda yale yote aliyofanya mazuri, aliyotuasa tusiyafanye, watu aliowakataa katu wasipewe uongozi kama watapewa watakuwa kama mbwa mwenye njaa aliyekabidhiwa nyama ailinde. Hao si wengine ni akina Bazil Mramba na Mwenzake Lowassa.
 
Laligeni...Napokea wageni wote wa kike na kiume!!! Peace & Love!!!
 
Well mine huwa linanikumbusha when I was 4 if nt five. Grandma used to call mi nyambala - Mwanamume (wa shoka) ofcourse. Ilinisumbua sana kufigure out the real meaning and it sounded so funny ukizingatia wakati huo nilikuwa sijajua lugha hiyo. Anyways I use the name just bcoz I care of those ol memories. And by the way ni Jibaba kweli kweli.
 
august maana yake kwa ki-latini ni great or/and magnificent , kwa hiyo ni mtu ninaye penda kuona tanzania ina kuwa hivyo kwa namna yake ya pekee, sio kwamba wawe na jeshi kubwa lenye kudhulumu wengine bali kuwa na vitu vizuri ili kulinda heshima ya mwanadamu iwe kiuchumi, kisiasa, kimichezo, kitaaluma, kiafya ,kiuongozi,kijeshi, mazingira yetu yawe safi nk nk inayo husiana na kitu kuwa kizuri. mfano vijiji vyetu viwe kamilifu na maji ya bomba , umeme, zahanati/hospitali nzuri shule nzuri na watendaji wazuri, sioni sababu ya zaidi ya miaka 40 ya uhuru wetu tunakosa vitu hivyo, watu wanabanabana kwenye pick-up kama njia ya usafiri nk nk.
 
Jina linajieleza. Niliamua kutumia jina hilo ili, kwanza kuuonesha umma kuwa hata katika nchi ambayo imejaa watu corrupt, bado tupo waadilifu wachache, na nimekuwa nikijitahidi siku zote (kwa msaada wa Mungu) kuishi sawa sawa na jina langu. Pili kuleta ladha ya tofauti, maana nimekuwa nikishuhudia majina yanayopendwa sana siku hizi, ni Fisadi(mtoto), Shetani, "mwaga ugali nimwage mboga"..etc. Tanzania yenye uadilifu inawezekana, usisubiri wawepo wengi, anza wewe wengine watafuata.

Naam ndugu yangu, Tanzania yenye uadilifu na isiyo na mafisadi inawezekana kabisa.
 
Mimi pia kwa wale waliotazama filamu ya analyze this
ya robert deniro
mtakumbuka kuna sehemu aliulizwa na daktari wake..
What do u do????
Akajibu ..what do i do???am the boss.....i dont do anything..
It was so funny....
 
Jina langu (Freetown)linatokana na mji nilioishi siku za nyuma huko West Africa, linanikumbusha mengi sana ndo maana bado nalitumia
 
All my children have their first names beginning with J.Ndivyo ninavyofahanika kule uswahilini kwetu.
 
All my children have their first names beginning with J.Ndivyo ninavyofahanika kule uswahilini kwetu.

Ha ha ha ha we mkali! Jay, Jay, Jay na Jay unanikumbusha George Foreman watoto wake wote wa kiume nadhani aliwapa jina la George na mwanamke akamuita Georgina.
 
Kwa hilo linahitaji ubunifu mkubwa. Kil bark. Kil ni Kilimanjaro ambapo ni asili yangu na bark ni sauti ya mbwa anayebweka kufukuza wezi. Sitaki kuwa mkabila isipokuwa naipenda asili yangu na watu wangu kwani sio waoga. Waulize CCM kuhusu mkoa wa Kilimanjaro.
 
hili ni jina langu la asili nililopewa na bibi, lkn wakanibatiza kwa jina lingine la kidhungu, bado nalipenda jina langu ndio maana nikaamua kulitumia hapa JF
 
Chimunguru ni Jina langu halisi lipo kwenye cheti changu cha ubatizo naitwa Chimunguru Chiziwa. NALIPENDA JINA HILI sababu sipendi tumia SLAVE NAMES, naamini ntakuwa nimetumia jina la asili yangu. Babu yangu alikuwa akiniambia miaka hiyo yuko hai, EEeh mnyanga, mtombo, chiziwa, mchoramiti, chimunguru, kateke manji tupuuze. Ntakuja wambia maana ya huu usemi.
 
Kwetu ayayoru maana yake ni sisi kwa sisi binafsi niliamua kutumia jina hilo baada ya kuona mambo hayaeleweki kila sehemu rushwa,ufisadi na nk so nikaamua kuatumia hiyo id coz hayo yote tunafanya sisi kwa sisi watanzania wenyewe watu wanaiba mali ya umma,haki hakuna kwa wanyonge na tofauti ya maskini na tajiri inaongezeka haya yote twafanyiana wenyewe sisi kwa sisi watanzania
 
KAITABA, ni uwanja wa mpira upo mkoani Kagera, mama yangu mzazi alikuwa bosi enzi hizo, akiwa anakagua gwaride uwanjani hapo akashikwa na uchungu,

Alipopelekwa chumba cha faragha uwanjani hapo nikazaliwa mimi,
 
53 Reactions
Reply
Back
Top Bottom