Je, jina lako/ID unalotumia JamiiForums lina maana yoyote?

TalibKweli aka Kweli ni jina ambalo nalitumia kwenye mitandao tofauti ya Kibongo kitambo, ni jina alilonipa swahiba wangu mmoja mnamo mwaka 1989 pale Piraeus,Greece kutokana na kupenda kwangu sana Hip-hop na kutema mistari kama Talib Kweli.
 
Hofstede: I admire the work of Geert Hofstede founder of five dimensions of culture in his study of national work related values:

1. Low vs. high power distance - This dimension measures how much the less powerful members of institutions and organizations expect and accept that power is distributed unequally

TZ tupo kwenye high power distance kwani viongozi wetu wengi wanajiona ni miungu watu, na kiburi hicho kinatokana na vyeo vya kupewa na kuiba kura. Mkuu wa mkoa kama angekuwa anapigiwa kura huru na haki jimboni basi angewajibika kwa wananchi na siyo kwa aliyemteua, sama tu most leaders hasa vijijini watu wananyanyasika sana.

2. Individualism vs. collectivism - This dimension measures how much members of the culture define themselves apart from their group memberships

Tulikuwa kwenye collectivism wakati wa Nyerere, Sasa tumeingia kwenye Individualism kwa kasi, viongozi hawajali wananchi kila mtu on your own, wananchi nao hawathaminiani kwa maisha magumu sana. "Struggle for existance, survival for the fittest"- rule of the jungle ndiyo inatawala Tanzania ya sasa.

3.Masculinity vs. femininity - This dimension measures the value placed on traditionally male or female values (as understood in most Western cultures). In so-called 'masculine' cultures, people value competitiveness, assertiveness, ambition, and the accumulation of wealth and material possessions.

TZ tupo kwenye masculinity japo mitandao ya TGNP imefanya kazi kupunguza

4. Low vs. high uncertainty avoidance - This dimension measures how much members of a society attempt to cope with anxiety by minimizing uncertainty.

Tanzania tupo kwenye "high uncertainty avoidance" kwani ni waoga sana hatuko tayari kuchukua maamuzi mazito yatakayoipeleka mbele nchi yetu. Wapiga kura wanaogopa kuandamana wakiibiwa, Polisi wanaogopa kuwakamata wizi wa kura CCM, Mkurugenzi anaogopa kujaribu idea yake ya kuleta maendeleo mpaka aambiwe na IKULU, Ikulu wanaogopa kuwachukulia hatua mafisadi huenda watawalipua mabaya yao, Bado ili mradi ni kukimmbia risk tu japo inaweza kuwa na reward kubwa.

5. Long vs. short term orientation - This dimension describes a society's "time horizon," or the importance attached to the future versus the past and present

Tanzania tupo kwenye short term orientation Hatuna mipango ya muda mrefu na kama ipo ni kwenye makaratasi tu hakuna anayepata ptessure ya kuitekeleza. Nakumbuka zamani miaka ya 80s tulikuwa na mipango tunaita 2005, 2010, 2012 etc ikimaanisha mwaka huo kitu fulani kitakuwa kimefanyika, lakini mwaka ukifika tunakifuta kwenye porojo na kukisahahu kabisa. Poor focus
 
Aisee, uliyeanzisha thread hii nakushukuru sana na itakuwa vema kama member yeyote wa JF akapitia kwenye thread hii na kueleza kwa kifupi Username yake na maana yake.

GM7: Ni kifupi cha jina langu na ni mzaliwa wa miaka ya 197X, Kwa mfano jina langu ni Calcium Carbonate na kifupi chake ni CC kwa sababu nilizaliwa miaka ya 1970s nikaunganisha na kupata CC7

Nadhani mmenipata, wengine je?
 
Mzee 'Tusker bariiiidi' username yako ina-reflect we ni wale wa2 wa mitungi kwa sana tu. Lol. Wa2 ambao wao kila siku kwao ni weekend.
 

Naisadiki asili yangu na niliposoma kitabu cha bwana Richard Wright mwandishi mmoja wa fasihi za afrika-amerika kiitwacho, "The Native Son" nikagundua ningekuwa muhusika mkuu katika fasihi ile ni machache yaliyofanywa na weupe dhidi yetu ningeyavumilia bila shaka ningekuwa na mtazamo mkali zaidi nakufanya mambo kadhaa dhidi ya ukandamizaji wa watu wa magharibi na amerika ya kaskazini kwa waafrika. Kwenye JF likaanza jina la "The Native Son" kuashiria kuchukia unyanyasaji unaofanywa na mwafrika yeyote wakiwemo viongozi wetu wa kiafrika na Tanzania ambao wanasahau asili zao na kutukuza ugeni wakigeuzwa vibaraka na kuzidhurumu nchi zao kwa ufisadi mkubwa, bila shaka haibu iwe juu yao.

