MwanajamiiOne
Platinum Member
- Jul 24, 2008
- 10,470
- 6,562
Habari zenu wote wapendwa...........................
Rafiki wa dada yangu amekuwa akilalamika hivi majuzi kuwa mume wake,
amekosa uungwana/upendo na uvumilivu. Huyu dada pamoja na kuwa anaishi mbali na mume wake kutokana na majukumu ya kazi, lakini amekuwa akiisaidia sana familia kwa kugharamia matumizi yote ya nyumbani kuanzia chakula, matibabu, usafiri na mambo yote muhimu ya kimaisha.
Sasa amekuja kugundua kuwa mume wake anatembea na mwanamke mwingine,na isitoshe huwa anamleta mpaka hapo nyumbani. Mara baada ya huyu dada kugundua hayo aliona ni bora asitishe kupeleka fedha nyumbani, ukichanganya na hasira kidogo aliyokuwa nayo basi ndo hivyo tena. Pamoja na haya yote bado mumewe amekuwa ni mtu wa kumletea dharau sana na maneno yasokuwa na heshma. Lakini kwa jinsi huyu bwana asivyokuwa na haya, anazidi tena kumpigia magoti mkewe ili atume pesa za matumizi hapo nyumbani!
wanajamii,Je huu ni uungwana kweli?
mume anaamini kuwa bado ni siri yake,
na wala mke wake hajui hilo!!!!!!!
bacha hapo kwenye red umeniacha kidogo.........mkewe hajui hilo li-nini?
kama yeye kaka anajua kuwa affair yake bado ni siri, huyu dada hajamtendea haki na kwa vyovyote kureact bila kumjulisha mwenzio kwa nini unareact haisaidii sana sana mke atachukuliwa kama ana kiburi na majigambo kwa kazi yake na kuwa anamnyanyasa mumewe UNLESS amemjulisha kwa nini anareact hivyo anavyoreact.
Halafu mke anavyokatisha matumizi hapo nyumbani hakuna watoto/watu wanaowategemea?? au ndo nao wanakula adhabu kwa kosa wasilolijua??
bacha mshauri dada yako amwambie rafiki yake kuwa ni vema akamjulisha/mwonyesha mumewe kuwa anajua kuwa mumewe anacheat ama sivyo kibao kitamgeukia na yeye aonekane ana makosa.