Nabaki hivyo.

dah! Mkuu umenigusa kumtima na hiyo riwaya. Dah! I read the novel & cudnt imagine. Walikuwa ni polisi elf 7 au 11 kama sikosei wakimsaka dogo. That was real the essence of internecine violence among blacks out there. Mfano wa hiyo violence ni pale ambapo mf. Mama ni ticha, then akala kichapo usiku au monie. Kwa vile hawezi kulipiza kwa mzee, basi madent wataipata. Big up kwa kuisoma. Mi mziwanda simply the last born
 
Mndundu kwa kifupi aliyebobea, kama hakiongei basi hakiwezi kumshinda....
 
Kama kuna baadhi mtapenda kuchangia kuhusu maana ya majina yenu na kama kuna sababu rasmi za kuamua kuyatumia majina hayo basi mnakaribishwa.
VeraCity (au Veracity) maana yake ni UKWELI.
Nimeamua kutumia jina hili kama kielelezo cha mwelekeo ninauotaka au ninaoamini na kuutumia.Uongo kwenye serious forums kama JF unaondoa maana nzima ya kuwepo kwa forum yenyewe.
 
....Hauxtable from the famous cosby show-Dr.Huxtable(Bill cosby),such an inspirational figure to listen to/watch THEN and NOW!!
 
I'm thirst for "mabadiliko" in our beloved country, but I decided to twist it a little bit.
 
Hili swali linawahusu wale ambao hawatumii majina yao ya kweli hapa ukumbini. Je, jina lako lina maana yoyote? Kuna sababu yoyote ile iliyokufanya uamue kutumia jina hilo!?

Nilikuwa nimeamua kutosema lolote kuhusiana na hali ya kisiasa ndani ya nchi yetu (kuwa bubu) pamoja na kwamba nilikuwa siridhiki na mambo mengi sana niliyokuwa nayasikia kwa Watanzania wenzetu, kuyashuhudia kwa macho au kuyasoma kwenye magazeti yetu mbali mbali. Niliamua kuwa kimya kwa sababu nilijua sauti yangu kama zilivyo sauti za Watanzania wengi ambazo hazisikilizwi na walio madarakani, haitafika kokote.

Mpaka nilipoanza kutembelea hapa miezi ya mwisho wa mwaka 2006 nikafurahishwa sana na michango ya baadhi ya wanachama na kuona hapa kuna sauti ya umma ambayo kama itaendelea na kushamiri basi itasaidia sana kuleta mabadiliko ya kweli ndani ya nchi yetu.

Nilibahatika kuwa Bongo kipindi cha kuapishwa Kikwete, pamoja na kuwa hakuwa amenigusa kama kiongozi mpya wa nchi yetu nilitiwa hamasa kubwa kuwaona Watanzania wenzangu wakiwa na shauku kubwa ya kumpata Kikwete kama Rais mpya wa Tanzania na weng walikuwa na matumaini makubwa toka kwake na wengine kumuita "Mkombozi wetu". Watu walipoanza kulalamika kuhusu utendaji wake kama Rais wa nchi, mimi nilikuwa nawaambia ni mapema mno kuanza kumlaumu. Niliomba apewe angalau kipindi cha mwaka mzima tangu aingie madarakani na hapo ndipo anastahili kuanza kutupiwa lawama mbali mbali kuhusu utendaji wake.

Basi nilipoamua kujiunga nikaamua jina la Bubu maana nilikuwa nimeamua kunyamaza kimya kwa miaka mingi pamoja na kutoridhishwa na mengi. Nikaukumbuka na ule wimbo wa 'Nginde ngoma ya ukae" Bubu ataka kusema mambo yanapomzidia. Ndipo baada ya mwaka na ushee tangu Kikwete aingie madarakani nikaamua rasmi kujiunga ili niungane na Watanzania wenzangu katika mijadala mbali mbali inayohusu hatima ya nchi yetu maana ile miezi 12 ilikuwa imekatika na kuvurunda kwa srikali ya Kikwete kulikuwa kunazidi kushamiri.

Hivi ndivyo jina BAK lilivyozaliwa rasmi na mnamo February 2007 nikajiunga rasmi na ukubi huu wakati huo ukiitwa Jambo Forums.

Kama kuna baadhi mtapenda kuchangia kuhusu maana ya majina yenu na kama kuna sababu rasmi za kuamua kuyatumia majina hayo basi mnakaribishwa.
2
Asprin= My real name.... yani kidonge chenyewe
 
Back
Top Bottom